Ni nini kimeiangamiza shoprite. ?

Nelson Kileo

JF-Expert Member
Joined
Oct 29, 2011
Posts
3,054
Reaction score
3,265
Nini kimetokea mpaka Shoprite kishindwa kuendesha biashara zake Tanzania..? Mpaka kufikia kuuzwa kwa Nakumat .. ?

Mbali na hapo wameshindwa kulipa stahiki za wafanyakazi wake wakiwa na deni la zaidi ya million 400. . ,huku mwajiri akidaiwa kutaka kukimbia kurudi South Africa.

KUNANI NINI SHOPRITE.
 
Hawa jamaa si kwamba wameshindwa bali wanataka tu kuuza biashara na wasepe, Shoprite ni kampuni kubwa sana na hata siku moja huwezi ilinganisha na Nakumat, Na kuondoka kwa Shoprite ni pigo kubwa sana, Hawa Wakenya Nakumat bidhaa zao si mchezo, wanauza ghari sana,
 

Mkuu shoprite wameshindwa kulisoma soko la Tanzania! Mwanzoni walipiga bao kwa sababu kulikuwa hakuna ushindani!
Tatizo kubwa la Shoprite ni kwamba wame-fail katika products definition na market segmentation! Zaidi ya 70% ya products zao ni imported, kuanzia viazi, matikiti hadi vitunguu! Soko lao kubwa linawafaa foreigners, ila bahati mbaya sana huko foreigners wengi wanakoishi wana supermarket zao za kutosha kama Masaki, Oysterbay, Upanga na Mikocheni na hivyo kujikuta soko lao ni finyu sana kwani kuwepo kwa supermarket nyingi zinazouza bidhaa local kunafanya market share ya shoprite kuwa finyu! Watanzania wengi wanafanya shopping TSN, Uchumi na Shoppers kwani products zao nyingi ni locally oriented!
 

mmmh kweli mtu unaweza kuacha pessa
.na useme unakimbia tu... sidhani .. !
 
Nilisikia watu wakisema sababu ya shoprite kuuzwa ni baada ya kushindwa kulipa kodi serikalini.. ! sijajua kama kuna ukweli hapo .
 
Mkuu majibu yako wazi,mfano mzuri ni ile ya kamata ambapo waliwaachia wezi kuiba vifaa vya magari ya wateja
huku kampuni za ulinzi zikijitetea kuwa magari ya wateja siyo dhamana yao na kumwacha mteja akiingia gharama ya kutengeneza gari yake.Kuna rafiki yangu alifanyiwa unyama huo nikathibitisha na kuanzia hapo nilihama kufanya shopping kwenye maduka yao,naamini hata wengine waliofanyiwa watakuwa walihama.Na siyo siri watu wenye uwezo angalau kuanzia wa kati ndo wanaenda kwenye hizi centres sasa ukianzisha biashara ya kuwaibia vifaa vya magari yao
huku ukikwepa kuwajibika,wanahama na hivyo tegemea kufunga hiyo centre soon.
 

Hii pia ni moja ya sababu .

PARK AT YOUR OWN RISK.
 
hawa walipewa tax holiday,wameshakwepa kodi,wanampa mwingine nae akwepe kodi.
 
Hii pia ni moja ya sababu .

PARK AT YOUR OWN RISK.
Sehemu nyingi za parking zina ujumbe huu,na hata sokoni k'koo lakini inapotokea ukaibiwa
hakuna majibu ya ovyo bali walinzi wanakupa ushirikiano na unaona wanajali na kujitahidi kuchukua hatua za kudhibiti huo uharifu.Na ni lazima uwe makini na huduma unayotoa,kama huduma yako inahusisha watu kuja na magari na biashara/huduma unayotoa ina ushindani,ukaendekeza "park at your own risk" wateja wanasepa wanaenda wanakojua watapata huduma na watakuwa safe na mali zao.Ndipo utaona biashara yako inakufa
Sehemu za public service ambapo tunafuata huduma nasiyo kwenda kwenye matumizi hao ndo wanahaki ya kutumia huo mfumo.
 

hakika
 
mmmh kweli mtu unaweza kuacha pessa
.na useme unakimbia tu... sidhani .. !

Hapo umenena ni bora kuwa na doubt kuliko kuandika unachowaza kichwani tu.
Inavyosemekana ni kuwa, kwa wengi wanaojua bidhaa za supermarket zote zina barcode ambazo ukifika counter unalipa kwa kupitisha kwenye mashine kwa hiyo kilichokuwa kinafanyika ni wafanyakazi walikuwa wanafanya as a team wanaoweka label za bei mpaka wanaonunua (team) na alieko counter wanachofanya ni waweka label wanabandika bei ya mkate kwenye nyama as much as they can na hapo anakuja mteja na kubeba nyama nyingi kwa bei ya mkate kama utanielewa hapo, at the end of the day itaonekana mauzo ni mengi lakini profit hamna ndio maana wakaona hakuna njia ila kufunga tu
 
 
 
 
 
Mandela nielewe vizuri wanaonunua kwa bei rahisi ni jamaa wa wafanyakazi na wanajuana na wa ndani pia
 
je wafanyakazi wamelipwa stahiki yao?,serikali iliangalie hili kwa umakini mkubwa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…