Nifahamisheni viwanda hivi viko wapi?

Nifahamisheni viwanda hivi viko wapi?

lee Vladimir cleef

JF-Expert Member
Joined
Feb 5, 2013
Posts
9,571
Reaction score
35,481
Utakubaliana na mimi kuwa Tanzania ilikua ina viwanda makini,na kama vingeendelezwa na kuwadhibiti viongozi wake waliokua wanaviendesha vibaya leo hii nchi yetu ingekua mbali kiuchumi na ingekua ni nchi ya viwanda? pengine ingekua kuikaribia south afrika?unakubaliana na mimi kuwa sera ya ubinafsishaji ilifanyika hovyo?

Kama ingefanyika vizuri leo hii tungekua hatukopi hata senti tano nje? sasa niambie viwanda vyetu viko wapi je unajua kuwa tulikua na kiwanda cha kutengeneza BISKELI zilizoitwa SWALA.Na hivi viko wapi? TAMCO kuunganisha SCANIA,General tyre kutengeneza magurudumu,Urafiki,Mwatex,Sungura tex,Mutex,Kilitex hivi vilitengeneza nguo,kiko wapi kiwanda cha kutengeneza majembe cha ubungo,Matsushita kilitengeneza radio,Tanganyika Parkers kilisindiks nyama za kopo,TIPER kilisafisha mafuta ghafi,Tz railways corporatiion na AIR TZ Corporatio hivi vilisaidia sana usafirishaji sio viwanda,Iko wapi Valmet.

Viko wapi wapi viwanda vyetu vya kutengeneza juice,tangold,liko wapi shirika la TZ Elimu suupplies,viko wapi viwanda vya sabuni za Gardenia,Lumi,Lux au hizi zilitoka nje?Unajua kiwanda cha chuma MANG'ULA,Viko wapi viwanda vya kuprocess pamba,tumbaku,chai,kahawa,katani na sukari?kiko wapi kwanda cha viatu Morogoro shoes na BORA,hivi ni vichache tu ndg zangu.

Je tangu zama hizo tusingekua tumeongeza vingine? Mwadui na Tancut almasi bado vyetu?nikumbusheni jamini bado vipo? na vingine vya siri na visivyo vya siri nimevisahau.tukumbushane tupate uchungu na nchi yetu.hii gesi haya madini tungeweza kuchimba wenyewe tu.unakikumbuka kiwanda cha mbolea Tanga TFC na kiwanda cha kutengeneza filamu ( sinema) TZ FILIM CORPORATION,hiki kisingewafaa akina Marehemu Kanumba,RAY,JB,na wengineo?Viwanda vingi China ni mali ya umma na sasa China ni world second largest economy.

Tukumbuke.
 
mitambo iliuzwa chuma chakavu vingine vingi sana viligaiwa kwa wahindi na waarabu wakavigeuza magodown
 
Hapa hutapata wachangiaji.
Sikuhizi maswali haya hayana majibu.
 
Kama vile ulikuwa umefariki miaka ya themanini hivi...ukafufuka leo! Hiyo ndiyo Tz bwana..chezea ccm wewe!!
 
Utakubaliana na mimi kuwa Tanzania ilikua ina viwanda makini,na kama vingeendelezwa na kuwadhibiti viongozi wake waliokua wanaviendesha vibaya leo hii nchi yetu ingekua mbali kiuchumi na ingekua ni nchi ya viwanda? pengine ingekua kuikaribia south afrika?unakubaliana na mimi kuwa sera ya ubinafsishaji ilifanyika hovyo?

Kama ingefanyika vizuri leo hii tungekua hatukopi hata senti tano nje? sasa niambie viwanda vyetu viko wapi je unajua kuwa tulikua na kiwanda cha kutengeneza BISKELI zilizoitwa SWALA.Na hivi viko wapi? TAMCO kuunganisha SCANIA,General tyre kutengeneza magurudumu,Urafiki,Mwatex,Sungura tex,Mutex,Kilitex hivi vilitengeneza nguo,kiko wapi kiwanda cha kutengeneza majembe cha ubungo,Matsushita kilitengeneza radio,Tanganyika Parkers kilisindiks nyama za kopo,TIPER kilisafisha mafuta ghafi,Tz railways corporatiion na AIR TZ Corporatio hivi vilisaidia sana usafirishaji sio viwanda,Iko wapi Valmet.

Viko wapi wapi viwanda vyetu vya kutengeneza juice,tangold,liko wapi shirika la TZ Elimu suupplies,viko wapi viwanda vya sabuni za Gardenia,Lumi,Lux au hizi zilitoka nje?Unajua kiwanda cha chuma MANG'ULA,Viko wapi viwanda vya kuprocess pamba,tumbaku,chai,kahawa,katani na sukari?kiko wapi kwanda cha viatu Morogoro shoes na BORA,hivi ni vichache tu ndg zangu.

Je tangu zama hizo tusingekua tumeongeza vingine? Mwadui na Tancut almasi bado vyetu?nikumbusheni jamini bado vipo? na vingine vya siri na visivyo vya siri nimevisahau.tukumbushane tupate uchungu na nchi yetu.hii gesi haya madini tungeweza kuchimba wenyewe tu.unakikumbuka kiwanda cha mbolea Tanga TFC na kiwanda cha kutengeneza filamu ( sinema) TZ FILIM CORPORATION,hiki kisingewafaa akina Marehemu Kanumba,RAY,JB,na wengineo?Viwanda vingi China ni mali ya umma na sasa China ni world second largest economy.

Tukumbuke.

Ndugu,
Usitegemee kupata wachangiaji kwenye thread kama hii! watu wamejikita kwenye kugombania madaraka ili watawale yote hayo. Wauze gesi na madini kirahisi. Sijui katiba mpya inasemaje kuhusu mali za serikali na mfumo wa kuzibinafsisha. Viwanda vyote vimegeuzwa magodown au kubadilisha matumizi na kuweka Bar. Sasa viwanda vilivyobaki ni Sigara na Bia unategemea nini hapo? Mabenki ndio usiseme kuna ile tuliyoambiwa ni kubwa sana na mpaka leo nafikiria sipati jibu ukubwa wake ni upi?
La msingi ni kwamba tumetambua tulipojikwaa sasa ni wakati wa kuanza upya katika sekta zote tukijikita zaidi kwenye elimu. Wako wapi watanzania tunaeweza kujisifia ujuzi wao. madaktari mpaka leo tatizo dogo tu unatoa kiasi upelekwe india. Makandarasi ndio kabisa! ukiuliza mwananchi engineering (MECCO) ilipopotelea sijui kama kuna mwenye kumbukumbu! .......................
 
achana na habari hiyo mkuuu utaumiza tu kichwa chako ....serikali yetu hiii wanaijuaaa wenyw
 
Hapa hutapata wachangiaji.
Sikuhizi maswali haya hayana majibu.
swali majibu yake yashajibiwa kitambo na yanaeleweka...watu washalalamika hadi vipara vikawatoka....so nikumizaa tu kichwa chake hyo mleta mada
 
Utakubaliana na mimi kuwa Tanzania ilikua ina viwanda makini,na kama vingeendelezwa na kuwadhibiti viongozi wake waliokua wanaviendesha vibaya leo hii nchi yetu ingekua mbali kiuchumi na ingekua ni nchi ya viwanda? pengine ingekua kuikaribia south afrika?unakubaliana na mimi kuwa sera ya ubinafsishaji ilifanyika hovyo?

Kama ingefanyika vizuri leo hii tungekua hatukopi hata senti tano nje? sasa niambie viwanda vyetu viko wapi je unajua kuwa tulikua na kiwanda cha kutengeneza BISKELI zilizoitwa SWALA.Na hivi viko wapi? TAMCO kuunganisha SCANIA,General tyre kutengeneza magurudumu,Urafiki,Mwatex,Sungura tex,Mutex,Kilitex hivi vilitengeneza nguo,kiko wapi kiwanda cha kutengeneza majembe cha ubungo,Matsushita kilitengeneza radio,Tanganyika Parkers kilisindiks nyama za kopo,TIPER kilisafisha mafuta ghafi,Tz railways corporatiion na AIR TZ Corporatio hivi vilisaidia sana usafirishaji sio viwanda,Iko wapi Valmet.

Viko wapi wapi viwanda vyetu vya kutengeneza juice,tangold,liko wapi shirika la TZ Elimu suupplies,viko wapi viwanda vya sabuni za Gardenia,Lumi,Lux au hizi zilitoka nje?Unajua kiwanda cha chuma MANG'ULA,Viko wapi viwanda vya kuprocess pamba,tumbaku,chai,kahawa,katani na sukari?kiko wapi kwanda cha viatu Morogoro shoes na BORA,hivi ni vichache tu ndg zangu.

Je tangu zama hizo tusingekua tumeongeza vingine? Mwadui na Tancut almasi bado vyetu?nikumbusheni jamini bado vipo? na vingine vya siri na visivyo vya siri nimevisahau.tukumbushane tupate uchungu na nchi yetu.hii gesi haya madini tungeweza kuchimba wenyewe tu.unakikumbuka kiwanda cha mbolea Tanga TFC na kiwanda cha kutengeneza filamu ( sinema) TZ FILIM CORPORATION,hiki kisingewafaa akina Marehemu Kanumba,RAY,JB,na wengineo?Viwanda vingi China ni mali ya umma na sasa China ni world second largest economy.

Tukumbuke.
kiwanda cha PHILIPS,Tanzania FOOD,kiwanda cha KIKO, NMC
 
Kama vile ulikuwa umefariki miaka ya themanini hivi...ukafufuka leo! Hiyo ndiyo Tz bwana..chezea ccm wewe!!
Ngorunde mimi nadhani hivi viwanda vilikuwa Tanzania na habari iliyopo ni kwamba vilichukuliwa na mafuriko. Wataalamu wanasema kuna uwezekani vimepotea kama ile ndege ya Malaysia na hata jana Lowassa alikuwa kwa TB Joshua kupata utabiri kama zitaonekana au la!!!!!
 
SPM kiwanda cha karatasi mgololo na sawala. walifosiwa kustaafu wakanyimwa mafao wanateseka sana
 
swali majibu yake yashajibiwa kitambo na yanaeleweka...watu washalalamika hadi vipara vikawatoka....so nikumizaa tu kichwa chake hyo mleta mada

Mie inaniuma sana mkapa alivyo iuza Nbc, hapo ndio alitenda unyama mwisho!
 
TAZANIA, TAIFA LA WATU LEGELEGE.
watoto wenu mnawapeleka kusoma procurement,accountant, political science, administration, linguistic na ujinga mwingi, unategemea nini? hivi vitu wataviona ni chuma chakavu tu,, madarasa ya science siku hizo hayana watu, waumini wa bongo fleva na bongo movie wapo wengi,, tunategemea hata kesho tukifufua hivi viwanda ni nani atazalisha? tanzania kama nchi masikini inahitaji kuwekeza kwenye rasilimali watu, watu ambao moja kwa moja watakuwa na impact kwenye uchumi, na maanisha kuwa na namba ya kutosha ya matechnologist, vinginevyo mwendo huu wa watu kutaka kusomea manunuzi na uhasibu kuhesabu hela za wahindi hatuwezi kutoka kwenye tope hili...
ukiangalia sector nyingi ambazo zinatakiwa ziongozwe na watalaam husika zinapewa wapiga porojo, angalia mfano nishati na madini enzi zile na sasa ambapo yupo mtalaam husika.

kaka viwanda vilikufa Kwa sababu vilikosa usimamizi, kuajili kwa kujuana hata kama mtu si proffesional, siasa, upeo mdogo nk, kaka tanzania ina watalaamu wengi sana nje ya nchi ambao ni competent ila kujuana na kutokusaminiana ndio kunasababisha kutokubali kufanya kazi tanzania.
nchi zote zilizoendelea ziliwekeza kwenye vyuma (viwanda) zikawa na techologist wakutosha bandaye
walivyoendelea ndio ujinga mwingine ukafuata.

TANZANIA NCHI MASIKINI MILELE, MPAKA HAPO WANANCHI WATAKAPO AMKA NA KUJITOA KWA UZALENDO KUIPIGANIA NA KUFA KWA AJILI YA NCHI YAO.. MUNGU IBARIKI TANZANIA NA WATANZANIA WAZALENDO, AMSHA NA WALE WALIOLALA PEPO LA USINGIZI LIWATOKE. AMEN
 
soma historia ya ulaya na marekani, historia ya nchi zote zilizoendelea utaona kuna watu wengi saana walikufa kwenye production kwa niaba ya vizazi vyao vipya,,, je ni mtanzania gani ameshakufa kwa ajili ya maendeleo ya nchi hii? (namaanisha kwenye production kwa ajili ya nchi) jibu utaona hakuna, Kwa hiyo utaona kuna stage tumeiruka ambayo bado inatutafuna,,,

INABIDI TUPATE KIONGOZI WA JAMI
HITTLER ATUTAWALE KAMA MIAKA 20 ILI TUFE SANA KWENYE KAZI, BAADA YA HAPO KIZAZI KIJACHO 2098 na kuendelea KITAKUWA SI KIZAZI CHA WATU LEGELEGE,DHAIFU NA WAZEMBE KAMA HIKI.

EEEEH MUNGU IBARIKI JAMII YA WATANZANIA WAZALENDO NA SHUPAVU. TUONDOLEE WANAFIKI, WABINAFSI,WEZI, WATU LEGELEGE, NA WALE WOOOTE WANAOJIPENDEKEZA NA KUSHABIKIA WANAUME WENZAO ILI WAO WALE..
 
Mie inaniuma sana mkapa alivyo iuza Nbc, hapo ndio alitenda unyama mwisho!

hapa ndio ilipoanzia failure trend ya tanzania, ila watu wanakuwa kama hawaoni,,, kilichomkuta JK ni sawa na gari ambalo limepoteza uelekeo halafu abiria wakiwa wamelala wakiamini kila kitu ni sawa.... Pole JK kwayaliokukuta, mwenzio kasign contract za migodi miaka 100,,, leo unapata shida na lawama.
Tanzania sasa inahitaji watu shupavu na sio legelege tena. tunahitaji uongozi wa mkono wa chuma ili kutengeneza kizazi cha watu shupavu na makini.

MUNGU IBARIKI TANZANIA IPATE WATU SHUPAVU NA MAKINI,, KIONDOE KIZAZI HIKI CHA WATU WANAFIKI NA LEGELEGE.
 
The time will tell. Wacha wale ila kuna stage watafikia mfupa, hapo hata yule aliyelala ataamka, mwenye njaa atatoa saut ya kudai na hapo haki itatafutwa na haitaombwa tena. Pamoja na mapambano yetu watanzania kuna haja ya kumuomba Mungu atupe kiongoz amri na kuweka woga pembeni namaanisha tupate yule atakayeitwa na mataifa ya magharibi "mwendawazimu".
Kwa sababu hili taifa linamaadui wawili wakubwa wa uchumi. Siasa na uongoz mbovu pamoja na shinikizo la mataifa makubwa. "TIME WILL TELL"
 
achana na habari hiyo mkuuu utaumiza tu kichwa chako ....serikali yetu hiii wanaijuaaa wenyw
vyuo vya ufundi,watu wanasomea engineering watafanya kazi wapi mkuu,haya si ndo mambo ya Tunisia ,mtu anamaliza UNIVERSITY anajiajiri kuuza genge.Au tusubiri EA Watanazania wakafanye kazi katka viwanada vya Kenya halafu bidhaa zije ziuzwe Tanzania.
 
Hapa hutapata wachangiaji.
Sikuhizi maswali haya hayana majibu.
Ni kweli Madam lakini unaonaje suala la ajira kama hatuna viwanda? unasemaje kuhusu vijana wanaomaliza masomo ya ufundi na engineering
watafanya kazi wapi? nchi bila viwanda ni janga Madam.
 
Kama vile ulikuwa umefariki miaka ya themanini hivi...ukafufuka leo! Hiyo ndiyo Tz bwana..chezea ccm wewe!!

mkuu unajisikiaje nchi yenye misitu minene kama hii kuagiza vijiti vya kuchokonolea meno kutoka nje?hata midoli ya kuchezea watoto tulikuwa tukitengeneza sasa inatoka Taiwani,China,India na kwingineko
 
SPM kiwanda cha karatasi mgololo na sawala. walifosiwa kustaafu wakanyimwa mafao wanateseka sana[/QUO Nafarijika sana kuwa bado nchi hii ina watu wenye kumbukumbu kama wewe juu ya viwanda vyetu na maddhira waliofanyiwa wafanyakazi wazalendo.hata hivyo bado kuna watu watatamani mfumo ulioua viwanda uendelee kuwepo.
 
TAZANIA, TAIFA LA WATU LEGELEGE.
watoto wenu mnawapeleka kusoma procurement,accountant, political science, administration, linguistic na ujinga mwingi, unategemea nini? hivi vitu wataviona ni chuma chakavu tu,, madarasa ya science siku hizo hayana watu, waumini wa bongo fleva na bongo movie wapo wengi,, tunategemea hata kesho tukifufua hivi viwanda ni nani atazalisha? tanzania kama nchi masikini inahitaji kuwekeza kwenye rasilimali watu, watu ambao moja kwa moja watakuwa na impact kwenye uchumi, na maanisha kuwa na namba ya kutosha ya matechnologist, vinginevyo mwendo huu wa watu kutaka kusomea manunuzi na uhasibu kuhesabu hela za wahindi hatuwezi kutoka kwenye tope hili...
ukiangalia sector nyingi ambazo zinatakiwa ziongozwe na watalaam husika zinapewa wapiga porojo, angalia mfano nishati na madini enzi zile na sasa ambapo yupo mtalaam husika.

kaka viwanda vilikufa Kwa sababu vilikosa usimamizi, kuajili kwa kujuana hata kama mtu si proffesional, siasa, upeo mdogo nk, kaka tanzania ina watalaamu wengi sana nje ya nchi ambao ni competent ila kujuana na kutokusaminiana ndio kunasababisha kutokubali kufanya kazi tanzania.
nchi zote zilizoendelea ziliwekeza kwenye vyuma (viwanda) zikawa na techologist wakutosha bandaye
walivyoendelea ndio ujinga mwingine ukafuata.

TANZANIA NCHI MASIKINI MILELE, MPAKA HAPO WANANCHI WATAKAPO AMKA NA KUJITOA KWA UZALENDO KUIPIGANIA NA KUFA KWA AJILI YA NCHI YAO.. MUNGU IBARIKI TANZANIA NA WATANZANIA WAZALENDO, AMSHA NA WALE WALIOLALA PEPO LA USINGIZI LIWATOKE. AMEN
Mkuu umemaliza,lakini ajabu kuna watu wanataka mfumo ulioua viwanda,spirit ya kusoma masomo ya sayansi uendelee kutawala,tuna safari ndefu,hata hivyo darasa ulilotoa usiache kuwafumbua na wengine wataamka tu.
 
Back
Top Bottom