Ni wakati wa Kanisa Katoliki kusimama na kukemea,Askofu Shoo ameonesha njia.Waumini wana manung'uniko

Ni wakati mwingine tena kauli ya Kiongozi Mmoja mkubwa wa kanisa la Tanzania imetikisa nchi.Hii ni sauti ambayo ilisubiriwa kwa muda mrefu toka kwa moja wa viongozi wa dini wanaoheshimika Tanzania.Hii ni kwa sababu,licha ya viongozi wa kisiasa kuwa na mamlaka na nguvu za kidola,bado viongozi wa kidini huwa na heshima na uaminifu wa kauli zao toka kwa waumini wao.

Ni bahati mbaya kuwa,tupo katika zama ambazo watawala tulionao wanajiona miungu watu,wanapenda kusifiwa,kutukuzwa na kuabudiwa.Wamejivika umalaika na ukuu usiohojika.Wanapenda kukemea pasipo wao kukemewa,wanapenda kuonya pasipo kuonywa na wanapenda kuwakosoa wenzao mbele kadamnasi ila wao wanapenda wasifiwe hadharani na kutukuzwa wakiwa faragha.

Imekuwa hivyo sehemu nyingi duniani,viongozi waliopo madarakani kuhakikisha kuwa "wanawateka" viongozi wa kidini ili wasikosolewe,wasionywe wala wasikemewe.Hii imeota mizizi pia hapa Tanzania.Watu hawataki kukosolewa,wanataka kusifiwa,hawataki kuonywa wanataka kuabudiwa,hawataki kukemewa wanataka kutukuzwa.

Juzi walipokaribishwa kumsimika kiongozi mkubwa wa dini kule nyanda za juu kusini,waliposifiwa na kuabudiwa,hawakusema kuwa "siasa imeingia kwenye dini",ila wakikosolewa wanasema dini imeingilia siasa.Juzi walikaribishwa pale Mwenge,kwenye kanisa binafsi la mtu,na walipewa nafasi ya kuhubiri kama wachungaji na kutafsiri vifungu vya biblia,hawakusema kuwa wanasiasa wameingilia dini.Askofu mwenye kanisa lake akawasifia na kuwatukuza,hawakusema dini imeingilia siasa.Ila wanapoonywa na kukosolewa,wanang'aka na kupayuka kuwa dini imeingilia siasa.

Siku chache zilizopita,waliamua kutoa ahadi ya kutoa zawadi ya jina la mtaa uitwe kwa heshima ya Kiongozi mmoja wa dini,na hilo kwao haikuwa siasa imeingilia dini.Kiongozi yule kupewa mtaa kwa heshima yake,wengine waliguna,maana walijua ndio mwanzo wa kiongozi mzawadiwa kupoteza uhalali wa kuikosoa serikali na maovu yake,na pia ndio mwisho wa kiongozi kuwatetea waumini wake wanyonge kwa gharama ya zawadi ya jina la mtaa.

Hii inaturudisha nyuma katika maandishi ya kitabu cha "How The Church and Government Got The Same Bed".

Wakati wa utawala wa Kifashisti kule Italia,Mussolini aliona tishio la Kanisa Katoliki ktk kufikia malengo yake.Maana kwa wakati ule,kanisa lilikuwa na "kontroo "ya maisha ya kiroho na serikali ilikuwa na "kontroo" ya maisha ya kisiasa.

Alichokifanya Mussolin ni kujipendekeza kwa kanisa na kutoa "rushwa" ili yote atakayoyafanya kanisa katoliki lililokuwa na nguvu sana Italia libaki kimyaa.Alifanikiwa.

Kwanza aliamua kumbatiza mwanae wa kiume,ambaye hapo awali hakuwa amebatizwa.Hapa akaliteka kanisa kwa karata ya kwanza.

Pili aliamua kufunga ndoa ya kikanisa,baada ya kuwa amekaa miaka 11 na ndoa ya "bomani" na mkewe Rachele.Hii ikawa karata ya pili ya kujisogeza na kujiweka karibu na kanisa ili kutimiza malengo yake ya ufashisti.

Karata nyingine;aliamuru kufungwa kwa maduka yote ya vileo(wine shops) na kufuta leseni za sehemu za starehe zote za usiku ili kuendana na kauli ya kanisa ya kupunguza uovu mitaani kwa ulevi na anasa za usiku.Hapa kanisa katoliki likanasa mtegoni.

Alienda mbali mpaka akatangaza kuwa "Public Swearing" kama "Public Crime"...Yaani mwananchi ukiwa mtaani mnabishana,mtu akikwambia sema haki ya Mungu...Ukisema tu "Haki ya Mungu ntayafunga majizi yote,msema kweli ni mpenzi wa Mungu".Basi ujue wewe una kesi ya jinai ya kujibu.Hapa alitaka kulifurahisha kanisa kwa amri ile ya "Usitaje bure jina la bwana Mungu wako"(Kwa hiyo amri hiyo ingekuwa enzi hizi,kuna mtu angekuwa jela zamaniii,maana huwa anajiapiza sana mikutanoni)

Mussolini akaamuru kupigwa marufuku vidonge vya majira na kampeni zote za matumizi ya uzazi wa mpango kama ulivyo msimamo wa kanisa.Wakati huo wa 1920's kanisa lilitaka wanawake wabaki nyumbani ili kulea watoto na kukuza familia vyema.Mussolini akalipigia chapuo hili na kulitungia sheria ili kuwafurahisha wazee wa kanisa.

Akatunga sheria ambayo ilifutilia mbali talaka kwa ndoa hata za bomani.Hii ilikuwa ni njia ya kuungana na kanisa ktk ndoa ya mke mmoja na isiyo na talaka mpaka Mungu awatenganishe.

Ndoano hii ikanasa vizuri kwa kanisa.
Hawakupepesuka wala kutikisika.Mambo yote ya ndoa yakaondolewa serikalini na kubaki kuwa "Full Control of the Catholic Church".Wale wapenda mteremko wa ndoa za bomani wakakosa pa kwenda.

Akatoa 109 acres ktk mji wa Roma ili yajengwe makao makuu ya Papa(Vatican) baada ya kuwa yalipokonywa wakati wa "Unification of Italy" ya miaka ya 1870's,na akaamuru kanisa lilipwe zaidi ya £130 milioni kwa wakati ule.Hii ilikuwa ni ndoano iliyoingia sawasawa kwa kanisa,na kanisa halikusema lolote juu ya "ufashisti" wa Mussolini hadharani;japo liliouona na kuuhisi kwake na kwa waumini wake.

Vatican ikawa nchi ndani ya mji,wakapewa mamlaka juu ya Post Office,jeshi dogo,polisi na "Rail station".Baada ya hapo,ugomvi ukawa ni nani anatakiwa "kukontrol" Elimu?Mussolini alihitaji elimu ili apandikize "ufashist" kwa watoto,na kanisa lilitaka elimu ili kupandikiza "dini" kwa watoto.

Mambo haya yote ambayo baadae,waumini wasio rasharasha waliona ni kama "rushwa" kwa kanisa ili liweze kusifia na kukaa kimya juu ya serikali ya kifashisti ya Mussolin yalifanikiwa.Si ajabu Papa John Paul II alikuja kuiomba jumuiya ya waumini na wasio waumini ktk jubilei ya miaka 2000 ya Ukristo kwa yale yote kanisa iliyoyakosea ktk kukuwa kwake.

Hakukuwa na Kardinali,askofu wala kasisi(padre) aliyeikemea serikali isiyo ya kidemokarasia ya Utawala wa Mussolini.Mengi yalitokea na kanisa lilikaa kimyaaa.Waumini waliteseka,waliumia na walipata machungu ya maisha...Lakini kanisa lilisema hewala,huu ni utawala mzuri tu,maana umerudisha heshima ya Papa katika nchi ya Vatican.

Kama kanisa la wakati huo lilibaki kimya juu ya ufashisti wa Benitho Mussolini,hili la kwetu la Tanzania,lisibaki kimya juu ya malalamiko ya wananchi,kutekwa kwa watu,kupigwa risasi kwa watu na kuongezeka kwa kasi uvunjifu wa haki za binadamu kwa mgongo wa hao wanaoitwa "Watu wasiojulikana".Kanisa la Tanzania lisikae kimya juu ya kauli za kibaguzi na zinazoligawa Taifa.

Hatumaanishi kuwa sasa Tanzania tuna "ufashisti",lakini tunakubaliana kuwa kwa sasa Tanzania maisha ni magumu,pesa imepotea na uchumi umenyambulika na kutikisika.Hii inaweza kuwa ni matokeo ya kipindi cha mpito kuelekea uchumi wa viwanda,lakini haiwezi kuwa sababu ya kutokusema ukweli kuwa "HALI NI NGUMU"

Tuwakumbushe viongozi wa dini wajibu wao,hata wale wanaoamua kunyamazia utekwaji wa watu,pengine ni kwa sababu wamezawadiwa majina ya mitaa.

Tuwakumbushe tu heri shari inayojengeka kutokana na kuali thabiti zinazoonyesha kuwatumikia watu na kuitumikia roho,kuliko kuendekeza uwoga na unafiki kwa manufaa ya zawadi za kimwili na sifa za kuwa karibu na wenye mamlaka.Ndio maana Lugha Mama ya Kanisa ya Kilatini ikasema "Nemo Liber Est Qui Corpori Servit" yaani "No One is Free who is a slave of his body"

Tuitumikie Roho inayodumu milele,kuliko mwili unaooza na kuliwa na nyenyere.
barafu wa JF
Machame,Kilimanjaro.
Naunga mkono hoja
 
Huu pia unaweza kuwa ni mtazamo sahihi,kwamba tusitake iongee kama Taasisi,bali mmoja kutoka katika hiyo taasisi.Upo sahihi na ninaweza kuwa sijaeleweka!!Ila katikati ya mistari yangu utamuona mlengwa

Mkuu nimependa sana maudhui ya post yako namba moja. Kwa huko Italy Mussolini aliweza hilo kupitia kanisa. Kwa hapa kwetu tabia hiyo inafanyika kupitia vyombo vya dola. Kumekuwa na matumizi ya vyombo vya dola kwenye maswala yasiyoyohitaji ushiriki wa vyombo vya dola hasa JWTZ. Ikafikia mpaka mahali kamisheni ya jeshi ikatumika kupokea wanaccm huku CDF akifurahi na kuamini ni kitendo kinachofanywa na rais mzalendo hivyo ni sawa bila kujali katiba inasema nini. Sasa hivi CDF anasimama na kutoa kauli unazoona kabisa ni za kuegemea mahali fulani kisa hao wanajeshi wanapata upendeleo fulani.

Kuna jambo lingine linaendelea japo linaonekana kufanyika kwa nia njema, lakini ukiangalia lengo lake ni kuteka taasisi za kidini kubariki mambo hayo, lakini lengo hasa ni kuziba taasisi hizo za dini kukemea mwenendo mbaya. Sasa hivi kila hafla ya kiserikali utaona viongozi wa dini wanaitwa kuomba, lakini ni mwiko kukemea kwani itaonekana wanataka kumkwamisha kiongozi anayeleta maendeleo.

Kuna dhuluma ya wazi kwenye chaguzi zetu tena zinazoratibiwa na vyombo vya dola, mpaka imefikia kwa baadhi ya vyama kutokushiriki, huku wapiga kura wakizidi kupungua. Na jambo hili linaonekana sawa kwani kinachofaidika na dhuluma hiyo ni chama cha kiongozi mzalendo. Hapa vyombo vya dola vimekuwa kimya kwani anayeamrisha hiyo dhuluma Anajali maslahi yao. Iwapo utaonyesha kupinga mwenendo uliopo sasa, hao viongozi wa dola utasikia lugha zao kwamba wanafuatilia lugha za kutaka kuharibu amani, kipigo cha mbwa koko, kupigwa mpaka mchakae. Wakati huo huo vyombo hivyo vya dola vikikaa kimya kuhusu mambo ya kutekwa, watu kupotea mpaka wengine kupigwa risasi.
 
Askofu Shoo ktk msiba wa Mengi kauli na matendo yake dhidi ya Makonda hayakuwa ya kiroho. Na pia hakupaswa kuachia madhabahu takatifu kutumika kisiasa tena ktk msiba wa mtu ambae tunamnadi kuwa mtu wa WATU.

Angefanya kikao cha awali cha usuluhishi kati ya Mbowe na Makonda kama aliona kuna umuhimu huo baada ya maridhiano ndio awalete madhabahuni pa bwana.

Makonda alikuwa sahihi kutaka apewe muda wa kufanya clarification na si kutumia madhabahu takatifu mbele ya jeneza la Mzee Mengi KUMSHURUTISHA aombe radhi.

Makonda ni kiongozi hata kama alikosea akiwa DSM kitendo cha kwenda Machame nahesabu ni sehemu ya kujutia kauli yake.

Otherwise niseme tu kilichofanyika pale ni askofu SHOO to condemn Makonda unheard. Which is great mistake against principals of natural justice.

Angekuwa anasifika alitakiwa asifiwe hapo hapo madhabahuni. Ndio hapo mleta mada anaposema mnachotaka kusikia ni kusifiwa tu tena hadharani, lakini kukosolewa iwe kichochoroni!
 
Hoja na mawazo yako ni mazuri sana.

Lakini upande wa pili lazima tuelewe kanisa likijiingiza sana ktk siasa au ukosoaji hadharani unaolenga upande wowote ikaacha kufanya hivyo na upande wa pili linaweza kuingia ktk lawama kama kanisa linalozipata kule Rwanda juu ya uhusika wake wakati wa mauwaji ya kimbali(genocide).

Kanisa lina nafasi kubwa ya kwenda kuionya au kuihoji serikali kwa mambo unayo taka liende kuhoji madhabahuni au majukwaani.

Katika hali ya kawaida mtu mkubwa au kiongozi au pengine mtu yeyote hukubali makosa na kujirekebisha bila kubishana au kuumizwa utu wake au tuseme 'ego' yake kama akiitwa faragha na kukosolewa.

Pengine ingekuwa busara kama Mbowe angeenda kumuomba Baba Askofu Shoo, Waziri Mkuu na Katibu Mkuu wa CCM bwana Bashiru wamuite Makonda faragha na kumuonya kisha wamtake aende kuomba radhi kwa kauli yake hadharani. Ile njia namna iliyotumika kanisani na kumtaka au kumlazimisha aombe radhi, kidogo ilikuwa ni kama kumjeruhi 'ego' yake na kumjeruhi kisiasa kitu ambacho kingeenda kumjenga Mbowe na chama chake.

Mfano wangu wa kuitana na kukosoana faraghani(privately) inatumika ofisini na katika familia.

Ukiwa kiongozi ofisini unapo ona mtu alie chini yako anakosea utamuita na kumkosoa au kumkanya mkiwa wawili au watatu faraghani.
Ni rahisi sana huyo mtu kujisahihisha kuliko ukamshambulia mbele ya wafanyakazi wenzie wengi.

Vivyo hivyo baba au mama akikosea mwenzie hatakiwi kumkosoa au kumkanya mbele ya watu au mbele ya watoto.

Na wazazi hawatakiwi kumkanya au kumgombeza mtoto mkubwa mbele ya wadogo zake.

Unampomsema au kumkanya mtu mkubwa au kiongozi mbele ya walio wadogo(kimamlaka) kwake unakuwa unampunguzia mamlaka (authority) yake kuweza kuwaongoza au kuwakanya walio chini yake pale wanapo kosea, maana ata dharauliwa na walio chini yake kwamba hastahili nafasi ile na hajui kitu.

Dhana hii hii ndio mnayotumia kumlalamikia Mh.Raisi anapo wawajibisha watu hadharani. Kwa hivyo Askofu Shoo, Mbowe na Bashiru wanafanya kile kile mnacho mlalamikia Magufuli.

Mwisho wa siku naunga mkono kukosolewa Makonda kwa kauli ile ya Ubaguzi lakini napinga namna alivyo rekebishwa katika tukio ka msiba tena kanisani na huku kamera za television zikirusha mubashara.

Wangapi kati yetu wangependa kukosolewa hadharani wakiwa wanarushwa kwenye TV na redio kibao huku wakifuatiliwa na malaki kama sio mamilioni ya watu? Huku mkeo na watoto wako na wazazi wako wakifuatilia?

Ile inaitwa kumuaibisha mtu na sio kumfunza mtu, na hakika kwa hulka na silika ya binadamu pale ndugu Makonda hawezi kukubali nafsini kwake ni lazima atatafuta namna ya kulipa kisasi. Na ndivyo ambavyo angefanya Titicomb, Askofu Shoo, Bashiru, Mbowe, barafu na mtu mwingine yeyote. It is about self esteem and personality.

Nashauri watu wapitie kitabu kimoja maarufu cha "How to make friends and Influence people" By Dale Carnigie.

Namna nzuri kwa viongozi wa makanisa na wa kiislam ya kumkosoa Magufuli au Makonda ni kuomba miadi ya kuonana nao na kuwaambia kwa faragha. Vinginevyo ni kujaribu kuwa 'undermine' 'authority' yao na kuwapunguzia approval rating yao na hiyo ni kazi ya viongozi wa vyama vya upinzani, sio kazi vya viongozi wa dini.
Viongozi wa dini lazima wacheze ktk neutral ground.

Ni kama kuwashinikiza maaskofu wawakanye kanisani na majukwaani viongozi wa upinzani wanao tumia lugha kali kama MDUDE na wengineo. Tuliona awamu ya nne ndugu Mbilinyi(Sugu) akitumia lugha kali isiyo na staha dhidi ya Waziri Mkuu Pinda wakati huo. Hatukuona wanaombwa maaskofu wamuweke kitimoto hadharani na matelevisheni ndugu Mbilinyi.

Ni hivi una maelezo mengi na mazuri, hilo sipingi. Kilichotokea jana ni coincidence hakuna aliyekuwa amejiandaa na kilichofanyika. Mbowe aliongea baada ya kupewa nafasi kama wengine, kwakuwa alikuwa na jambo lililomkera akalitolea ufafanuzi kwa kumkanya aliyesema maneno yale, kisha akaomba asamehewe kwa kauli zile lakini zisirudiwe. Askofu wakati wa mahubiri, kazi ambayo ni ya viongozi wa dini naye akakazia jambo hilo. Alipoitwa katibu mkuu wa ccm yeye ndio aliyemuita Makonda aombe msamaha na ikatokea yaliyotokea tena kwa nia njema.

Na hata kama ni huko faraghani unapopasema ni mara moja au mbili huyo Makonda ameonywa na bado habadiliki? Ni kurahisishie, huyo Makonda ni mtovu wa nidhamu na yeye anamtii tu Magufuli wengine wote ni bure. Hicho ni kiburi cha madaraka. Sasa kwa kukusaidia muite ww huko faraghani mwambie ajirekebishe.
 
Barafu;
Asante kwa madini uliyotema leo, nimesoma bila kuchoka huu uzi ni mtamu sana! Leo ndo nimeelewa vizuri kuhusu Mussolini .
 
Ni hivi una maelezo mengi na mazuri, hilo sipingi. Kilichotokea jana ni coincidence hakuna aliyekuwa amejiandaa na kilichofanyika. Mbowe aliongea baada ya kupewa nafasi kama wengine, kwakuwa alikuwa na jambo lililomkera akalitolea ufafanuzi kwa kumkanya aliyesema maneno yale, kisha akaomba asamehewe kwa kauli zile lakini zisirudiwe. Askofu wakati wa mahubiri, kazi ambayo ni ya viongozi wa dini naye akakazia jambo hilo. Alipoitwa katibu mkuu wa ccm yeye ndio aliyemuita Makonda aombe msamaha na ikatokea yaliyotokea tena kwa nia njema.

Na hata kama ni huko faraghani unapopasema ni mara moja au mbili huyo Makonda ameonywa na bado habadiliki? Ni kurahisishie, huyo Makonda ni mtovu wa nidhamu na yeye anamtii tu Magufuli wengine wote ni bure. Hicho ni kiburi cha madaraka. Sasa kwa kukusaidia muite ww huko faraghani mwambie ajirekebishe.
Makonda ni tatizo kubwa.
Nafikiri alitakiwa aondolewe ktk nafasi inayo muweka mbele kuwasiliana na umma.

Anatakiwa apelekwe mafunzo jinsi ya kuwasiliana na umma. Inamfaa zaidi nafasi kama ya ukurugenzi na nyingine za kutumikia nyuma ya pazia (underground) huku akijifunza mawasilano kwa umma.

Yeye na mkuu wa mkoa wa Tabora wakiona makamera na vipaza sauti wanapata mihemko na kuwa 'overwhelmed' na kuanza. kuvuka mistari.
 
Mtoa mada umesema kweli,Askofu Shoo ameonyesha njia,sasa na Kanisa Katoliki nao wasimame imara kukemea matendo maovu ya Serikali
 
Yaani una maana waige? RC ni taasisi, Dr. Shoo ni mtu individual
Kwani wakiiga jambo jema kuna Ubaya?Dr Shoo ni individual lakini yule ni Mkuu wa KKKT (Tanzania)kama taasisi pia,hivyo kauli yake ndio kauli kwa niaba ya Kanisa analoliongoza.
 
Ni wakati mwingine tena kauli ya Kiongozi Mmoja mkubwa wa kanisa la Tanzania imetikisa nchi.Hii ni sauti ambayo ilisubiriwa kwa muda mrefu toka kwa moja wa viongozi wa dini wanaoheshimika Tanzania.Hii ni kwa sababu,licha ya viongozi wa kisiasa kuwa na mamlaka na nguvu za kidola,bado viongozi wa kidini huwa na heshima na uaminifu wa kauli zao toka kwa waumini wao.

Ni bahati mbaya kuwa,tupo katika zama ambazo watawala tulionao wanajiona miungu watu,wanapenda kusifiwa,kutukuzwa na kuabudiwa.Wamejivika umalaika na ukuu usiohojika.Wanapenda kukemea pasipo wao kukemewa,wanapenda kuonya pasipo kuonywa na wanapenda kuwakosoa wenzao mbele kadamnasi ila wao wanapenda wasifiwe hadharani na kutukuzwa wakiwa faragha.

Imekuwa hivyo sehemu nyingi duniani,viongozi waliopo madarakani kuhakikisha kuwa "wanawateka" viongozi wa kidini ili wasikosolewe,wasionywe wala wasikemewe.Hii imeota mizizi pia hapa Tanzania.Watu hawataki kukosolewa,wanataka kusifiwa,hawataki kuonywa wanataka kuabudiwa,hawataki kukemewa wanataka kutukuzwa.

Juzi walipokaribishwa kumsimika kiongozi mkubwa wa dini kule nyanda za juu kusini,waliposifiwa na kuabudiwa,hawakusema kuwa "siasa imeingia kwenye dini",ila wakikosolewa wanasema dini imeingilia siasa.Juzi walikaribishwa pale Mwenge,kwenye kanisa binafsi la mtu,na walipewa nafasi ya kuhubiri kama wachungaji na kutafsiri vifungu vya biblia,hawakusema kuwa wanasiasa wameingilia dini.Askofu mwenye kanisa lake akawasifia na kuwatukuza,hawakusema dini imeingilia siasa.Ila wanapoonywa na kukosolewa,wanang'aka na kupayuka kuwa dini imeingilia siasa.

Siku chache zilizopita,waliamua kutoa ahadi ya kutoa zawadi ya jina la mtaa uitwe kwa heshima ya Kiongozi mmoja wa dini,na hilo kwao haikuwa siasa imeingilia dini.Kiongozi yule kupewa mtaa kwa heshima yake,wengine waliguna,maana walijua ndio mwanzo wa kiongozi mzawadiwa kupoteza uhalali wa kuikosoa serikali na maovu yake,na pia ndio mwisho wa kiongozi kuwatetea waumini wake wanyonge kwa gharama ya zawadi ya jina la mtaa.

Hii inaturudisha nyuma katika maandishi ya kitabu cha "How The Church and Government Got The Same Bed".

Wakati wa utawala wa Kifashisti kule Italia,Mussolini aliona tishio la Kanisa Katoliki ktk kufikia malengo yake.Maana kwa wakati ule,kanisa lilikuwa na "kontroo "ya maisha ya kiroho na serikali ilikuwa na "kontroo" ya maisha ya kisiasa.

Alichokifanya Mussolin ni kujipendekeza kwa kanisa na kutoa "rushwa" ili yote atakayoyafanya kanisa katoliki lililokuwa na nguvu sana Italia libaki kimyaa.Alifanikiwa.

Kwanza aliamua kumbatiza mwanae wa kiume,ambaye hapo awali hakuwa amebatizwa.Hapa akaliteka kanisa kwa karata ya kwanza.

Pili aliamua kufunga ndoa ya kikanisa,baada ya kuwa amekaa miaka 11 na ndoa ya "bomani" na mkewe Rachele.Hii ikawa karata ya pili ya kujisogeza na kujiweka karibu na kanisa ili kutimiza malengo yake ya ufashisti.

Karata nyingine;aliamuru kufungwa kwa maduka yote ya vileo(wine shops) na kufuta leseni za sehemu za starehe zote za usiku ili kuendana na kauli ya kanisa ya kupunguza uovu mitaani kwa ulevi na anasa za usiku.Hapa kanisa katoliki likanasa mtegoni.

Alienda mbali mpaka akatangaza kuwa "Public Swearing" kama "Public Crime"...Yaani mwananchi ukiwa mtaani mnabishana,mtu akikwambia sema haki ya Mungu...Ukisema tu "Haki ya Mungu ntayafunga majizi yote,msema kweli ni mpenzi wa Mungu".Basi ujue wewe una kesi ya jinai ya kujibu.Hapa alitaka kulifurahisha kanisa kwa amri ile ya "Usitaje bure jina la bwana Mungu wako"(Kwa hiyo amri hiyo ingekuwa enzi hizi,kuna mtu angekuwa jela zamaniii,maana huwa anajiapiza sana mikutanoni)

Mussolini akaamuru kupigwa marufuku vidonge vya majira na kampeni zote za matumizi ya uzazi wa mpango kama ulivyo msimamo wa kanisa.Wakati huo wa 1920's kanisa lilitaka wanawake wabaki nyumbani ili kulea watoto na kukuza familia vyema.Mussolini akalipigia chapuo hili na kulitungia sheria ili kuwafurahisha wazee wa kanisa.

Akatunga sheria ambayo ilifutilia mbali talaka kwa ndoa hata za bomani.Hii ilikuwa ni njia ya kuungana na kanisa ktk ndoa ya mke mmoja na isiyo na talaka mpaka Mungu awatenganishe.

Ndoano hii ikanasa vizuri kwa kanisa.
Hawakupepesuka wala kutikisika.Mambo yote ya ndoa yakaondolewa serikalini na kubaki kuwa "Full Control of the Catholic Church".Wale wapenda mteremko wa ndoa za bomani wakakosa pa kwenda.

Akatoa 109 acres ktk mji wa Roma ili yajengwe makao makuu ya Papa(Vatican) baada ya kuwa yalipokonywa wakati wa "Unification of Italy" ya miaka ya 1870's,na akaamuru kanisa lilipwe zaidi ya £130 milioni kwa wakati ule.Hii ilikuwa ni ndoano iliyoingia sawasawa kwa kanisa,na kanisa halikusema lolote juu ya "ufashisti" wa Mussolini hadharani;japo liliouona na kuuhisi kwake na kwa waumini wake.

Vatican ikawa nchi ndani ya mji,wakapewa mamlaka juu ya Post Office,jeshi dogo,polisi na "Rail station".Baada ya hapo,ugomvi ukawa ni nani anatakiwa "kukontrol" Elimu?Mussolini alihitaji elimu ili apandikize "ufashist" kwa watoto,na kanisa lilitaka elimu ili kupandikiza "dini" kwa watoto.

Mambo haya yote ambayo baadae,waumini wasio rasharasha waliona ni kama "rushwa" kwa kanisa ili liweze kusifia na kukaa kimya juu ya serikali ya kifashisti ya Mussolin yalifanikiwa.Si ajabu Papa John Paul II alikuja kuiomba jumuiya ya waumini na wasio waumini ktk jubilei ya miaka 2000 ya Ukristo kwa yale yote kanisa iliyoyakosea ktk kukuwa kwake.

Hakukuwa na Kardinali,askofu wala kasisi(padre) aliyeikemea serikali isiyo ya kidemokarasia ya Utawala wa Mussolini.Mengi yalitokea na kanisa lilikaa kimyaaa.Waumini waliteseka,waliumia na walipata machungu ya maisha...Lakini kanisa lilisema hewala,huu ni utawala mzuri tu,maana umerudisha heshima ya Papa katika nchi ya Vatican.

Kama kanisa la wakati huo lilibaki kimya juu ya ufashisti wa Benitho Mussolini,hili la kwetu la Tanzania,lisibaki kimya juu ya malalamiko ya wananchi,kutekwa kwa watu,kupigwa risasi kwa watu na kuongezeka kwa kasi uvunjifu wa haki za binadamu kwa mgongo wa hao wanaoitwa "Watu wasiojulikana".Kanisa la Tanzania lisikae kimya juu ya kauli za kibaguzi na zinazoligawa Taifa.

Hatumaanishi kuwa sasa Tanzania tuna "ufashisti",lakini tunakubaliana kuwa kwa sasa Tanzania maisha ni magumu,pesa imepotea na uchumi umenyambulika na kutikisika.Hii inaweza kuwa ni matokeo ya kipindi cha mpito kuelekea uchumi wa viwanda,lakini haiwezi kuwa sababu ya kutokusema ukweli kuwa "HALI NI NGUMU"

Tuwakumbushe viongozi wa dini wajibu wao,hata wale wanaoamua kunyamazia utekwaji wa watu,pengine ni kwa sababu wamezawadiwa majina ya mitaa.

Tuwakumbushe tu heri shari inayojengeka kutokana na kuali thabiti zinazoonyesha kuwatumikia watu na kuitumikia roho,kuliko kuendekeza uwoga na unafiki kwa manufaa ya zawadi za kimwili na sifa za kuwa karibu na wenye mamlaka.Ndio maana Lugha Mama ya Kanisa ya Kilatini ikasema "Nemo Liber Est Qui Corpori Servit" yaani "No One is Free who is a slave of his body"

Tuitumikie Roho inayodumu milele,kuliko mwili unaooza na kuliwa na nyenyere.
barafu wa JF
Machame,Kilimanjaro.
Hongera sana Mkuu Barafu, umejenga hoja vizuri sana, umeichambua historia vizuri kabisa. Tunahitaji kuwaambia viongozi wetu wa Kanisa Katoliki kwamba WAMEZIDI MNO KULA RUSHWA ZA SERIKALI. Kwa kweli wanachofanya hakina tofauti na UKAHABA. Niliumia sana wakati wa sherehe ya miaka 150 ya ukristu Tanzania kule Bagamoyo mwaka jana. yaani katika sherehe ile, Maakofu walidiriki kumwomba Magufuli kwamba wana mambo wanataka kumwomba, hivi wanaomba wakutane naye. walifanya hivyo huku kukiwa na matukio ya kunyanyaswa kwa Askofu mwenzao, Severin Niwemugizi, ambaye nadhani mpaka sasa hajarejeshewa paspoti yake. KANISA KATOLIKI MNATUAIBISHA WAUMINI!!!!
 
Kwani wakiiga jambo jema kuna Ubaya?Dr Shoo ni individual lakini yule ni Mkuu wa KKKT (Tanzania)kama taasisi pia,hivyo kauli yake ndio kauli kwa niaba ya Kanisa analoliongoza.
Ungependa watoe hayo maneno lini?
 
Kwanza ndugu zangu wa JF naomba niwasalimu wote.

Pili naomba niseme ukweli wangu kutoka moyoni ya kuwa Leo katika Ibada ya Mazishi ya DR. MENGI, nimefurahishwa sana na kile alichosema ASKOFU DR. SHOO. Sababu kubwa ni hizi;

i.Amesema ukweli bila kuogopa kama muhusika yupo au la.

ii.Amewasemea wanyonge na wenye hofu ya kusema ukweli.

iii.Ametoa ushauri bila kuogopa wenye mamlaka kama wapo au la.

iv.n.k

Binafsi nimejiuliza, "JE KUNA KARDINALI, ASKOFU au PADRI MWENYE UWEZO WA KUVAA JAPO SOKSI TU NA SIYO VIATU VYA ASKOFU DK.SHOO AKIPEWA NAFASI YA KUSEMA NENO MBELE YA VIONGOZI WA SERIKALI?"
Kwani alivyosema Shoo haijatosha?
Kumbe na ninyi pia mnajua sauti ya wakatoliki ni kubwa zaidi siyo!!
Lakini ipo hivi,Kanisa lina utaratibu wake wa kusema,na likisema panatetema
 
Back
Top Bottom