Nifanyeje ili mke wangu ashike mimba haraka

Miezi sita ni muda mfupi sana kuanza kupanick. Wewe fanya tu baada ya miezi sita mingine ndiyo uanze kuwa na wasiwasi.
 
Dah ila maisha ukiwa singo ukipiga hata kimoko pakupunguzi haufiki mbali tayari ila kuna watu kweny ndoa miaka bila mimba
 
Huenda mnagegeduana siku ambazo sio za kushika mimba mkuu, simply fanya hivi.

Kaa na mkeo siku akiingia bleed hesabu siku 11 kuanzia hiyo siku aliyoanza kubleed ndio iwe day 1.... kuanzia siku ya 11 gegedaneni kama siku 10 hivi non stop asiposhika mimba wahi hospital jamaa yangu.
 
Kitabibu, miezi 6 bado siyo tatizo. Itachukuliwa kama tatizo iwapo baada ya mwaka 1 wa ngono bila kinga hakutakuwa na ujauzito. Kwa sasa hata ukienda hospitali km daktari anaijua kazi yake vizuri atawarudisha mkaendelee tu na mchezo mpaka mwaka uishe. Kama una wasiwasi na hali yako kwa sababu yoyote ile unayoijua, wahi kupima mwenyewe. Ni rahisi sana kumpima mwanaume kuliko mwanamke.

Fahamu mzunguko wa mwezi wa mwenzi wako. Kama uko regular (haubadiliki badiliki kila mwezi) basi ni rahisi kupata ujauzito (km nyote hamna tatizo). Akiingia mwezini, anza kumhesabia. Siku ya kwaza ya mwezi (kutoka damu) iwe 1, siku ya pili iwe 2, hesabu hivyo hivyo hata baada ya kutoka. Hata akitoka, endelea kuhesabu mpaka siku anaingia tena. Akiingia tena unaanza kuhesabu 1. Mzunguko wake kwa mwezi huo utakuwa siku zote ulizohesabu kuanzia siku ya 1 mpaka siku 1 kabla ya kuingia tena mwezini. Kwa shemeji yako hapa huwa ni siku 28. Kwa huyo wa kwako inaweza kuwa tofauti. Mhesabie tena mwezi wa pili, wa tatu, nk. Kama mzunguko wake ni regular hesabu yako itakuwa ni siku zile zile kila mwezi. Kwa shemeji yako hapa ni hiyo hiyo 28.

Sikiliza sasa jinsi ya kumpa ujauzito. Wanawake hutoa yai siku 14 kabla ya kuingia mwezini. Kama mwanamke ana mzunguko regular ni rahisi kujua hiyo siku ya 14 katika mzunguko. Wa kwangu mzunguko wake ni siku 28. Kwa hiyo siku ya 14 baada ya siku ya kwanza kwenda mwezini najua yai lake litakuwa tayari. Lakini kumbuka mbegu za kiume zinakuwa hai ktk mwili wa mwanamke hadi siku 3. Kwa maana hiyo hata ukiziweka ktk mwili wake siku 3 kabla ya yai kutelemka, bado kuna uwezekano wa kumpa ujauzito. Na yai nalo linadumu ktk mwili wa mwanamke hadi siku 3 hizi. Kwa hiyo siku zenye uwezekano wa ujauzito ni 7 katika mzunguko wa mwakamke. Siku 3 kabla ya siku ya yai kushuka, siku 1 ya yai kushuka na siku 3 baada ya kushuka. Ukiweka mbegu zako mwanzoni mwanzoni mwa siku hizo 7, uwezekano mkubwa ni mtoto wa kike. Ukiweka mwishoni mwisho, uwezekano mkubwa ni wa kiume. Mbegu ya X (ke) hutembea taratibu lakini haifi haraka. Mbegu ya Y (me) inakimbia haraka, kuchoka na kufa haraka.

Njia ya uhakika ya kujua km mkeo yuko tayari ni kutumia ovulation kit. Zinauzwa katika pharmacy lakini sina uhakika kama pharmacy za Bongo zipo. Inapima kwa njia ya mkojo na unaweza kuifanyia nyumbani wewe mwenyewe. Iko kama kipimo cha UKIMWI cha nyumbani. Ina maelekezo mazuri (kwa Kiingereza) ya jinsi ya kuitumia na kujua majibu yanapokuwa positive ama negative. Ikiwa positive unaweka mbegu siku hiyo ndani yake. Kwa sababu itakuwa gharama kupima kila siku katika mzunguko, inabidi ukisie siku zile za katikati katika siku zile 7 "hatari" ili upime mara 2-3 hivi na kupata majibu chanya.

Kuna watu wamesema fanya ngono naye kila siku. Hilo ni kosa. Mbegu kama zilivyo za mahindi, zinahitaji muda kukomaa. Kufanya ngono kila siku kunaweza kuwa na matokeo hasi kwa mtu anayetafuta mtoto.
 
Miezi 6 michache sana ukikaa mwaka si Ndo utazidi kupaniki.

Pole sana kwa changamoto hofu, Mashaka na Wasiwasi wakati uliopita, wakati wa sasa na wakati ujao ni kitu hatari sana kwa maisha ya mwanadamu .
 
huyo mke ana umri gani na wewe una umri gani tuanzie hapo kwanza,usije kua umeoa bikra wa mtoto wa miaka 9 kijijini huko alafu unakuja kulia lia hapa
 
Ratiba ya nini, apige kitu kila siku anaweza akabahatisha.
Hayo mambo sio ya kubahatisha mkuu, ndio maana kuna kalenda yake, kama kuna tatizo hata mfanye kila sekunde bado mimba haitaingia, na kama hakuna tatizo kwa kutumia kalenda ni mala moja tu!!
 
Cha kwanza mkapime afya ya uzazi wote wawili ibainike tatizo. Ni la Ke au Me mambo mengne yatafata mkuu
Mapema sana kuanza mambo ya kuwa na stress za kupima. Watulie wafurahie tu ndoa yao mimba itakuja yenyewe. Huyu kaanza stress mapema sana.
 
Habarini ndugu zangu.

Kama kichwa cha habari kinavyojieleza hapo juu.mimi mdogo wenu nimeingia kwenye ndoa mwezi wa kwanza mwaka huu,hadi sasa mimi na shemeji yenu tuna miezi 6 ya ndoa yetu .lakini mke wangu mpaka sasa navyoandika uzi huu hana dalili yeyote ya kuwa na mimba inaniuma sana kwa kweli...
Mwende hospital MKAPIME hormones zenu na Mambo mengine Kama mirija ya kupitisha mayai n.k baada ya Happ Kama Kuna tatizo Nipe majibu hayo pm nikuelekeze cha kufanya
 
Ratiba ya nini, apige kitu kila siku anaweza akabahatisha.
Jamaa anatakiwa apige mashine daily hadi kieleweke.Mimi mke wangu miezi sita ile ya mwanzo sikumbuki kama kuna siku ilipita bila kula mzigo.Siku za bleed pekee ndio nilikuwa na skip
 
Kunywa asplini sita na tangawizi nane then chemsha pili kichaa tisa changanya na maji halafu kunywa, then kunywa safari nne hala nenda kalale ukiamka utamkuta ana mimba
 
Back
Top Bottom