Nifanyeje baba yangu mzazi ajue kwamba mimi ni mwanae?

Nifanyeje baba yangu mzazi ajue kwamba mimi ni mwanae?

Uko sahihi, mtafute ba ako ili usahihishe makosa yaliyopita yaliyotendwa na wazazi wako, ni vema ukaiandika upya historia na asili yako kwa manufaa ya vizazi vyako vijavyo. wewe unaweza kuignore lakini wajao huwezi kuwasemea. How to do this, kaa na mama yako kwa upole na unyenyekevu muongee juu ya swala la baba yako halisi, ukimuonyesha kuwa huna nia mbaya na swala hilo ila unataka kuiweka sawa historia yako na ya watoto wako hata wajukuu, kwani ni wewe mwenye uwezo wa kuirekebisha historia hiyo. Tumia watu wazima waliopo kama vile mama yako mkubwa, mjomba, babu, bibi zako ili wakuonyeshe njia. siku hizi vipo hata vipimo vya DNA kama baba yako atakataa wewe si mwanae. Mwambie baba yako kuwa huna nia ya kutaka mali zake ila unataka kuweka sawa historia yako.
 
Da Mkubwa Nyamayao nimefurahi kukuona. Case yako wewe ni tofauti na pengine na ya gfsonwin pia but zipo case nyingine ambazo kwa sababu tu ya mazingira baba mzazi anakuwa amedhulumiwa haki ya kumjua mwanae. Na akaishia tu kusikia kuwa kuna mwanao sehemu flani na ikahappen na huyo mtoto akajua uwepo wa babake huyo, je hastahili kumfahamu? Hata kama huyo baba hana uwezo wa kumtafuta?
naamini wewe unaweza kujua ninafeel vipi.
hili swala nimelipotezea muda mrefu sana lkn kila nikilikataa linagoma akilini mwangu kabisa.
 
gfsonwin, take courage...... mtafute babako kimya kimya, usiweke matangazo kisha ukimpata mwonyeshe cheti cha kuzaliwa na ushahidi ulionao juu ya wewe kuwa mwanae mf. mahali alipokutana na mamako, wapi ulipozaliwa e.t.c. Baada ya hapo kuhusu kumwumiza mama au lah mfanye mama rafiki wa karibu sana, tena sana kisha pigeni story atafunguka tu. Unaweza kukaa nae, ukiwa na facts, ushahidi na ikiwezekana hata kile cheti cha kuzaliwa. Mwombe kwa upole akueleze ukweli, mhakikishie kuwa wewe huna nia mbaya. Msikie atasemaje. Maana inawezekana alitengwa na huyo babako, au mimba ilikataliwa na baba akasusa kabisa, mama atakueleza na utajua uchukue uamuzi gani . (Hivi ni wewe ulisema hauko karibu na mama au hujisikii kumpenda ?? Sikumbuki vizuri ile topic)
 
Last edited by a moderator:
na mimi siend kwake kisa ni waziri nina kwenda kwake kwasababu ni baba yangu. manake jamani miaka yote hii yupo tu hivi huwa anassume kitu gani juu ya mtoto wake?? ama ndo hivyo ukizaliwa na baba na asipomwoa mama yako basi wewe unafutwa kwenye ramani yake??

exactly, na hiyo ndiyo hasa sababu ya kumfata jiulize je, asingekuwa waziri usingemfata pia? au hicho kilemba cha uwaziri na umaarufu ndo kinakutisha wewe kumfata? Yeye ni mwanadamu kama wanadamu wengine huo umaarufu ni kilemba tu. hivyo mwambie hili swala baada ya kukubaliana na mama na baba yako lakini na wewe pia uwe psychologically ready kwa reaction yoyote atakayokuonyesha. DONT EXPECT A HUG.
 
gfsonwin, take courage...... mtafute babako kimya kimya, usiweke matangazo kisha ukimpata mwonyeshe cheti cha kuzaliwa na ushahidi ulionao juu ya wewe kuwa mwanae mf. mahali alipokutana na mamako, wapi ulipozaliwa e.t.c. Baada ya hapo kuhusu kumwumiza mama au lah mfanye mama rafiki wa karibu sana, tena sana kisha pigeni story atafunguka tu. Unaweza kukaa nae, ukiwa na facts, ushahidi na ikiwezekana hata kile cheti cha kuzaliwa. Mwombe kwa upole akueleze ukweli, mhakikishie kuwa wewe huna nia mbaya. Msikie atasemaje. Maana inawezekana alitengwa na huyo babako, au mimba ilikataliwa na baba akasusa kabisa, mama atakueleza na utajua uchukue uamuzi gani . (Hivi ni wewe ulisema hauko karibu na mama au hujisikii kumpenda ?? Sikumbuki vizuri ile topic)
nope sio mimi, ule uzi aliweka mdada mwingine jina nimesahau.
 
Mi nadhani mwenye neno la mwisho na wa kukuruhusu wewe kwenda kuongea na baba yako mzazi ni mama yako, usilazimishe jaribu kuongea na mama yako, ina wezekana baba yako wa kambo anajuala bda walikuficha jambo hili kwa sababu za malezi.
 
gfsonwin, take courage...... mtafute babako kimya kimya, usiweke matangazo kisha ukimpata mwonyeshe cheti cha kuzaliwa na ushahidi ulionao juu ya wewe kuwa mwanae mf. mahali alipokutana na mamako, wapi ulipozaliwa e.t.c. Baada ya hapo kuhusu kumwumiza mama au lah mfanye mama rafiki wa karibu sana, tena sana kisha pigeni story atafunguka tu. Unaweza kukaa nae, ukiwa na facts, ushahidi na ikiwezekana hata kile cheti cha kuzaliwa. Mwombe kwa upole akueleze ukweli, mhakikishie kuwa wewe huna nia mbaya. Msikie atasemaje. Maana inawezekana alitengwa na huyo babako, au mimba ilikataliwa na baba akasusa kabisa, mama atakueleza na utajua uchukue uamuzi gani . (Hivi ni wewe ulisema hauko karibu na mama au hujisikii kumpenda ?? Sikumbuki vizuri ile topic)

my dear wala sitaki kufanya publicity nataka iwe btn mm na yy ama familia yake na familia niliyozaliwa basi.
nitafurah sana japo kuliskia neno lake liwe baya ama zuri lkn nitakuwa nimesha tua mzigo mzito nafsini mwangu
 
Mi nadhani mwenye neno la mwisho na wa kukuruhusu wewe kwenda kuongea na baba yako mzazi ni mama yako, usilazimishe jaribu kuongea na mama yako, ina wezekana baba yako wa kambo anajuala bda walikuficha jambo hili kwa sababu za malezi.

yawezekana kabisa iyo ikawa ni sababu yao na hili sina tatizo lake kabisa.
 
gfsonwin

Hilo ni tatizo kubwa sana na wala si dogo kuliko linavyoonekana.

Ushauri wangu ni kuwa, kabla ya kuchukuwa uamuzi mwingine wowote inabidi kwanza uongee na mama'ko mzazi kuhusu hili ili akuweke wazi ni nini kilitokea mpaka wewe akakuficha. Baada ya kuongea nae ndio utajuwa cha kufanya. She is the most important player in your saga.
 
Last edited by a moderator:
my dear wala sitaki kufanya publicity nataka iwe btn mm na yy ama familia yake na familia niliyozaliwa basi.
nitafurah sana japo kuliskia neno lake liwe baya ama zuri lkn nitakuwa nimesha tua mzigo mzito nafsini mwangu
Da gfsonwin, iwe ni wewe na yeye tu, akiamua kuihusisha familia yake ni yeye but cha muhimu ni wewe na yeye kwanza. Mimi wa kwangu nilimfuata (may be tofauti ni kuwa sio mtu maarufu) so haikuwa shida mara tu baada ya kujua location zake nikaenda na cha ajabu aliponiona tu alisema .......' Hatimaye ile siku niliyoisubiri kwa hamu imefikia, nilijua kuwa sitakufa kabla sijakuona' kwangu yalikuwa maneno ya faraja ambayo mpaka sasa sijawezamwuliza ilikuwaje. Sisemi kuwa nawe itakuwa rahisi sana unawezakutana na maswali ya kukera yakitaka kuthibitisha uhalali wako but take heart, na uwe tayari kwa lolote.
Believe me hata kama atakukana, but utakapoondoka utakuwa umeiridhisha nafsi yako na yeye kama alipita kwenye hizo anga basi dhamira itaongea naye. But, nasisitiza but, mtangulize MUNGU katika yote, mwombe akuonyeshe the right way. I did, na nilipewa majibu kuwa nenda, all shall be well with you, so I went.
 
Last edited by a moderator:
  • Thanks
Reactions: Mbu
gfsonwin

Hilo ni tatizo kubwa sana na wala si dogo kuliko linavyoonekana.

Ushauri wangu ni kuwa, kabla ya kuchukuwa uamuzi mwingine wowote inabidi kwanza uongee na mama'ko mzazi kuhusu hili ili akuweke wazi ni nini kilitokea mpaka wewe akakuficha. Baada ya kuongea nae ndio utajuwa cha kufanya. She is the most important player in your saga.

thanks for this my dearest........ukweli nauona uakubwa kwa sasa na jins ambavyo linaweza kuwa na impact kwa wengine
 
Da gfsonwin, iwe ni wewe na yeye tu, akiamua kuihusisha familia yake ni yeye but cha muhimu ni wewe na yeye kwanza. Mimi wa kwangu nilimfuata (may be tofauti ni kuwa sio mtu maarufu) so haikuwa shida mara tu baada ya kujua location zake nikaenda na cha ajabu aliponiona tu alisema .......' Hatimaye ile siku niliyoisubiri kwa hamu imefikia, nilijua kuwa sitakufa kabla sijakuona' kwangu yalikuwa maneno ya faraja ambayo mpaka sasa sijawezamwuliza ilikuwaje. Sisemi kuwa nawe itakuwa rahisi sana unawezakutana na maswali ya kukera yakitaka kuthibitisha uhalali wako but take heart, na uwe tayari kwa lolote.
Believe me hata kama atakukana, but utakapoondoka utakuwa umeiridhisha nafsi yako na yeye kama alipita kwenye hizo anga basi dhamira itaongea naye. But, nasisitiza but, mtangulize MUNGU katika yote, mwombe akuonyeshe the right way. I did, na nilipewa majibu kuwa nenda, all shall be well with you, so I went.

thanks my dearest!!!!!!!!!! yaani hujui tu jins unavyonitia moyo na sasa naanza kuuona wepesi fulan nafsini.
stay blessed my dearest.
 
gfsonwin

Hilo ni tatizo kubwa sana na wala si dogo kuliko linavyoonekana.

Ushauri wangu ni kuwa, kabla ya kuchukuwa uamuzi mwingine wowote inabidi kwanza uongee na mama'ko mzazi kuhusu hili ili akuweke wazi ni nini kilitokea mpaka wewe akakuficha. Baada ya kuongea nae ndio utajuwa cha kufanya. She is the most important player in your saga.
gfsonwin

Hilo ni tatizo kubwa sana na wala si dogo kuliko linavyoonekana.

Ushauri wangu ni kuwa, kabla ya kuchukuwa uamuzi mwingine wowote inabidi kwanza uongee na mama'ko mzazi kuhusu hili ili akuweke wazi ni nini kilitokea mpaka wewe akakuficha. Baada ya kuongea nae ndio utajuwa cha kufanya. She is the most important player in your saga.

Da FaizaFoxy uko sahihi kabisa, hili ni la muhimu sana. But naomba utoe na ushauri wa what she should do kama mama atakataa kumjibu ukweli? Kuwa amwulize mama na bado mama akagoma kusema ukweli (au hata uchungu alionao juu ya hili). Mimi ilinitokea na kama ilivyokuwa kwa gfsonwin nilibahatika kuona cheti change cha kuzaliwa (ambacho nacho kilikuwa na jina la uwongo-na halikuwa la baba mlezi) but sikukichukua wala kuwa nacho kama reference so nikaishia kumwuliza mama kwa mdomo, the only jibu nlilopata ni kuwa hapana umekosea babako ni huyu............ (Ingawa kwangu tofauti ilikuwa ni kwamba ndugu wa baba mlezi walionyesha wazi kuwa mie si damu yao na wengine walikuwa wakisema kabisa)........
 
Last edited by a moderator:
,,,...Mimi sidhani kama kuna umuhimu wowote wa wewe kumtafuta baba yako ambaye hajawahi kukutafuta hata siku moja tangu uzaliwe!!!
...,,Tambua kwamba lazima kuna sababu ya maana kwanini mama yako mzazi hajakwambia mpaka sasa kuhusu biological father wako kama kweli huyo ndiye(i.esikubaliani na rizon uliyoitaja ya jeshini)!!
...,,Alieykulea ndiyo mzazi wako katika dunia hii,hivyo kwa mtazamo wangu suala la kumtafuta unayedhani ni biological father wako kimyakimya bila hata kumshirikisha mama yako mzazi itakuwa ni kama dharau kwake yeye na huyo unayemuona si baba yako!!!
...,,Jiulize swali moja,,Hivi itokee mume wako kakubali adopt mtoto ambaye lets say biological father wake alikukana/alimkana mtoto na kukuacha from ze moment umemwambia una mimba yake,zen mwanao kakua kakutana na ''wambea'' kama ulivosema,wakampa true story zen aamue kumtafuta biological father wake bila kukupa taarifa wewe wala mumeo sijui utajisikiaje..,,???
...,,NA KWANINI HAYA MATATIZO YA KUWATAFUTA BIOLOGICAL PARENTS WALIOWAKANA WANAO YAKO SANA KWETU WAAFRIKA UKILINGANISHA NA DUNIA NYINGINE AMBAKO MTOTO ANAMKANA MZAZI WAZIwazi ANAYEJIFANYA KUJILETA LATE IN LIFE!!??,,..
,,,..N wonder everybody is too afraid of adopting in our countries,sabu mwisho wa siku mtoto akimaliza chuo na kupata kazi anakukimbia na kumtafuta baba/mama ambaye maybe alimkana kama si kumtupa jalalani kabisa baada ya kuzaliwa akaokotwa na wasamria wema,,..!!
 
Pole sana, ni haki yako kujuana na baba yako mzazi kama kweli ndiye. Lakini nakushauri uwashirikishe mama na baba mlezi kile unachokusudia pengine watakwwambia ukweli wote na baada ya hapo waweza kuchukua uamuzi wa kuonana nae au kuacha. Rafiki yangu alikutwa na mkasa kama huu ambapo baba mlezi alikuwa tayari kumwambia hata kabla yeye hajaujua ukweli kama yule baba si baba mzazi (si kwamba alikuwa hampendi wala kumjari) lakini mama hakuwa tayari kumwambia mtoto kitu kilicho leta mtafaruku kidogo, mwisho wa siku baba mlezi alijitosa akamwambia ukweli ndipo mama akawa hana jinsi tena kuendelea kuficha. So baba wa mtoto aliambiwa na akawa tayari kuonana na bintiye wakaongea na siku zilivyosonga akamtambulisha kwa familia (coz ameoa na anawatoto) na yule dada aliendelea kuishi kwao (alipokulia). Mama wa rafiki yangu alifariki miaka mitatu iliyopita, najaribu kufikiri kama asingemwambia binti ukweli na kumkutanisha na babaye angemwacha binti na majonzi makubwa. I support you kutaka kuonana na baba mzazi lakini itakuwa vyema ukiwashirikisha hao waliokulea kwanza. All the best
 
Da FaizaFoxy uko sahihi kabisa, hili ni la muhimu sana. But naomba utoe na ushauri wa what she should do kama mama atakataa kumjibu ukweli? Kuwa amwulize mama na bado mama akagoma kusema ukweli (au hata uchungu alionao juu ya hili). Mimi ilinitokea na kama ilivyokuwa kwa gfsonwin nilibahatika kuona cheti change cha kuzaliwa (ambacho nacho kilikuwa na jina la uwongo-na halikuwa la baba mlezi) but sikukichukua wala kuwa nacho kama reference so nikaishia kumwuliza mama kwa mdomo, the only jibu nlilopata ni kuwa hapana umekosea babako ni huyu............ (Ingawa kwangu tofauti ilikuwa ni kwamba ndugu wa baba mlezi walionyesha wazi kuwa mie si damu yao na wengine walikuwa wakisema kabisa)........

Inatakiwa kwanza aongee na mama kama ulivyofanya wewe, baada ya kuongea nae ndio itajulikana cha kufatilia.

Kumbuka, haya mambo huwa yana "impact" kubwa sana sana "psychologically" kwa wote na nnamuelewa mum wako aliposema "babaako ni huyu". Kuna uwezekano kuwa hao ma baba wazazi waliwakataa kabla hamjazaliwa na mama anaona kwanini leo ibadilike? ni mambo ambayo yanahitaji subira na uvumilivu wa hali ya juu sana.

Kwa haya tunayoyasikia humu ndio tunaelewa kwanini tunaamrishwa tuoane na tusifanye zinaa. Na hizi sio kesi "unique" zipo nyingi sana tena sana, watu hawana pa kuziongelea.

Hapa inabidi tuwapongeze wote walio na moyo wa kuweza kuyamwaga humu. Nna uhakika kuna ahueni fulani inayopatikana kisaikolojia.
 
Back
Top Bottom