Rare Sapphire
JF-Expert Member
- Jul 24, 2021
- 576
- 1,626
Habari Wakuu,
Naamini wengi sio wageni na akaunti za watoto kwenye mitandao ya kijamii kama vile Instagram, Facebook, TikTok na kadhalika.
Akaunti hizi zinazofunguliwa na wazazi/walezi zimekuwa zikisimamiwa na wazazi wenyewe mara nyingi, na mara chache mtoto anaachiwa kuendesha account hiyo mwenyewe.
Wazazi/Walezi wengine huenda mbali zaidi na kufanya kama vile mtoto huyo anafanya mazungumzo kwenye akaunti hizo, yaani anaweka kitu pamoja na jibu kanakwamba mtoto wake wa miaka 2 au mitatu kajibu.
Akaunti hizi huwa na taarifa nyingi kumuhusu mtoto huyo kama vitu anavupenda kufanya, anavyopenda kula, picha mtoto akiwa ameweka pause tofauti tofauti, video ya matukio mbalimbali kama siku ya kuzaliwa ama mtoto akiwa anacheza, sehemu anayoishi ikiwemo na mazingira ya chumbani nk, shule anayosoma (kama ameanza shule) na mambo mengine kadha wa kadha.
Naleta kwenu mjadala huu tupate cha kujifunza kadri tutakavyoendelea, ni sababu gani zinazowafanya wazazi/walezi wafungue akaunti za kijamii kwa ajili ya watoto wao?
Naamini wengi sio wageni na akaunti za watoto kwenye mitandao ya kijamii kama vile Instagram, Facebook, TikTok na kadhalika.
Akaunti hizi zinazofunguliwa na wazazi/walezi zimekuwa zikisimamiwa na wazazi wenyewe mara nyingi, na mara chache mtoto anaachiwa kuendesha account hiyo mwenyewe.
Wazazi/Walezi wengine huenda mbali zaidi na kufanya kama vile mtoto huyo anafanya mazungumzo kwenye akaunti hizo, yaani anaweka kitu pamoja na jibu kanakwamba mtoto wake wa miaka 2 au mitatu kajibu.
Akaunti hizi huwa na taarifa nyingi kumuhusu mtoto huyo kama vitu anavupenda kufanya, anavyopenda kula, picha mtoto akiwa ameweka pause tofauti tofauti, video ya matukio mbalimbali kama siku ya kuzaliwa ama mtoto akiwa anacheza, sehemu anayoishi ikiwemo na mazingira ya chumbani nk, shule anayosoma (kama ameanza shule) na mambo mengine kadha wa kadha.
Naleta kwenu mjadala huu tupate cha kujifunza kadri tutakavyoendelea, ni sababu gani zinazowafanya wazazi/walezi wafungue akaunti za kijamii kwa ajili ya watoto wao?