Nianze na CPA au bachelor degree?

Nianze na CPA au bachelor degree?

Panctuality

JF-Expert Member
Joined
Jun 11, 2019
Posts
925
Reaction score
1,386
Habarini wakuu.
Naomba kusaidiwa kimawazo, Mimi ni muhitimu wa Diploma in Accounting and Finance mwaka 2014 na tangu 2016 mpaka sasa ni muajiriwa as an accountant katika taasisi (private),

Nafikiria kujiendeleza kielimu katika tasnia hii hii ya accountancy na katika kufuatilia hapa na pale inaelezwa kuwa unaweza ukachukua CPA (T) kwa kuanzia Foundation level, intermediate level na hatimaye Final level na kuwa CPA holder au kuingia bachelor degree ya accountancy na kusoma CPA kwa kuanzia level ya intermediate level hadi final level.

Naomba kushauriwa nipitie njia gani ili nibaki salama kwenye ajira yangu na maisha ya familia yaendelee? Na je, foundation level naweza kupata exemptions kwa baadhi ya masomo ikizingatiwa Diploma yangu ni ya Accounting and Finance GPA 4.1 ?
 
Kiufupi kapige CPA moja kwa moja hiyo degree achana nayo....

Maake tofauti ni hiyo foundation tuu miez minne ukasome degree miaka mitatu,

Wapo ambao wamesoma kozi za injinia, na walianza chini na sasa ni CPA T
Okey nashukuru kwa ushauri, japo inasemekana mitihani ya bodi inakazwa kweli kweli lakini kama wameweza mainjia wasio kuwa na msingi wowote wa accounting na wakawa ma CPA nishindweje mimi mwenye msingi huo from A-level (EGM) to Diploma (DAF).
Nitakaza tu ngoja nijipange tu
 
Okey nashukuru kwa ushauri, japo inasemekana mitihani ya bodi inakazwa kweli kweli lakini kama wameweza mainjia wasio kuwa na msingi wowote wa accounting na wakawa ma CPA nishindweje mimi mwenye msingi huo from A-level (EGM) to Diploma (DAF).
Nitakaza tu ngoja nijipange tu
Inakazwa kikubwa kusoma kwa bidii, basi na kuwa na uelewa zaidi maake unaenda kuwa professional
 
Habarini wakuu.
Naomba kusaidiwa kimawazo, Mimi ni muhitimu wa Diploma in Accounting and Finance mwaka 2014 na tangu 2016 mpaka sasa ni muajiriwa as an accountant katika taasisi (private), nafikiria kujiendeleza kielimu katika tasnia hii hii ya accountancy na katika kufuatilia hapa na pale inaelezwa kuwa unaweza ukachukua CPA (T) kwa kuanzia Foundation level, intermediate level na hatimaye Final level na kuwa CPA holder au kuingia bachelor degree ya accountancy na kusoma CPA kwa kuanzia level ya intermediate level hadi final level.
Naomba kushauriwa nipitie njia gani ili nibaki salama kwenye ajira yangu na maisha ya familia yaendelee? Na je, foundation level naweza kupata exemptions kwa baadhi ya masomo ikizingatiwa Diploma yangu ni ya Accounting and Finance GPA 4.1 ?
Kwanza kwa mujibu wa sheria wewe sio accountant,ni karani tu,soma cpa ili usajiliwe kuwa mhasibu
 
Kwanza kwa mujibu wa sheria wewe sio accountant,ni karani tu,soma cpa ili usajiliwe kuwa mhasibu
Ni sahihi kabisa sikupingi kama ilivyo hata kwa mwenye Bachelor degree au masters in accountancy bila CPA bado nae ni karani tu japo anakuwa karani wa kiwango cha rami/karani aliyechangamka kichwani
 
Habarini wakuu.
Naomba kusaidiwa kimawazo, Mimi ni muhitimu wa Diploma in Accounting and Finance mwaka 2014 na tangu 2016 mpaka sasa ni muajiriwa as an accountant katika taasisi (private),

Nafikiria kujiendeleza kielimu katika tasnia hii hii ya accountancy na katika kufuatilia hapa na pale inaelezwa kuwa unaweza ukachukua CPA (T) kwa kuanzia Foundation level, intermediate level na hatimaye Final level na kuwa CPA holder au kuingia bachelor degree ya accountancy na kusoma CPA kwa kuanzia level ya intermediate level hadi final level.

Naomba kushauriwa nipitie njia gani ili nibaki salama kwenye ajira yangu na maisha ya familia yaendelee? Na je, foundation level naweza kupata exemptions kwa baadhi ya masomo ikizingatiwa Diploma yangu ni ya Accounting and Finance GPA 4.1 ?
CPA ndio Confused Public Accountant?
 
Kulikuwa na haja ya kuweka hyo GPA 4.1 kwenye maelezo yako mkuu!!

Jiulize mara tatu unataka kusoma CPA ili iweje....kama ni mshahara go on ila ila kujiendeleze wewe mwenyewe kiuchumi ,hyo pesa + diploma yko wekeza sehemu kwa faida yako na kizazi chako.
 
Habarini wakuu.
Naomba kusaidiwa kimawazo, Mimi ni muhitimu wa Diploma in Accounting and Finance mwaka 2014 na tangu 2016 mpaka sasa ni muajiriwa as an accountant katika taasisi (private),

Nafikiria kujiendeleza kielimu katika tasnia hii hii ya accountancy na katika kufuatilia hapa na pale inaelezwa kuwa unaweza ukachukua CPA (T) kwa kuanzia Foundation level, intermediate level na hatimaye Final level na kuwa CPA holder au kuingia bachelor degree ya accountancy na kusoma CPA kwa kuanzia level ya intermediate level hadi final level.

Naomba kushauriwa nipitie njia gani ili nibaki salama kwenye ajira yangu na maisha ya familia yaendelee? Na je, foundation level naweza kupata exemptions kwa baadhi ya masomo ikizingatiwa Diploma yangu ni ya Accounting and Finance GPA 4.1 ?
Anza CPA, By the time wenzio wanamaliza degree wewe utakuwa na experience ya kazi by 3+ years na pengine unakaribia kupata CPA, by the time wengine wana experience ya miaka 2 kazini wewe utakuwa na 5+ years experience, una CPA.

Diploma + CPA > Degree.
 
Kulikuwa na haja ya kuweka hyo GPA 4.1 kwenye maelezo yako mkuu!!

Jiulize mara tatu unataka kusoma CPA ili iweje....kama ni mshahara go on ila ila kujiendeleze wewe mwenyewe kiuchumi ,hyo pesa + diploma yko wekeza sehemu kwa faida yako na kizazi chako.
CPA foundation level kutokea Diploma GPA ikiwa chini sana hupati exemptions za kutosha trust me.
Elewa neno EXEMPTIONS in accountancy field
 
Maliza Bachelor ndipo uingie CPA
Miaka 10 ya ajira ndani yake kuna majukumu ya kifamilia yaliyaanzishwa, nikianza degree huku ajira inajifunga. Labda nikuulize OPEN university ina offer degree ya BAF ili nisibanwe na kuwa darasani kwa usalama wa kutopoteza ajira niliyonayo?
 
Kwa sisi ambao hatuna elimu yoyote ya uhasibu, tukianzia ATEC 1 & 2, tunaweza kwenda Foundation Level > Intermediate > Final?
Ukifikia NTA level 6 (ATEC II) ndio inakuwa sawa na diploma ya uhasibu hapo ndio unaenda foundation level, intermediate level to final level (professional level)
 
Back
Top Bottom