Nifanyaje ili mbwa wangu awe mkali!? Naomba ushauri

Nifanyaje ili mbwa wangu awe mkali!? Naomba ushauri

VPN USED2020OCTOBER28

JF-Expert Member
Joined
Oct 27, 2011
Posts
1,505
Reaction score
676
Mimi Nina mbwa ni anapata msosi Wa kueleweka sana na analala sehemu nzuri sana. Sasa ni kwamba mbwa wangu sio mkali hata kidogo!

Sasa naombemi msaada Wa ushauri wenu ni mlishe nini ili awe mkali!! Naombeni ushauri wenu wadau maana ninampenda sana mbwa wangu!

Karibuni washika dau na poleni na majukumu ya kila Siku!!! Karibuni kwa jukwaaaa
 
Mbwa kuwa mkali inategemea ulivyomfuga km ni mkubwa lakini km bado mdogo jaribu kufanya asizoee kila mtu uwe unamfungia awe na mda maalum wa kufunguliwa
 
Mchanganyie msokoto na nyamaa mkuu...unauchambua fresh afu unamchanganyia na nyamaa...
 
Usimzoeshe kumfungua mchana labda kama unamuogesha...mpe chakula mara moja tu usiku ukimfungulia..mpe chakula ila at least mara moja nyama na mifupa kutest meno yasilemae na softfood....halaf ujaribu kuwa una msemesha matendo kama kukamata au kuacha kufanya kitu....zingatia itasaidia...ila inategemea na aina ya mbwa ulikomtoa...kama ile jamii flan inayoshinda sebulen kwa Wema Sepetu hawezi kuwa mkali hata ukimvutisha bange ndo atazidisha usingizi
 
Kuna sehemu Mwenge niliona bango la mwalimu wa mbwa (dog trainer) inawezekana wao wanajua sababu za kitaalam zinazomfanya mbwa awe mkali au mpole kesho nikipita nitasoma namba yake nitaileta hapa. Ila moja ya basics ni kumtenga,asiwe ana mazoea na watu awe anafungiwa mapema alfajiri na kufunguliwa usiku si chini ya saa nne,niliwahi kuwa na mbwa nikiwa mdogo mbinu hii ilinisaidia japo matokeo hayakuwa mazuri kama nilivyotaka. Wengine waliniambia mbwa hatakiwi kula vyakula vilivyoungwa na vyenye chumvi, wengine ndo kama mkuu dabo wakadai niwape bange ila zote hizi hazina uhakika na ni kama imani tu (myth). Mbwa umpe bange akiwa kichaa akakudhuru wewe mwenyewe utasemaje?
 
Last edited by a moderator:
Usimzoeshe kumfungua mchana labda kama unamuogesha...mpe chakula mara moja tu usiku ukimfungulia..mpe chakula ila at least mara moja nyama na mifupa kutest meno yasilemae na softfood....halaf ujaribu kuwa una msemesha matendo kama kukamata au kuacha kufanya kitu....zingatia itasaidia...ila inategemea na aina ya mbwa ulikomtoa...kama ile jamii flan inayoshinda sebulen kwa Wema Sepetu hawezi kuwa mkali hata ukimvutisha bange ndo atazidisha usingizi

Ningekupa like mkuu,ila sehemu nyingine button ya like haionekani sijui kuna shida gani.
 
Back
Top Bottom