Ni ngumu kuyapandisha maji mlimani

Extrovert

JF-Expert Member
Feb 29, 2016
67,092
173,803
Inasikitisha kuona kuna raia bado wanateseka na hili swala la mapenzi bila kujua ni vyema ukapenda pale ambapo unathaminiwa.

Mtu kama hakuoneshi ushirikiano ni aheri umuache tu ila cha ajabu mtu anateseka ila hashauriki sasa sijui ndio uchizi au niiteje. Kuvumilia nyodo za mwanamke sio ushujaa.

Screenshot_20210313-132957.png


Endapo unafikia hatua ya namna hii basi ni vyema kuamua kujikung'uta mikono na kusonga mbele kama injili.
 
Huyo jamaa anahitaji kupigwa shoti ya umeme kifuani ili kuushtua moyo uweze ku pump damu vizuri. Yawezekana flow ya dam mwilini mwake haipo vizuri, kuna baadhi ya sehem kama kwenye uti wa mgongo na kichwani damu itakuwa haifiki vizuri.
Ni jamaa yangu close na ukweli nimeshamwambiaga long sana kuwa hapo anapotea ila yeye anajifanya Mfilipino.

Yeye anawaza amvizie amjaze mimba ili amkamate ila pia sio suluhisho la kudumu.
 
Jackie akimpotezea Vickie ataumwa sana atakuwa anajishtukia tu ila Ni dharau sana mtu anakutumia jasho lake halafu unamfanyia nyodo za hivyo,, dhambi ndogo ndogo km hiyo iniepuke tu
Jamaa anampenda demu anatamani amuoe kabisa, alianza nae akiwa mdogo frm5 ila wakapotezana. Baada ya mtoto kuingia jiji la Makonda na kukamua 3 yrs IFM mambo yamekuwa magumu upande wa lango la upinzani 😁 sasa jamaangu anateseka anataka kujimilikisha koloni.
 
Ni jamaa yangu close na ukweli nimeshamwambiaga long sana kuwa hapo anapotea ila yeye anajifanya Mfilipino.

Yeye anawaza amvizie amjaze mimba ili amkamate ila pia sio suluhisho la kudumu.
Akimjaza mimba hapo atakuwa amejifunga kitanzi mwenyewe. Demu kama sio wa kutulia, hata akiwa na mimba hatotulia. Sana sana jamaa yako atajiongezea zigo la stress
 
Jamaa anampenda demu anatamani amuoe kabisa, alianza nae akiwa mdogo frm5 ila wakapotezana. Baada ya mtoto kuingia jiji la Makonda na kukamua 3 yrs IFM mambo yamekuwa magumu upande wa lango la upinzani 😁 sasa jamaangu anateseka anataka kujimilikisha koloni.
Kuna wanaume wagumu kuelewa ila Vickie nae sio kwa kupewa hela ya kula halafu akaleta nyodo angekuwa mstaarabu tu kujibu text zake hizo nyingine
 
H
Sawa lakini ndoa ni institution paana sana, hizi sms sio tosha kuona kama mke hakujali.

kuna baathi ya wanawake niwazuri kwenye mapenzi ya kwenye simu paka unatamani chart zake usizifute ila nyumbani ni pasua kichwa, kiburi dharau nk.
Huyu ni Gelofrendi tu ila anamzingua sana jamaangu. Kiasi kwamba anamfyatua akili maana hampendi dhahiri ila mchizi analiwa hela tu.😂😂😂

Na nilimwambiaga hiko kitu, kama demu hakupendi atakulia hela tu. Yeye asipotuma hela anapuuzwa ila anakomaa tu😹 anahisi demu atabadilika ampende
 
Back
Top Bottom