Etwege
JF-Expert Member
- Jul 4, 2018
- 5,746
- 15,223
Mbunge wa Geita vijijini Joseph Kasheku alimarufu Dk Musukuma amesema alisikia kuwa Tundu Lissu anataka kwenda kwenye kaburi la Hayati Magufuli kumwombea na kumwambia namna ufisadi unaoendelea sasa hivi nchini ikiwemo kuuzwa kwa bandari zote za Tanganyika!
Dkt. Musukuma amesema kama mtu wa karibu na Hayati Magufuli na kama mwana familia ya Hayati Magufuli hawataruhusu hilo litokee kwani Lissu ametumia maisha yake kumtukana na kumdhalilisha Magufuli kwa tuhuma ambazo hana ushahidi wa kuwaonyesha watanzania hadi leo!.
Mbunge Musukuma amesema hataruhusiwa kwenda kunajisi kaburi la aliyekuwa rais wa awamu ya tano wa nchi yetu hivyo abaki akiongelea hukohuko majukwaani.
Dkt. Musukuma amesema kama mtu wa karibu na Hayati Magufuli na kama mwana familia ya Hayati Magufuli hawataruhusu hilo litokee kwani Lissu ametumia maisha yake kumtukana na kumdhalilisha Magufuli kwa tuhuma ambazo hana ushahidi wa kuwaonyesha watanzania hadi leo!.
Mbunge Musukuma amesema hataruhusiwa kwenda kunajisi kaburi la aliyekuwa rais wa awamu ya tano wa nchi yetu hivyo abaki akiongelea hukohuko majukwaani.