Ni sawa kwa Mama Tunu Pinda?

Status
Not open for further replies.
Nishakujibu kwamba hilo gari lenye nembo limetumika makusudi kuwaonyesha wazi watu kwamba kuna ujumbe wa familia ya PM hapa, hawakukosa shangingi la STK hawa watu wana magari kama wewe ulivyo na suruali labda.

Mwishowe utasema Waziri Mkuu asipande kwenye gari lenye nembo na mkewe, mkewe amfuate nyuma anajiendesha kwenye ki-Datsun.

unareason kitoto,acha na sisi tukupeleke kitoto unavyotaka,kwa hiyo hata kama angeenda mtoto wake na gari yenye nembo ni sawa tu,ili mradi watu waone gari la serikali? Swala hapa ni nembo ilitumika ipasavyo au wali miss use matumizi ya nembo?
 
Acha jazba, rudia kusoma ulichoandika then hoji ' itifaki' inasemaje kuhusu uwakilishi wa Waziri mkuu kwenye Msiba huo.

Tukisema bongo lala eti ni jazba, sasa mama pinda amuwakilishe waziri mkuu kwanini yeye ni sehemu ya serikali au ni ofisa wa ofisi ya waziri mkuu? Yeye anaweza kumuwakilisha Mizengo pinda kama sehemu ya familia na ndio maana kwa namna hiyo hawezi kutumia gari yenye nembo ya serikali. Ni vema ieleweke hatutaacha kukemea matumizi mabaya ya mali za umma na mmomonyoko wa maadili ya uongozi eti kwakuwa nchi ina matatizo mengine makubwa ie ajira, mfumuko wa bei nk sisi hatuna tatizo dogo wala kubwa yote yapaswa kukemewa kwa nguvu sawa!
 
  • Thanks
Reactions: Nzi
jamani huyu mama alikuwa beki3, sasa lazima ajionyeshe kwa mashosti zake kwamba she is somebody now, more over mtoto wa mkulima hana pingamizi kwake ili aendelee kumtunzia siri ambayo its no longer siri kwa wengi we2,hasa ukizingatia aliwatibua ma Dr.

hapo kwenye red, eti umesemaje (dadavua)?
 
ningependa kujua mama tunu ana kazi?? i mean kaajiriwa mahali? au ni mama wa nyumbani?

Hata kama alikuwa na kazi nyuma, mwenzako akipata cheo kama hicho unatakiwa kuwa nae bega kwa bega maana ndio kazi yako kumfanya aweze kufanya kazi vizuri
 
Hayo ndiyo matumizi mabaya ya rasilimali za taifa ndugu yangu.
Na siku hizi umezuka utaratibu ambao magari mengi ya serikali hasa vx G8 yakiwa na namba za binafsi na zingine vioo vya tinted zikiwa mitaani saa zisizo za kazi ukitaka kujua ni gari ya serikali angalia kwenye kioo kunakuwa hamna karatasi yoyote ie bima, l/licence, etc
 
Nimepitia blogu ya Michuzi na kuona Mama Pinda akiwa kwenye msiba wa Steve Kanumba. Lakini vilevile Mama Pinda kaenda pale akiwa kwenye gari ambayo ikiwa na nembo ya Taifa ambayo inatumiwa na Raisi au Waziri Mkuu. Je ni haki kwa mke wa Waziri mkuu au Raisi kutumia gari iliyo na nembo ya Taifa wakati wenyewe hawana hadho hiyo?

View attachment 51318

attachment.php
mkuu, uenda alikuwa na PM wakamwacha sehemu, watampitia badae
 
Aliyeandika wamekosa la kuandika ana ufinyu wa mawazo mama Tunu Pinda hakustahili kutumia gari ya serikali kwa mambo binafsi kama msiba wa bwana Marehemu Steven Kanumba angetumia usafiri wake binafsi kwani hata akitumia usafiri wake ulinzi si atakuwa nao kuwa na gari ya serikali haimaanishi ati ile nembo inaogopwa la sivyo kwa maana hiyo hapaswi kutumia gari ya serikali hata kama ni Pinda mwenyewe akienda kwa shughuli binafsi haruhusiwi kutumia gari ya serikali lakni kwa kuwa Tanzania kila kitu kinawezekana sishangai.Nakumbuka nilikuwa na ndugu yangu ambaye yuko serikalini huyu mzee kwa kweli tungekuwa na watu kama wale 10 kwa serikali naona nchi ingekuwa poa sana,nasema hivyo kwa kuwa wakati huo gari la serikali lipo lakini kama ana shughuli zake binafsi hata siku moja sijawahi kumuona akitumia gari ile alikuwa anatumia kigari chake ki Mark2 mpaka hata mke wake yuko aaah sasa mzee umezidi lakini Uncle hakusikiliza ushauri wa Shangazi kama ni shamba tulitumia ile Landrover Discover na mzee alikuwa anasema ni jinai kutumia gari ya serikali kwa shughuli zangu binafsi na mzee huyu alikuwa kigogo wa wizara nyeti sana tu lakini alikuwa hana makuu kabisa.huyu hakika alikuwa kiongozi.
 
Hii kitu mie nimeiona pahala tofauti kwenye shughuli mbalimbali; hawa wake za VVIPs wote wana hizo nembo, lkn naona hawapeperushi bendera ya Taifa maana hawapaswi kufanya hivyo ni Pm na Vpsd ndo wanapaswa kupeperusha bendera hiyo hata mawaziri hawapeperushi bendera ya Taifa panapo uwepo wa VVIP; hivi hakuna shughuli hapa karibuni chunguza hii kitu utagundua"
 
WATU WABAYA HAWAJIFICHI MANENO NA MIENENDO YAO INAFANANA.
SWALI: Jamaa akitaka kwenda ukweni KANYIGO kutoa mahali (Kama talaka ikitoka) hatatumia gari la Chama na kuweka sababu ya kuwa anakwenda kwenye ziara ya kukiimalisha chama? We Mb*** utajuwaje? Je, kama alikuwa katokea kwenye shughuli halali ya serikali na ikabidi apitie msibani! May be ktk msafala wake kuna mmojawapo (hata kama si yeye) msiba unamhusu! We utajuaje? Aende nyumbani kwanza akachukue gari lake aache la serikali huku watu wengine wanaendelea na sughuli za msiba? Ama achukue Tax na dereva arudishe Gari Magogoni? Basi huyo ni Waziri Mkuu KIVULI
HUO NI UNAFIKI NA WIVI MBAYA TENA WA AJABU KUONEA WIVU MAITIulikuwa unamtaka LULU nini? Basi jamaa kaondoka mchukue kama una jeuri **** we
 
Wana jf hamjui kuwa tz ni shamba la bibi kwa wachache wanaojiona tz ni yao?
 
magari ya Serikali twayaona sana usiku kwenye magesti ya huku Sinza.

Na hawakomi coz kila kukicha yanapigwa power window na vikolokolo vengine vya kuuzika maeneo ya Kariakoo Gerezani...

ila kwenye hizo picha nimeona wananchi wengi sana hapo! hivi hao wananchi sio serikali??

whatever we can say, sioni ubaya wowote ule......maana magari haya wanayatumia mpaka kwenye shughuli za ajabu, wanaendea mashambani kwao weekend n.k

kwa kifupi kama tumeishashindwa huko nyuma hatuwezi leo...labda kesho

imetoka hiyo

......acheni uvivu wa kufikiri....

huyu mama hana uwezo wa kuamrisha gari ya kwendea msibani,
waulizeni watu wa Protocol na wasemaji wa ofisi ya Waziri mkuu
kwanini 'itifaki' imemruhusu kutumia gari hiyo.

Kila siku mnayaona magari ya STK nk yakisubiri watoto shule mwajionea sawa tu..
Accountability mtihani ee?

UK!! we are Tanzanian for God sake!

Wakati mwingine kuiga mazuri si jambo baya.
Katika hili la matumizi ya magari ya serikali haswa kwa viongozi waandamizi (ukitoa rais, makamu wa rais, spika, waziri mkuu na jaji mkuu) wa serikali kama mawaziri, makatibu wakuu wa wizara, wakurugenzi wa idara na wakala za serikali, wakuu wa mashirika yanayotegemea ruzuku kutoka serikali kuu n.k., kuna haja ya kuiga mfumo wa serikali ya Uingereza.

Ambapo kuna mfumo was ministerial car pool; kiongozi wa wizara (waziri,naibu waziri, mkurugenzi, katibu mkuu) anapewa gari ya ofisi kama yupo London tu, na tena kama amebeba makabrasha muhimu classified documents/papers ambayo anaenda kufanyia kazi ofisini. Kama si hivyo, basi kiongozi huyo anapaswa aombe gari kutoka kwenye pool au atumie usafiri wa umma.

Sasa kwanini na sisi katika kuandaa katiba ya wananchi, tusifikiri namna gani ya kupunguza matumizi mabaya ya gari za serikali kwa kuiga mfumo huo?! Mfumo huo utawafanya viongozi hao wawe na nidhamu na magari hayo; tuna mifano katika vyuo vya umma, ambapo kuna mfumo wa car pool; ukitaka kutumia gari kwa shughuli ambazo haziko mahusiano ya moja kwa moja na ofisi, basi kodi gari kutoja kwenye pool. Ingawa mfumo huu waweza kuwa na mapungufu, lakini mimi naona faida nyingi kuliko hasara.

Viongozi wa waandamizi wa wizara kama hawana jambo la maana la kiofisi, basi hasitumie gari la ofisi; atumie gari lake binafsi, si anaenda kazini?! Pia matumizi ya gari la ofisi kama ana jambo la maana la kiofisi yawe yana mipaka na mahala. Kwa mfano, kama makao yetu makuu ya nchi ni Dar es Salaam, basi iwe ni kwa Dar tu; akienda nje ya Dar kiongozi akodi gari kutoka kwenye pool. Hili pia litaondoa kabisa utaratibu wa viongozi waandamizi wa serikali kutumia magari ya serikali kwenda kufanya kampeni za kisiasa kwenye majimbo yao na mahal apengine.
 
Nyie mnashangaa Mrs Pinda kutumia gari yenye nembo ya Taifa................hamjamuona Mrs Kikwete akisindikizwa na ving'ora akiw apeke yake!!...........sikuwahi kuona Mrs JKN au Mrs AHM au Mrs BWM kusindikizwa na ving'ora wakiwa peke yao i.e. bila waume zao.........
 
Usafiri anaweza kupewa, hilo hatuwezi kukataa lakini hoja hapa ni kwa nini atumie gari yenye nembo ya Taifa? Viongozi ambao dwanatakiwa kutumia nembo ya Taifa wake zao nao wanatakiwa kutumia?
Kama ni kwa mke wa Rais hilo nadhani sio tatizo kwani mke wa Rais ana hadhi inayotambulika kama first lady,na hii ni duniani kote. Kwa hadhi hiyo basi, tunaweza kusema si tatizo sana. Lakini kwa mke wa PM hasa katika nchi yenye mfumo wa utawala wa Rais mtendaji,inaleta ukakasi kidogo.
 
Nyie mnashangaa Mrs Pinda kutumia gari yenye nembo ya Taifa................hamjamuona Mrs Kikwete akisindikizwa na ving'ora akiw apeke yake!!...........sikuwahi kuona Mrs JKN au Mrs AHM au Mrs BWM kusindikizwa na ving'ora wakiwa peke yao i.e. bila waume zao.........

Ogah hebu acha kuudanganya UMMA; Mrs JKN,Mrs AHM na Mrs BWM hawatumii ving'ora kwenye mitoko yao hebu wacha kukurupuka uwe na uhakika na ukiletacho hapa"
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom