Ni yupi MwanaJF bora kwa mwaka 2022

Kanali G

JF-Expert Member
Oct 21, 2013
9,902
14,377
Mwaka unakaribia kuisha ni wazi kwamba wapo wana JF wengi walijitokeza na kufanya vizuri au kuchangamsha kutokana na mada au michango yao mbalimbali.

Baadhi ya wa JF wameonekana kufanya vizuri zaidi kwa mwaka huu, unadhani ni nani anastahili Tuzo ya mwana JF bora kwa mwaka 2022, kwa upande wangu ningechagua miongoni mwa wafuatao;

1. Mshana Jr - Hujitokeza katika majukwaa mbalimbali kwa kuchangia au kutoa mada, ni mzuri sana kwenye mada za Dini na za Sayansi ya asili.

2. Paschal Mayalla - Pamoja na kujipambanua itikadi yake kisiasa lakini haiondoi ukweli kuwa mada na michango yake ili elimisha wengi.

3. Gentamycin - Hushambuliwa na baadhi ya wana JF kila anapotoa uzi, lakini haiondoi ukweli kuwa alikuwa bora kwa mwaka huu, anastahili Tuzo.

4. Erythcrote- Mwana CHADEMA kindakindaki, hujitokeza pia kwenye majukwaa mengine hasa michezo, amekuwa mwana JF mzuri kuharisha members wengine kwa mwaka huu, naona pia anastahili Tuzo.

5. MK254 - Kwenye vita ya Urusi na Ukraine amekuwa akitoa breaking news kila inapotokea ingawa ameegemea sana upande wa Ukraine.

6. Okwi Boban Sunzu - Hupatikana sana kwenye michezo akiisapoti timu yake ya Simba na pia Siasa akikisapoti chama chake cha Chadema, alikuwa member mzuri mwaka huu.

7. Sky Eclat - Ni mwanamama mwenye madini mengi kichwani na amekuwa akiyatoa bila shida kwa wana JF.

8. Umughaka - Story zake za kusisimua zimewaburudisha na kuwafundisha wengi kungekuwa na Tuzo angekuwa miongoni mwa wanaowania.

9. Victoire - Yeye pia ni miongoni mwa wana JF alitamba kwenye majukwaa mbalimbali mwaka huu.

10. Mpwayugu village - Mtaalam wa story ingawa zingine zilikuwa hazifiki mwisho.

11. Shaadeya - Mwana Yanga lia lia, yeye na Yanga yake.

12. Bujibuji - Amechangia sana kwenye majukwaa mbalimbali bila kumdhihaki mtu.

13. Rickboy - Sijui kama nimepatia spelling, huyu yeye kwenye Jukwaa la kugegedana amepakamata.

14. Mzee Mohamed- Jukwaa la Historia ni kama lake, amekuwa akishusha nondo za uhakika, ingawa anashutumiwa kwa kupendelea Dini yake.

Kwa upande wako unadhani nani anastahili Tuzo hii kama ingekuwa inatolewa?
 
Mbona kama Ballon d’or contenders list almost ni wale wale?Anyway
Kuna jamaa mwaka huu kaupiga kama “Benzema” dakika zake za ki UEFA UEFA ni yule mzee wa kusubiri “hatma kutoka kwa vijana wa Buguruni”

Kuna kina [mention]mzabzab [/mention]wanakimbiza kama mwaka ule wa kina [mention]Joseverest [/mention].
 
Back
Top Bottom