Niende s/Africa au Mauritius?

Niende s/Africa au Mauritius?

Acha uongo.nauli za lin hizi??
-Dar mpaka h/re ni 80000tsh
-H/re jo'berg ni 250/300.sa rand ambayo ni kama 50000tsh
-jo'berg mpaka cape ni 600rand ka intercape hzo ni bus za luxually.pia kuna bus mpaka za 400


Naomba nikukosoe mkuu! Dar to Harare mwaka juzi nilienda kwa 140,000 kwa Taqwa, Na Jana nimetoka kuuliza nauli kwa Bus nikakuta imepanda, binafsi nna safari ya Lesotho naona bora nichukue flight to J'burg then nichukue Bus mpaka Lesotho...Nikichangia mada binafsi sishauri mtoa mada uende SA, ukiaccha Ubaguzi Kuna matatizo Mengi, nenda Mauritius, Namibia, Lesotho, Botswana hata Mozambique, Kuna vitu sisi tunafanya hapa huko hakuna au wanafanya tofauti, so nna uhakika ukienda Na ma idea ya kwetu hapa unapiga hela but kwa SA utaumizwa mpaka Na Watanzania wenzako ambao walishapoteza, japo wenyewe hawapendi lakini huo ndo ukweli.
 
Nenda Mauritius hutajuta.

Ni rahisi kupata agents wa kupokea bidhaa toka Tanzania kwenda huko.

Hakujafunguka sana kama S.A.

Watu wa kule ni wakarimu sana, unaweza ukagoma kurudi.

Asante mkuu, umenipa moyo sana
 
Gelofriend Najua zile camera zako zilivyo nzito +zubeda lako la nguo. Nahisi vitakushinda tu kubeba alonooo, na huwezi kumsumbua boss akusaidie kubeba. Afu me siongeagi barabarani wala kula sana, kwa hiyo sitawabugudhi safarini. Tutaenjoy kwa kweli

Gelofriend are you want to go with me and amicus
mmh you are overtaking me at the corner, amicus will choose you and leave me
i have started to practice the language of South Africa and Malaysia
 
Weee bora hata uende songea, south africa hapafai wanakatakata watu na mapanga kuleee, alafu mauritius kuna mafuriko. Heaven Sent njoo umuone boss wako anatoa experience ya nchi alizotembelea ndotoni.
 
Last edited by a moderator:
Weee bora hata uende songea, south africa hapafai wanakatakata watu na mapanga kuleee, alafu mauritius kuna mafuriko. Heaven Sent njoo umuone boss wako anatoa experience ya nchi alizotembelea ndotoni.

Hahahhah boss lady nakuaminia. Ushatembelea nchi zote ndotoni. Next time nichukue tu na mimi ndotoni, maana sijawahi hata kuvuka mpaka jamani
 
Last edited by a moderator:
Mkuu mimi ninaishi Johannesburg. Maisha ya huku ni poa kama una kazi. Kuja kutembea ni poa tu kwani utakuwa huku kwa muda mfupi ila usifikirie ndoto za kuzamia. Maisha ni magumu na watu hawana huruma.

Kama unakitu specific unataka kujua usisite kuuliza, nitakusaidia. Nakushauri njoo na ndege kuna hotel nyingi tu unaweza kuishi. Kuna hata guest house za watanzania ninaweza kukutafutia lakini cha muhimu uje umejiandaa. Maisha ya huku ni mchaka mchaka na kila kitu kinahitaji hela. Kuna mshikaji alikuja na basi wakati Fulani, akakutana na Mtanzania mwenzake. Jamaa alitegemea huyo mtanzania atamsaidia ila matokeo yake jamaa alimuibia begi lake na ndani kulikuwa na wallet na vitu vingine muhimu. Maisha yalikuwa magumu mno, ana bahati tulikuwa tunafahamiana akajaribu kuja sehemu yangu ya kazi ndio akanipata. Ila sio mchezo maisha bila kazi bora Tanzania kuna mjomba,shangazi na ndugu wengine wanaoweza kukusaidia. Huku ni vingine, kama hujajipanga vizuri unaweza kuja kujiingiza kwenye vitendo vya uhalifu kuwa makini.
 
Back
Top Bottom