Ni wapi wanatoa mafunzo ya Martial Arts?

Papa Mopao

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2009
Posts
4,157
Reaction score
2,663
Kuna sehemu wanatoa haya mafunzo?

===========

Kawe, Mbezi, Mbagala, Kisutu, Don Bosco, n.k, inategemea ni staili gani ya sanaa ya mapigano na gharama pia

Nenda Manzese Tiptop, muulizie Sensei Jango!

Nenda Tanganyika Pakers Kawe, muulizie Sensei Chikoko!

Nenda Ubungo Islamic High School, muulizie Sensei Yahaya Mgeni!

Njoo JamiiForums, ni PM

Kama upo Dar, nenda Kawe - Tanganyika Pakers Mtafute Sensei Chikoko

 
Last edited by a moderator:
unapatikana wapi ili nikutajie mahala karibu?
 
Hebu taja vituo vilivyopo Dar wanavyotoa hayo mafunzo.
kawe, mbezi, mbagala, kisutu, donbosco, n.k inategemea ni staili gani ya sanaa ya mapigano na gharama pia
 
kawe, mbezi, mbagala, kisutu, donbosco, n.k inategemea ni staili gani ya sanaa ya mapigano na gharama pia

Style gani nzuri mkuu!? Mimi nataka Systema au Combat Karate.
 
Kuna sehemu wanatoa haya mafunzo?
serikali ya china ilikua inatafuta vijana wanne wasomeshwe china mwaka mmoja,ila deadline ilikuwa mwezi june
nenda pale utumishi wa umma chumba namba kumi na saba watakusaidia
 
Style gani nzuri mkuu!? Mimi nataka Systema au Combat Karate.

Mkuu kimsingi hakuna staili inayoitwa "combat karate"...ile wanayofundishwa jeshini ni baadhi tu ya mafunzo ya staili fulani. Yaweza kuwa shotokan au goju ryu pamoja na vitu vichache vya aikido au jiujitsu.

Pili hakuna sanaa ya mapigano ambayo ni bora zaidi ya nyingine. Msanii ndio huwa bora. Ni kama sanaa ya muziki. Haijalishi unaimba muziki gani, wewe kama msanii ndio waweza kusababisha muziki wako kupendwa au kuchukiwa.
Nitatoa mfano wa wasanii wa sanaa ya mapigano walio shawishi watu kujifunza baadhi ya sanaa zao:

Jackie Chan-Kungfu(Drunken & Snake)
Bruce Lee-Jeet Kune Do
Jet Lee-Wushu
Van Damme-Shotokan Karate
Tony Jaa-Muai Thai & Tae Kwon do
Scott Adkin(Boyka)-Kick Boxing&Tae kwon do
Shoku Sugi-Ninjitsu
Steven Seagal-Aikido
Donie Yen-Judo,Wushu & Wing chun

Hao ni baadhi tu. Leo hii kuna maelfu ya watu wanaojifunza hizo sanaa kwa ushawishi wa hao watu.
Kwa hiyo haijalishi utajifunza sanaa gani ila wakati wote kumbuka kuwa,'Sanaa haimfanyi mtu bali mtu ndiye huifanya Sanaa'.
Kila lakheri.
 
Hii ya Donie Yen-Judo,Wushu & Wing chun, naikubali sanaaa tu.......nimekuwa nikimwangalia hasa ile movie ya IP-Man 1&2 na Kung.Fu.Jungle.(2014)
 

Hii Tae Kwon do nimepiga sana pale Nairobi.
 
Hii ya Donie Yen-Judo,Wushu & Wing chun, naikubali sanaaa tu.......nimekuwa nikimwangalia hasa ile movie ya IP-Man 1&2 na Kung.Fu.Jungle.(2014)
donnie kajifunzza style nyingi san. hadi boxing, mieleka na zile za kibrazil.
 
kuna moja ni nzuri xana inaitwa shorinj. wana falsafa nzuri xana
 
I did shotokan for 3 good years kwa sempai Gilbert manzese, mpaka leo siwezi acha ku practise. Inafundisha discipline ya hali ya juu sana. All in all style zote nzuri. Chagua ambayo itakuwa karibu na wewe.
 

Mkuu unajua hizi mambo...nice comment mkuu●■
 
Mdau umeuliza suali nzuri sana. Nami naulizia sehemu hizi kwa maeneo ya Arusha. Nipo huku kwa kikazi so ningependa nitumie muda huu kujifunza.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…