Elections 2015 Ni Tundu Lissu pekee(Sababu moja sifa kumi)

Wanajamvi habarini!

Niliweka post hivi majuzi na kuahidi kurudi tena na kuelezea kwa nini nimeamua kushawishi umma wa Tanzania ya kwamba TANZANIA ya leo inamuhitaji Tundu Lissu kama mwajiriwa mkuu wa wananchi.

wakati umefika na wakati ndio huu!

Utangulizi:

Nikijikita katika mada moja kwa moja napenda kusema kuwa Tanzania ya leo sio Tanzania ya Nyerere,hapa namaanisha sio Tanzania yenye maadui watatu yaani Ujinga,Umasikini na Maradhi...maadui hawa walishadhibitiwa usiniulize lini au na nani bali tulie tuelezane.

Watanzania wa leo wana elimu bwana...watu wanatumia simu,TV na teknolojia za kigeni bila shida.elimu ya msingi kwa sasa ni kidato cha nne,maelfu kwa maelfu ya vijana wako vyuo vikuu.hivyo sitarajii kumsikia mtu akilalamika juu ya watanzania kupata elimu iwe bora au hiyo hiyo ya kuungaunga...Adui alikuwa ni upatikanaji wa elimu na sio ubora wake!!!

Swali la kujiuliza jee elimu hii wanayopata vijana wetu hasa ile asilimia 75 ya wakulima na labda kwa kuongezea asilimia 10 ya wafugaji inafanana na ile wanayopata asilimia chini ya kumi ya tabaka la viongozi/masingasinga na washirika wao?

Hivi hii elimu waliyopewa watoto wa mbwa imelenga kuajiriwa au kujiajiri?

Watanzania wa leo sio maskini bwana.mabarabara ya lami kila kona,umeme vijijini wa kuwasha taa tu(wanakijiji wataanza kuchelewa kulala).Watu wanamiliki simu,toyo na mafundi cherehani wa sikuhizi hawajui kuweka viraka.Ukiongelea msosi hii sio issue tena kwani siku hizi hakuna kupanga foleni ya mkate huku kuna skonzi za Azam.

Umasikini hakuna tena...naam

Watanzania wa leo hawaumwi kipindupindu,Ukoma,vikope n.k watanzania wa leo wanaumwa dengue,B.P na rare cases kansa ya Tezi....
Isitoshe kuna zahanati au kituo cha kutoa huduma za afya kila kijiji.Adui alikuwa ni upatikanaji wa huduma za afya sasa zipo.

Jiulize sasa huduma hizi za hospitali hata ile zahanati kuu ya Muhimbili zinakujia kwa hisani ya nani?Jibu lako kaa nalo.

Wakuu msichoke naendelea na utangulizi.

ADUI WA TAIFA HILI NI YUPI HASWA KWA SASA??

Kabla sijamtaja ningependa kusema kuwa inawezekana miaka yote tuliyofanya uchaguzi hatukuwahi kuwa na ajenda kama taifa bali tuliendelea kuimbishwa kama kasuku kuhusu maadui hawa watatu.Sasa
ni wakati muafaka tukaingia kwenye uchaguzi huu tukiwa na ajenda ya pamoja.

Adui pekee aliyebaki Tanzania ni UFISADI...yaani huyu ndiye kubwa la maadui .Hata hayati JKN hakustuka au aliunderestimate uwezo wa Adui hili na ndio maana leo hii limekuwa kubwa la maadui.

Tanzania ya leo inakwamishwa na Ufisadi ama mfumo na mtandao wa kifisadi unaokuwa kwa kasi.....

Vijana wanakosa mikopo ya kusoma vyuo vikuu mpaka wanasingizia wazazi wao ni vilema au wafu ili tu wapate mkopo ilihali kuna mafisadi wamehifadhi vijisenti uswisi.

Madawa yanakosekana katika zile zahanati za kila kijiji ikiwemo ile zahanati kuu kisa ni madeni au labda watu wanataka kujipigia 10%

Kwa ufupi ufisadi ni janga janga janga la kitaifa kwani hata umeanza kukidhihirisha makanisani.

Tunahitaji kuwawajibisha,kuwachukia na ikiwezekana kuwapoteza.

Kazi hii hahitaji mtu legelege bali mwenye dhamira na tabia isiyokoma ya kuwa na misimamo isiyoyumba....Hii ndio SABABU MOJA YA KUMPA LISSU KIJITI KWA TIKETI YA UKAWA.

Tunapomkabidhi Mama Tanzania tumwambie kazi yako ni moja tu ya kutuondolea ufisadi na mafisadi.

Kama ni viongozi tunao tunachohitaji ni kuwaondoa viongozi wenye nasaba za kifisadi.

Kama ni madaktari au waalimu au majaji wapo na tutaendelea kuwapata lakini tunahitaji kusafisha watumishi wote wenye genes za kifisadi.

Hatuna uhaba wa maafisa ugavi au wahasibu wanaoshiriki ufisadi tunahitaji kuzalisha wagavi au wahasibu waadilifu n.k n.k

SIFA KUMI ZA TUNDU LISSU KWA MUKTADHA WA HOJA HII

1-Tundu Lissu ni mkweli kwa kimombo yuko Honest.mara nyingi hujiweka wazi katika misimamo yake na hivyo kuwafanya wake kumuelewa na wao kuamua au kuchukua upande.Kijiko hukiita kijiko na sio beleshi dogo!

2-Maono/Malengo yaliyonyooka ama kwa kimombo niseme anaweza kufocus.
Kama uliwahi kumsikiliza bungeni basi utajua hajaikosa hii tabia kwani hata panapotokea distractions kama vile kutukanwa basi yeye hubaki katika mstari na kuendelea kukifafanua au kukifikia kile anachotaka.

3-Heshima kwa utu.Toka mwanzo wa siasa/harakati Tundu lissu amejikuta akipambania utu wa mwanadamu,rejea harakati za migodini.

4-Uwezo wa kujenga hoja na kushawishi.
Hili ni jambo muhimu kwani ukienda Zanzibar Tundu Lissu ameweza kuwavutia wazanzibar mpaka kupachikwa jina la Messi wa Ukawa.Naweza kusema hakuna kiongozi kutoka bara tena mkiristo anayeweza kuwa na ushawishi kwa upande wa zanzibar isipokuwa TL.iwe ndani au nje ya UKAWA.

Na hii ndio turufu muhimu kwa UKAWA kwa wakati huu.

5-Ujasiri
Tundu lissu hajawahi kuogopa especially kuwaogopa mafisadi.

6-Ujuvi au labda kwa lugha ya malkia niite Arrogance.Arrogance ni tabia isiyopendwa na wengi lakini Tabia hii ndio inayohitajika pindi unapopewa kazi ya kipambana na mafisadi papa na watumishi wajuaji.

pia ni sifa hii inayohitajika pale utakapokutana na mataifa makubwa yanayotaka kunyakua rasilimali za nchi hii.

7-Ni kijana na bado ni mkakamavu.

8-Ni mwanasheria nguli anayejua kucheza na sheria na hiki ndio kiama cha mafisadi kwani watafilisika kwa kukodi mawakili wa kupambana na Rais mwenye dhamira ya kuwanyoosha.

9-Ameishi na kukulia katika umasikini.Amekumbana na kuchukia dhahma za kuchangishwa michango ya kipuuzi huku kodi zikiliwa na mafisadi.

10-Anajifunza na kucope na mazingira kwa haraka.Uwepo wake ndani ya bunge baada ya Dr Slaa kuondoka umekuwa ni chachu ya mabadiliko nchini.


Nimalize kwa kusema kuwa Tundu Antiphas Mughwai Lissu ni aina ya kiongozi anayehitajika kwa sasa.Tuungane kutokomeza ufisadi.

Hata Bibi Bomba wa kule Bungeni anamkubali TL hata Mnyika pia. TL akiingia kwenye lango la CCM hawatoki. Anacheka na nyavu zao kama alivyocheka nazo kwenye jimbo lake katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa.
 
lisu ni wakili makini hakuna AG tanzania wa kufanana nae anae juwa sheria kama yy. kimsingi anahitaji muda zaidi wa kujijenga kisiasa. mheshimiwa yuko makini sana kisheria na huo ndo ukweli hata kama mimi ni ccm
 
lisu ni wakili makini hakuna AG tanzania wa kufanana nae anae juwa sheria kama yy. kimsingi anahitaji muda zaidi wa kujijenga kisiasa. mheshimiwa yuko makini sana kisheria na huo ndo ukweli hata kama mimi ni ccm

kwa mfano Lissu akifa leo, nani atachukua nafasi yake?
 
Hivi nyerere alikuwa malaika hata asifanye makosa? je asikosolewe? mkapa kafanya mangapi lakini anakosolewe? mzee mwinyi mbona anakolewa? amefanya mengi tu mema mbona hamuongei? lisu kama anataka kugombea afanye hivyo mwisho wa siku watz wataamua anae washwa nani? tanzania ya leo si kama ya zamani watu ndo watakao amua
 
Alafu lissu atashindwa kuulinda Muungano, ni bora ya Kikwete. Mtazamo wa Lissu juu ya Muungano wetu ni hasi sana.
 
Hebu tuwekee matokeo yake ya mtihani, kuanzia darasa la Saba, form four, form six, first degree GPA na masters GPA tumcheki kama ubongo unachaji. Mambo ya kurudia kuwa na raisi wa GPA 2.1 mvivu hata kupitia hotuba hata ripoti ya cag hasomi hatuyataki...

Ila naskia huyu jamaa hajawahi kuomba wala kupokea rushwa, kama ni kweli magamba watasanda

Eeeeeeehhheeeee mkuu huyo tundu lissu ni noma sana yaani wakiweka hapa cv yake jamaa yuko vizuri huyo acha.
 
..mleta uzi umefanya kazi nzuri kumchambua mh.Lissu...ili watanzania wengi wazidi kumjua...maana hakika watu kama hawa wanahitajika kwa ukombozi wa mkwamo unaoikabili TZ ya leo....Taifa hili linahitaji sana rais mithili ya Lissu ili kuwakoma nyani kilagi...maana hakika taifa hili linaangamizwa na mafisi na manyang'au walafi...

...Nitaunga mkono uteuzi wa mtu huyu kugombea urais kwa nguvu zangu zote...na namwombea uzima kwa mola...ili siku moja aliongoze taifa hili...Siwaoni watu/wanasiasa wengi kama Lissu katika taifa hili...
 
Tumia akili. Lisu humjui wee. Huyu tundu lisu ni mtu wa haki na usawa. Unafiki hapendi. Halindi haki kutumia unafiki au ulaghai. Muungano una haki zake ili uwe imara utoke kwenye migogoro. Huwez linda muungano kwa mtutu wa bunduki ikiwa una kasoro. Njia pekee ni kutoa hizo kasoro. Na tundu lisu anazitoa hizo kasoro ndo maana zanziba kule wanamuita ronaldo wa realy madrid. Hutaki meza wembe.

Sio swala la kumeza wembe.
Lissu yuko very volatile kwenye swala la muungano.

Ni mtu anayekubaliana na aina nyingi sana za Muungano,kumbuka Muungano sio haki ya Binaadamu, Lengo kuu la Muungano ni kutengeneza dola yenye nguvu kwa namna zote, sio swala la haki.

Tunataka Rais atayejikita kutufanya sisi ni Taifa kubwa lenye nguvu,hata kama hati za muungano ni fake.
 
Tatizo lingine la lissu ni kwamba, anaweza kuharibu kabisa confidence ya mahakama kutimiza wajibu wake bila kuingiliwa. Lissu ni mtu ambaye haziamini kabisa mahakama zetu.

Akiwa rais anaweza kulazimisha Mahakama ziwe chini ya ofisi ya Rais, kitu kitakachotuingiza matatani na nchi wahisani.

Yes kwa mahakama zenye mahakimu na majaji wanaopokea hongo lazima confidence iharibiwe na huu ndio umuhimu wa Lissu kwa sasa.

watu wanajichukulia sheria mikononi kwa kuwa hawaamini mfumo wa mahakama au wa kipolisi.Ni ujinga kuendelea kuwa na mahakama ambayo ni kichaka cha mafisadi na wawekezaji mithili ya singasinga,hii weakness ya mahakama imetumiwa na mafisadi,wanasiasa walaghai,wawekezaji feki,wauza unga na hata serikali yenyewe kwa manufaa binafsi na sio ya umma.watu wanaiba wakijua tutawafikisha mahakamani na watahonga watatembea mbele.
 
lisu hakuwahi kurudia mtihani kama lameki kidevu...,hapo ndipo nitapiga kura yangu kwa mara ya kwanza.
 
Alafu lissu atashindwa kuulinda Muungano, ni bora ya Kikwete. Mtazamo wa Lissu juu ya Muungano wetu ni hasi sana.
mtizamo wa Lissu kuhusu muungano ni reflection ya mtizamo na maoni ya jamii yetu kufuatia utafiti wa tume ya jaji warioba.Jiulize kwa nini amekubalika Zanzibar na Bara pia?By the way unafahamu misimamo juu ya muungano ya hao wagombea urais wanaotajwatajwa?Nimesema hapo juu kuwa sifa moja wapo ya Lissu ni kuishi na kuusema ukweli hakuna unafiki wala mawaa ndani yake.watanzania wa leo si wale wa miaka hiyo....watanzania wa leo wanahoji na wanataka majibu yenye tija na sio uongo uongo.
 
Tundu Lissu ni mropokaji na mpiga makelele anayetumia uwezo wake wa kuropoka na kuongea kwa sauti ya ukali kuweza kuwashawishi na kuwaaminisha watu kuwa anachokisema ni kweli. Hawezi kuwa mwanasheria bora huku hata hajui kama kinga ya Mbunge kwa kile anachokisema bungeni ni kwenye suala la madai tu na si kosa la jinai.
 
Sio swala la kumeza wembe.
Lissu yuko very volatile kwenye swala la muungano.

Ni mtu anayekubaliana na aina nyingi sana za Muungano,kumbuka Muungano sio haki ya Binaadamu, Lengo kuu la Muungano ni kutengeneza dola yenye nguvu kwa namna zote, sio swala la haki.

Tunataka Rais atayejikita kutufanya sisi ni Taifa kubwa lenye nguvu,hata kama hati za muungano ni fake.

Muungano huanzia mioyoni mwa wanaoungana. Huwezi kuunganisha watu bila kuwapa faida zao za kuungana. Unapaswa kuwaambia hao watu watafaidikaje na muungano na uwasikilize wao wakupe aina ya muungano wanaoutaka na sio ule watawala wanaoutaka wao kwa maslahi yao. Muungano wowote ni lazima pande zote mbili zinufaike na kuungana kwao. Huwez sema muungano sio suala la kupata haki sawa sasa huo utakuwa muungano wa viongoz wachache kwa maslahi yao na sio wa watawaliwa yani wana nchi. Unahitaji uelewa kwenye swala la muungano wew. Hoja za kuwa taifa kubwa bila wananchi wake kuridhia ni ulaghai wa watawala. Upo hapo?
 
Unayosema nikweli ila cdhani km upole umelisaidia Taifa hili...kwa jazba ni kweli TL yuko hivyo lkn sasa ikiwa tumetawaliwa na wapole kwa miaka mingi nahakuna tulichofanikiwa cmbaya tukaongozwa na wenye jazba huenda wakatuvusha km Taifa

Inayohitajika ni jazba iliyochanganyika na busara. Jazba ya Tundu Lissu, waulize wananchi wa kijiji cha Mahambe, Wilaya ya Ikungi. Jazba yake inatokana na dozi ya dawa alizopewa pale hospitali moja ya Dodoma. lakini kama hatuamini, agombee urais mwaka huu, tutampigia kura lkn tuwe tayari kwa matokeo ya urais wake.
 
mtizamo wa Lissu kuhusu muungano ni reflection ya mtizamo na maoni ya jamii yetu kufuatia utafiti wa tume ya jaji warioba.Jiulize kwa nini amekubalika Zanzibar na Bara pia?By the way unafahamu misimamo juu ya muungano ya hao wagombea urais wanaotajwatajwa?Nimesema hapo juu kuwa sifa moja wapo ya Lissu ni kuishi na kuusema ukweli hakuna unafiki wala mawaa ndani yake.watanzania wa leo si wale wa miaka hiyo....watanzania wa leo wanahoji na wanataka majibu yenye tija na sio uongo uongo.

Mueleweshe huyo hajui. Wazanzibari wanamuita ronaldoooo.....akawaulize wazanzibari kuwa lisu ni nani.
 
Inayohitajika ni jazba iliyochanganyika na busara. Jazba ya Tundu Lissu, waulize wananchi wa kijiji cha Mahambe, Wilaya ya Ikungi. Jazba yake inatokana na dozi ya dawa alizopewa pale hospitali moja ya Dodoma. lakini kama hatuamini, agombee urais mwaka huu, tutampigia kura lkn tuwe tayari kwa matokeo ya urais wake.

Hakuna asiekuwa na jazba duniani hatamaandiko matakatifu yanasema kuweni na hasira ila msitende dhambi. Je, ni wapi lisu alikuwa na hasira akatenda dhambi yakuuwa? Hata Mungu mwenyewe ana hasira sembuse Binadamu!? Naona hamna baya la lisu badala yake mnataka kufanya personal attack kwa chukibinafsi tu hapa. Hamnaga kitu kibaya kama uvivu wa kufikiri kwani hilo ndo tulichokosea tukamchagua kikwete eti kisa ana sura nzuri na ni mshikaji wa night club matokeo yake amekuwa mdhaifu kuliko hata mm.
 
Unaua kabisa ndugu yangu,kumbe nchemba ndo walewale
Mnyika ni namba nyingine, darasa la Saba aliongoza mkoa na form four akapata point Saba. Ndio maana akili ya Mnyika inachaji Sana...

Angalia watu waliofeli darasa la Saba na kurudia mara tatu kama Sospeter Muhongo, au waliorudia mara moja moja kama HKigwangali aka Saidi Bagaile au Lameki Madelu aka Mwigulu Nchemba walivyo watu wa kukurupuka na kutotumia akili. Sio kwamba hawapendi kutumia akili, ila hawana hiyo akili. Nadhani umeelewa kwa nini nataka kujua matokeo ya awali ya TL sasa.
 
Back
Top Bottom