Nifanyeje baba yangu mzazi ajue kwamba mimi ni mwanae?

Nifanyeje baba yangu mzazi ajue kwamba mimi ni mwanae?

rafiki yangu EMT.....
nimekusoma saana na post yako ndeefuuu. Umejitahidi sana kumfanya gfsonwin aone anachotaka kukifanya ni haki yake na ni faraja kwake. well, ni mtazamo pia....
najua rafiki unajua kabisa gfs siyo mtoto wa kwanza kukataliwa na babake, wapo wengi sana, na sidhani kama kati ya hao woote waliokataliwa au ambao hawajui baba zao wameweza kukwepa kuoana, tena nina uhakika kuna watu wengi tu ambao wameoana mtu na dadake, sidhani kama hayo matatizo ya kiafya yanawakuta.
Na kuhusu gfs kuendelea kuumia kwa ajili ya wengine, mimi sidhani kama hili litamuumiza sana gfs kiasi cha kusema akadead au kuzimia..... yeye ni mtu mzima, kijana, ana nguvu, ni swala tu la kwenda kwa counsellor mara kadhaa na atapona. je ameshamfikiria mamake na babake ambao ni wazee sasa? je akienda kuwaambia anamtafuta baba waziri na babake mzazi akapata hear attack kwa ajili hiyo? unajua mzazi atawaza nini? kwamba labda sikuweza kumfanyia mambo anayotaka ndo maana anatafuta babake, au labda kuna kitu nimefanya ndo maana anatoka. unafikiri baba ataamini kuwa anataka ajue kuwa anaishi tu? hakuna jingine? sidhani kama baba atalikubali hilo.
All in all, afwate moyo wake. kama anaona amani ya moyo wake ni muhimu zaidi kuliko ya waliojitolea kwa ajili yake, fine..
sisi wote ni watu wazima na tunajua kabisa sadaka ni nini..... tena tunatoa sadaka kubwa sana kila siku sababu tu ya kuwakinga watu tunaowapenda na kuwajali sana. sidhani kama gfs atajisamehe akija kuona kwa sababu ya ubinafsi wa moyo wake tu, kawaumiza watu waliokuwa wamejitolea sadaka kubwa sana katika kuhakikisha amekuwa hivyo alivyo
mawazo mazuri sana.......naye atoe sadaka tu kwa kutomtafuta huyo baba......binafsi heri amani ya moyo nisipate lakini nisimuumize baba mlezi mana kitendo alichonifanyia ni kikubwa sana.......si unajua mtoto anavyosumbua mara kuumwa...sijui kafanyaje.....baba wa watu kahangaika weee na leo amefikia hapo alipo anataka kumjua baba aliyeshindwa kufanya hayo yote........binafsi simshauri hata......naye aitoe nafsi yake kwa ajili ya wazazi wake haswa baba mlezi....
 
sijamanaisha kwamba nataka kumkwaza.
nachojiuliza mbona wewe ulimtafuta?? je ulikuwa unayawaza haya kama unayosema?? sijasema nataka kujitenga nae na toka anilee na nijitegemee hakuna anayepokea heshima ya baba zaid yyake yy.

lkn nina haki ya kuiskia hata kauli ya baba yangu mzazi juu yangu mimi..............na siwez kusema nisimtafute kisa eti nitamvunjia heshima baba mlezi hapana manake hiyo sio lengo langu.

hivi kwani kilikuwa kipi rahisi?? mimi kukubali ubini wa baba mzazi mpaka leo ama kuukana nilipoona maisha nayamudu??

sikumtafuta baba yangu, na sikuwahi kujua anaishi wapi, mama kama angependa angetuambia, lakini na yeye alipiga kimya,na sikuwa na haja ya kumtafuta, kwa kuwa hakutupenda na sisi hatumpendi, sasa ndugu zake wakaamua kututafuta, ndo hao wakawa wanatoa habari baba yenu amefariki, mara baba yenu aliacha ardhi ya urithi, hakuna anaewajali, wakae na mali za baba si ndo aiwapenda bana,
 
toka mama ana mimba yangu, aliandika jina la baba ni yeye na nilipozaliwa kabla sijabatizwa niliitwa kwa jina lake but nilipobatizwa baada ya kuwa tayari mama anaish na baba mlezi nilitumia jina la baba mlez na mpaka wa leo ndilo nitumialo.

sina nia mbaya ya kuruin maisha ya mtu yyte na natamani hata nitumie njia ya mimi na yeye tu ili akikubali/akikataa iwe poa lkn niwe nimetua mzigo ulioko nafsini mwangu basi.

Rafiki, kwanza pole.

Kitendawili hiki kwa sehemu kubwa anayeweza kutengua vizuri ni mama yako. Kuna maswali kadhaa yeye ndiye anaweza kuyajibu kwa ufasaha.

Je baba mlezi anajua kuwa wewe sio mwanae wa kumzaa? Kama jibu ni ndio, wewe umejuaje kuwa anajua hivyo?

Suala lingine, ambalo, naamini ni la muhimu zaidi ni sababu za mama yako yeye mwenyewe kutokukwambia ukweli kuhusu baba yako (umesema uliambiwa na mama mdogo!). Je alifanya makusudi au ni kweli pengine mpaka sasa hivi hajajua kwa uhakika baba yako ni yupi - kati ya huyo "mlezi" na huyo "mzazi". Kwa namna ulivyoeleza, naona kuna uwezekano kuwa mama alikuwa na mahusiano na wote kwa wakati mmoja. Suala la kuandika jina fulani kwenye kadi ya clinic kwa maoni yangu bado sio "litmus" kwa sababu hata kama by then mama alikuwa hana uhakika baba wa mtoto ni yupi, kwenye kadi angetakiwa kuandika la mmoja tu.

Kwa namna ulivyoelezea hapa jamvini, wewe unaamini kuwa huyo baba yako mzazi hajui kama wewe ni mwanae. Assuming baba mlezi anajua kuwa wewe siye mwanae, je mama na baba yako mlezi walikuwa na makubaliano gani kukuhusu na kuhusu "haki na wajibu" wa huyo baba mzazi? Je kuna uwezekano kuwa mama alimdanganya baba mlezi kuhusu uwepo wa baba yako?

Mimi nisingekushauri hata kidogo kufanya chochote bila kwanza kupata ukweli au maelezo ya mama yako moja kwa moja kutoka kwake. Kama baba "mlezi" hajui kuwa wewe sio mtoto wake wa kumzaa, then nadhani ni tatizo kubwa zaidi.
 
nakumbuka kuna siku Zinduna sijui aliitisha mtanange wa kukusuta kule cc.....
kulikuwa na group la wasutaji wakikusuta, wakaishia kusutwa wao, lol! angalau sikuwepo kwenye huo msuto.....
sasa hapa najua hata tukisema vipi umesha-make up your mind........
nenda kaonane na mheshimiwa Waziri.... ila hala hala asiwe MUME WANGU, lol! nilishamuahidi akileta mtoto wa nje nitampigia amle, kwa hiyo chunga sana...
cc. snowhite, cacico, Kaunga .......
utajiju, usije tu kuja kutafuta :help: hapa

hongera shostito kumbe umeolewa na waziri??
sasa mnataka mnisute kisa nimemtafuta baba yangu??
 
huo ni ushauri tu! Kam umeshamake your mind kuwa ni lazima umtafute basi usingekuja kuomba ushauri, nasema hivi, coz i knw how it feels especially kwa huyo baba aliyekulea! Huyo unayemtafuta if at all ni true his blood, he only knew to pour his ......... Leave, 9sorry to say this) tena kama mimi ni wwewe hata wazo la kumfikiria nisingekuwa nalo, coz he doesnt worth it, he doesnt even worth kuwa my waste! I hate cowards!
hapa wote tunamsemea huyo baba mlezi, yaani sitamani tu kuwa kwenye shoes zake maana ningeumia sana. siyo jambo rahisi kuona mtoto uliyemlea anakuja kukuonyesha dharau kiasi hiki. gfsonwin ukubali au ukatae, kitu cha kwanza babako atachokifikiria ni kwamba unafanya hivi sababu unaona huyo bio father ni zaidi yake, isingekuwa hivyo wala usingemtafuta. msome sana snowhite! nadhani mimi namwelewa sana sijui kama wewe mwenzangu unamwelewa kama ambavyo mimi namwelewa.... sasa kama upo tayari kumuumiza babako kiasi hiki sawa, go ahead.
 
Last edited by a moderator:
Namshukuru Mungu mie muoga hasa wa rejection. Na inanilinda haswa. Na kufungua 'can of worms' sithubutu.

Ukiona miaka hii yote mamako amevumilia kutokukuambia hata kwa bahati mbaya, na babako hajakutafuta hata kwa bahati mbaya, basi iko namna. Pole sana kwa kuwa njia panda dada. Japo natamani ungempotezea tu. Na huo uwaziri wake tena ndo atakuumiza kabisa. Hakusikia hata bintiye anaolewa jamani?
Hakika kuna jambo limejificha; mara nyingi kwa mila zetu za kiafrika, harusi za watoto ndio huwa zinaunganisha wazazi....ni kitu gani kilitokea hadi hata baba mzazi akashindwa kuhudhuria au hata kutoa baraka kwa bintie. This is more than a can of worms!!
 
hongera shostito kumbe umeolewa na waziri??
sasa mnataka mnisute kisa nimemtafuta baba yangu??
nilikuwa nakumbushia tu ule msuto, na kusema kwamba hukubali kushindwa.....
hili pia hutashindwa hata tukikushauri vipi......
 
mawazo mazuri sana.......naye atoe sadaka tu kwa kutomtafuta huyo baba......binafsi heri amani ya moyo nisipate lakini nisimuumize baba mlezi mana kitendo alichonifanyia ni kikubwa sana.......si unajua mtoto anavyosumbua mara kuumwa...sijui kafanyaje.....baba wa watu kahangaika weee na leo amefikia hapo alipo anataka kumjua baba aliyeshindwa kufanya hayo yote........binafsi simshauri hata......naye aitoe nafsi yake kwa ajili ya wazazi wake haswa baba mlezi....
kumbe umekua mdogo wangu, lol!
 
  • Thanks
Reactions: BAK
hapa wote tunamsemea huyo baba mlezi, yaani sitamani tu kuwa kwenye shoes zake maana ningeumia sana. siyo jambo rahisi kuona mtoto uliyemlea anakuja kukuonyesha dharau kiasi hiki. gfsonwin ukubali au ukatae, kitu cha kwanza babako atachokifikiria ni kwamba unafanya hivi sababu unaona huyo bio father ni zaidi yake, isingekuwa hivyo wala usingemtafuta. msome sana snowhite! nadhani mimi namwelewa sana sijui kama wewe mwenzangu unamwelewa kama ambavyo mimi namwelewa.... sasa kama upo tayari kumuumiza babako kiasi hiki sawa, go ahead.
dah!! ninashindwa kuelewa kwann nyie mnaona kwamba naenda kwasababu ya ubosi wake. hivi Fixed Point unafikiri ubosi wake unanifaa nini mimi kwasasa?? je wakiitwa wote wawili yupi atakaye aibika kati ya huyu mlezi ama huyu mzazi??

ingekuwa ni wkasababu ya uwaziri ningeenda alipoteuliwa miaka 10 iliyopita na mpaka sasa nilichukulia poa kabisa na najua soon ataretire na hivyo ubosi wake hauna impact yyte kwangu.
baba mlezi wangu hajawah kukosa chochote toka kwangu, na heshima ya baba anaipata yy period ila tu binafsi nafikir kulifumba hili moyoni linaniua kimya kimya
 
Last edited by a moderator:
huu uzi unanitisha guests wako wengi sana sijui na wenyewe wana fall kwenye cases kama yangu ama??pengine na baba mwenyewe anasoma pasi mm kujua mweeeh!!!
 
Mtafute uongee nae, pengine hana taarifa zako maybe angekua nazo angekutafuta na kukurecognize kama mwanae,yule ndio baba yako mzazi no matter what na his blood is flowing in your vain sasa kwa nini ujidanganye sio baba yako

Tafuta privacy nae umweleze na umwambie dhumuni lako ni kutaka tu ajue wewe ni mwanae thats all,am sure akikuona wewe ni mtu civilised wala haitampa shida maana huonekani kama mtu wa kutake advantage yeyote from whom he is, probably atakutambulisha hata kwa wanafamilia wengine mjuane bila kinyongo chochote.

Wewe ni mtu mzima dadangu do it kiutu uzima besides kujaribu ni bora kuliko kutojaribu kabisa (na pengine kuna sababu za msingi kbs zilizomfanya ashindwe kukutafute you never know so just explore the truth)
 
huu uzi unanitisha guests wako wengi sana sijui na wenyewe wana fall kwenye cases kama yangu ama??pengine na baba mwenyewe anasoma pasi mm kujua mweeeh!!!

Neno 'waziri' litakuwa limevuta nadhari za wengi na kuacha maswali vichwani mwao.
 
Duh Kiranga sijui kwanini nafsi yangu imeshaanza kumuhukumu Waziri wa nchi ofisi ya Rais Utawala bora.

Mpaka sasa ushamuharibia.Tena si yeye tu, umewaharibia mawaziri wote wana wingu la suspicion.Kila nikimuona waziri wa Tanzania nitakuwa najiuliza "sijui ndo huyu baba yake rafiki yetu aliyemtelekeza kwa miaka yote hii"?

Mapaparazzi washaanza kupekua, usishangae kesho headline kuwa

"Waziri mwenye mtoto aliyemtelekeza kwa miaka 30 anatafutwa na mwanawe".

Habari kutoka vyanzo vyetu vya habari vya kininja vinasema ni Waziri wa kutoka mkoa ____

Unashangaa anatajwa kwa sifa zote mpaka inakuwa kama wamemtaja jina.

Utakuwa bado hujamharibia tu?
 
Last edited by a moderator:
swali zuri sana hili.
bada ya kuambiwa na watu nikachunguza kwa mama nikakuta ni kweli ingawa mama hakuniambia yy.
niliambiwa na mdogo wake na mama (ma'mdogo) ukweli na alinionyesha hadi picha ya baba ambazo walipiga na mama wakati wako na uhusiano. kutoka hapo nikaanza kuangalia nilivyosadifu na ndugu zangu nikagundua kuna utofauti mkubwa sana.

lkn pia nilipochukulia tarehe ya mama kufunga ndoa na niliyozaliwa iliacha gap kubwa sana na niliwah kuisoma kadi ya mama ya kliniki akiwa na mimba yangu iliandika jina la huyu baba mzazi. sijawah kumwambia mama hili manake niliiona kwa bahati mbaya tu kabatini mwake.

istoshe niliambiwa kwamba nilipozaliwa aliambiwa ila kwasabau ya system ya jeshi ya wakati huo hakuweza kusema juu ya hatma yangu, so alimwacha mama kwenye wakati mgumu sana na hapo ndipo walipopotezana kimawasiliano.

Mpotezee huyo Waziri hakupendi hata chembe.
 
Mtafute mapema mueleze ukweli.. akae akijua hali halisi si mpaka mtu anapofariki ndio ujitokeze.. we mueleze mapema usikie kama atakukubali au lah..
 
huu uzi unanitisha guests wako wengi sana sijui na wenyewe wana fall kwenye cases kama yangu ama??pengine na baba mwenyewe anasoma pasi mm kujua mweeeh!!!
hao guests wasikutishe, wametokea fb
 
  • Thanks
Reactions: BAK
mimi am not sailing with you!
NATAKA KWENDA KUMSINDIKIZA KWA MSHUA!
japo niwe tu kweny basement floor nikimsubiri ashuke twenzetu tukapige zanzi na strawberry lips!
ha haa, kwa raha zako mdogo wangu......
halahala muende na helmet.... siku hizi ni acid tu
mpaka hapa wake wa mawaziri watu wazima wote wameshaorder acid
 
Back
Top Bottom