Lissu alimkashifu magufuli kutokana na matendo na kauli zake- udikteta, ubaguzi, wizi wa kura, kuvuruga chaguzi, kununua wanasiasa wa upinzani, kuteka/kupoteza/kuuwa watu etc.Ndugu zangu watanzania,
Unatakiwa ujitoe ufahamu,ujizime akili na kujifanya kichaa na mwendawazimu kuamini neno lolote litakalo katika mdomo wa Tundu Lissu. Ni ujinga wa hali ya juu sana kwa mtu mwenye akili Timamu kumuamini Tundu Lissu kwa neno lolote litokalo kupitia mdomo wake. Lissu wa leo anayepiga makelele bila breki wala aibu kutaka kwenda kwenye kaburi la Hayati mwalimu Dr John pombe Joseph Magufuli ndiye huyo huyo kwa mdomo wake huo huo usio na adabu wala hekima wala staha aliongoza mashambulizi ya kumtukana sana hayati Magufuli,alimtukana mpaka akawa anatokwa na mate mdomoni katika kumporomoshea matusi Hayati Dr Magufuli. Akishirikiana na wahuni wengine aina yake alitoa kila aina ya ubaya kumpaka Hayati Dr Magufuli,aliiomba nchi zote za ulaya na Marekani zitutenge Tanzania na kutunyima chochote tulichohitaji,alitaka Taifa letu litengwe kimataifa kwa hoja kuwa Hayati Magufuli alikuwa ni kama shetani ndani ya Ardhi ya Tanzania na chochote alichofanya kwa Tanzania kilikuwa ni kama angamizo kwa Taifa letu.
Lissu kwa mdomo wake huo huo alipita hadi BBC shirika la habari la Uingereza akipayuka na kumtukana sana Hayati magufuli.hata alipoacha kuonekana hadharani na baadaye kutangazwa kifo chake ni Lissu huyo huyo aliyekuwa wa kwanza kufurahia sana kana kwamba yeye ataishi milele katika Dunia hii.ni huyo huyo aliyeendelea kurusha maneno ya kumfedhehesha na kumdhalilisha Hayati Dr magufuli hata pale alipokuwa amepumzika katika nyumba yake ya milele.
Sasa leo utaweza vipi kuamini neno lolote alitoalo Lissu kupitia mdomo wake? Ni vipi umuamini mtu huyu licha ya umri wake kuwa mkubwa lakini mwenye maneno ya kitoto na yaliyokosa adabu na heshima? Ni vipi aende na aruhusiwe kwenda kwenye kaburi la hayati Dr magufuli aliyemtukana na kufurahia kifo chake? Ni vipi mamlaka Imruhusu kufanyia siasa eneo alipo lala Hayati Magufuli? Anakwenda kufanya nini? Kwanini asiombe kwanza msamaha kwa kuita tena vyombo vya habari vya ndani na kwenda kuzunguka tena kwote alikokuwa anapita kumtukana Hayati ili aseme kwamba alikuwa anamsingizia Hayati Dr magufuli?
Ni vipi watanzania wenye akili Timamu wanaweza wakamuamini leo? Je hamuoni kuwa Lissu yupo kazini na anafanya hivyo kuvuruga amani ,utulivu na amani ya nchi yetu kwa maagizo ya watu anaowatumikia na wanao mfadhili? Uadilifu wa Lissu upo wapi kikauli? Hamuoni ni zaidi ya kinyonga? Hamuoni ni msaliti na aliye tayari kuleta machafuko hapa nchini hata kwa kutoa uongo wa aina yoyote ile kama afanyavyo leo? Kwanini tumuamini kwa sasa ili hali ni muongo kupindukia?
Mnakumbuka namna alivyomtukana na kumdhalilisha mh Edward lowasa majukwaani kwa miaka zaidi ya nane? Je huyo lissu kwa mdomo wake huo huo alisema nini ilipofika uchaguzi wa 2015 juu ya lowasa? Siyo yeye aliye anza kumsafisha kwa ulimi na mate ya Mdomo wake? Ni vipi leo kumuamini huyu kiumbe? Mnaanzia wapi watanzania wenzangu wenye akili Timamu?
Lissu ni wakupuuzwa na kumkemea kwa kauli zake za uongo,uchochezi ,ubaguzi na zenye kuleta na kuchochea uhasama hapa nchini,siyo wa kuendelea kumlea huku akieneza chuki na sumu ya ubaguzi pasipo kumchukulia hatua za kisheria na kutompatia vibali vya mikutano anayoitumia kupandikiza chuki na uongo kwa wananchi. Hana uadilifu wa kauli na hapaswi kuaminiwa hata kidogo.
Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel mwashambwa,kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.
0742-676627.
Lissu anasema anaenda kumshtaki huyu 'mwanamke' & co. kwa magufuli kwamba wameuza bandari zetu. Lissu hajasema kwamba sasa anamkubali magufuli, ila anataka kuwaambieni kwamba pamoja na ubaya wa magufuli, hii dhambi ya kuiuza nchi hangeitenda.
Au ulidhani anaenda kumfufua aongee naye?
Halafu hujitambui tu, wewe ndio mjinga wa hali ya juu, kichaa, mwendawazimu juha kabisa, mtu wa kujikomba. Huna, na hutoweza kuwa na hadhi ya Lissu.
Hivi hiyo numba unaweka hapo kila siku wanaume bado hawajakupigia tu?