Ni nini kinasababisha watu kuchepuka

Ni nini kinasababisha watu kuchepuka

tpmazembe

JF-Expert Member
Joined
Jan 5, 2012
Posts
2,469
Reaction score
588
Kuna kitu kinanishangaza mtu ana ndoa haina hata miezi sita anachepuka kwa kasi ya kimbunga, sasa kama aliyemuweka ndani hampendi alimuoa wa nini?

Au mkewe anakuwa hana ladha au ugomvi bora hata ndoa ya mwaka au miaka utasema wamechokana, sasa imekuwa mtu anakatisha haneymoon ili akachepuke.

Najiuliza nini kinasababisha
 
kuna kitu kinanishangaza mtu ana ndoa haina hata miezi sita anachepuka kwa kasi ya kimbunga, sasa kama aliyemuweka ndani hampendi alimuowa wa nini?
au mkewe anakuwa hana ladha au ugomvi bora hata ndoa ya mwaka au miaka utasema wamechokana, sasa imekuwa mtu anakatisha haneymoon ili akachepuke.

Najiuliza nini kinasababisha

Mkuu ndoa zenyewe mwayangu mwayangu "umelazimishwa tu, mbuzi kwenye gunia, ulimpa mimba demu, au wazazi wamekukomalia"
 
kukaa bila mchepuko ni sawa na kusafiri bila spea tairi, ndugu tafuta kazi ya nje wewe....
 
kama hakuna matatizo ya ndoa basi huwa ni hulka za mtu yeyote ambae ni malaya, huwa haridhiki na baada kuchepuka huuchepukia mchepuko mchepuko mwingine
 
Kabla ya kuolewa wanawajibika kila idara.Ile wakiwekwa ndani wanajisahau(Habari ndio hii)Utaki wewe jeuri..
 
Mmmh,,,,,,komenti za hapa, hili suala la kuchepuka ni janga la kitaifa kama si la dunia.
 
kuna kitu kinanishangaza mtu ana ndoa haina hata miezi sita anachepuka kwa kasi ya kimbunga, sasa kama aliyemuweka ndani hampendi alimuowa wa nini?
au mkewe anakuwa hana ladha au ugomvi bora hata ndoa ya mwaka au miaka utasema wamechokana, sasa imekuwa mtu anakatisha haneymoon ili akachepuke.

Najiuliza nini kinasababisha

1. Tamaa ya fedha au mwili
2.majaribio ya aina ya wanaume au wanawake
3.masuala ya kiimani, mfano pepo
4.kutoridhika kwa hali yoyote na mtu uliyenaye
5.mob psychology ( kutegemeana na uwezo Wa kufikiri Wa mtu)
 
Ukiwa na ndoo kichwani kidumu kiwe mkononi maana bahati mbaya ndoo ikalegaa kidumu kitakusave na pia Figa moja haliinjiki sufuria....
 
Back
Top Bottom