Ndenji five
JF-Expert Member
- Nov 1, 2021
- 1,985
- 3,083
Ama kweli tenda wema nenda zako, na leo yamenikuta, ni miaka mitano sasa tokea nilipomchukua, mke wangu na mdogo wake, ambae ni wa kike, tukaishi kwa upendo na amani, huyu mdogo wake nilimchukulia kama mdogo wangu, wa tumbo moja na kila nilipopata nafasi ya kusafiri kikazi nilikuwa siachi kuwabebea zawadi na mke wangu, lakini baada ya muda mambo yalibadilika, shemeji akawa ameanza vimitego vya kichokozi, na bila kusita nilikuwa namuonya, kuhusu tabia zake nisizipendi, ikapita muda hatimaye siku dada yake yuko kazini mimi nikiwa nimejipumnzisha akawa ameniingilia chumbani akiwa mtupu.
Nikalaani kile kitendo na kufikisha taarifa kwa dada yake, ila kilichofuata sikuamini, shemeji akaanza kusema namtaka kimapenzi, na hata zile zawadi nilizokuwa nanunulia, zilikuwa, kama za kumshawishi, dada yake kwa kutochunguza ukweli, akaamini na mwisho nikaonekana mimi ni mkosaji suala likaenda kwa mshenga, ili kuokoa ndoa yangu nikakiri makosa, japo inaniuma sana kusingiziwa kitu ambacho sijafanya, wakuu nipo njia panda?
Nikalaani kile kitendo na kufikisha taarifa kwa dada yake, ila kilichofuata sikuamini, shemeji akaanza kusema namtaka kimapenzi, na hata zile zawadi nilizokuwa nanunulia, zilikuwa, kama za kumshawishi, dada yake kwa kutochunguza ukweli, akaamini na mwisho nikaonekana mimi ni mkosaji suala likaenda kwa mshenga, ili kuokoa ndoa yangu nikakiri makosa, japo inaniuma sana kusingiziwa kitu ambacho sijafanya, wakuu nipo njia panda?