Ni simu gani smartphone uliwahi kuikubali kwa sababu ya chaji na vitu vingine?

Kuna simu inaitwa "Doogee 88" ...ni hatarii fireee, sema kibongo bongo haipatikani kabisa mpaka ku order mbelefele. Or else unaeweza jiweka Samsung M62.
 
Simu nzuri na inayotunza chaji muda mrefu ni samsung Galaxy A12. Katika uzuri wa muonekano na uimara hiyo ni mojawapo. na bei yake pia inaendana na ubora wake.
 
Mimi ni mpenzi wa iphone muda mrefu, sijawahi kupenda android phones, ,kuna kipindi niliamua kununua infinix hot 10 liteโ€ฆ.hii infinix haijawahi kuniangusha aisee, inakaa sana na chaji na haistuck kabisa, sema infinix wanachofeli ni upande wa camera tu
 
nilishatumia Samsung na iPhone ,kuna kununua infinix nikajiuliza nilichelewa wapi,data on mda wote na chaji iko vizuri tu
Nimetumia sumsung miaka saba na iPhone miaka mitatu ila ila infinix inanifurahisha
 
Ni kweli infinix kwenye picha ndio wamefeli ila ni simu nzuri
Mimi ni mpenzi wa iphone muda mrefu, sijawahi kupenda android phones, ,kuna kipindi niliamua kununua infinix hot 10 liteโ€ฆ.hii infinix haijawahi kuniangusha aisee, inakaa sana na chaji na haistuck kabisa, sema infinix wanachofeli ni upande wa camera tu
 
nina mashaka utumie SAMSUNG na IPHONE
kisha uhamie INFINIX na Uisifiee

kwanza hilo neno "Data on mda wote" huwa ni la TECNO user

watumiaji haswa wa SAMSUNG na IPHONE huwa hawajipigi kifua mbele DATA ON MUDA WOTE
mkuu Sasa unabisha experience ambayo nimepitia wakati mtumiaji ni mimi,wabongo mmezoea kufanga ligi kila kitu
 
nimetumia android(xiaomi,samsung,htc), ios,na windows phone(lumia)
- operating system ,window phone was the best,kwa ukaribu ikifuatiwa na ios
-camera-samsung ni moto sana
-battery -xiaomi yangu ilikuwa kidedea
-value for price-xiaomi
-well rounded phone samsung
-overpriced-iphone
ukiniuliza unatamani kununua simu ipi huko baadae
natamani microsoft afufue windowphone ,ila haitowezekana so ntabaki na samsung note yangu tu....ikichoka nitanunua foldable phone
sipangiwi mimi......imeisha hiyo.....
 
Nimetumia simu nyingii ila niliipenda s8 ndogo ya samsung kwa sababu napenda simu ndogo
Chaji ilikua average ila kila kitu kilikua plus kwanzia camera mpaka charge


Inaoyokaa na betri ilikua camon x tecno...such a nice phone inakaa na charge mpaka unashangaa afu camera was quite nice
 
Naona watu wengine tumejaribu kueleza simu zinazokaa na chaji muda mrefu, simu nyingi zilizotajwa ni zile zenye battery capacity 5000mAh, hata hivyo kukaa na chaji muda mrefu pia kunategemea na matumizi yako.
 
Back
Top Bottom