Wakuu unaona niyupi anagombania urais 2015 ndani ya CCM bila aibu?
irais ndiyo nini babu?rekebisha title ya thread kwanza
kuhusu mada:kwani mtu akigombea urais bila aibu kuna tatizo gani?nadhani ndiyo safi ili tumjue vizuri kama atafaa kuwa rais wetu au naye ni walewale tu.au we unadhani wanaojifichaficha ndiyo wagombea wanaofaa?
Kwa mtazamo wangu 2015 CDM itashindwa kama 57% nakuendelea kama uchakachuaji hautakwepo,
ila kwa vile watanzania wengine hawajielewi mzee wa mvi atasumbua sana ingawa kupata urais ni ngumu.
Mwenye macho haambiwi "tazama." Ni nani aliyegundua hivi karibuni kuwa ukosefu wa ajira kwa vijana ni tatizo la kitaifa? Ni nani anayezurura akichangisha fedha za makanisa? Mwenye macho haambiwi "tazama."