Ni Nchi gani hiyo

Ni Nchi gani hiyo

jrmlaurence

Member
Joined
Dec 2, 2010
Posts
80
Reaction score
57
tafadhali kama una jibu tusaidie tupate mkwanja:

• Nchi gani ambapo wadada hawataki kupewa maua siku za Valentine na birthday zao?
• Wapi ambako wazazi wote kila moja anadai alikuwaga wa kwanza darasani?
• Wapi ambako unaweza kuwa na leseni ya udereva wakati hujawahi kushika usukani hata siku moja?
• Wapi ambapo viongozi wa serikali hawajui kuimba wimbo wa Taifa?
• Wapi ambapo wananchi wanaweza kukuua kwa kuiba kuku na wakakuabudu kwa kuiba mabilioni?
• Wapi ambapo watu hugombania kuingia darasani, mpirani na hata kwenye mabasi?

• Wapi ambapo kila unaekutana nae amewahi kuibiwa simu?
• Wapi ambapo unaruhusiwa kulalamika kuwa ndugu zako wamekuroga kwa kila tatizo?
• Wapi ambapo matajiri wote wana vitambi?

• Wapi ambapo iPhone 5 zinauzwa kwenye foleni za magari kwa shilingi laki moja?
• Wapi ambapo kupata dhamani polisi lazima ulipie?

• Wapi ambapo basi la watu 25 linaweza kubeba watu 60.
• Wapi ambapo ukimsindikiza mtu eapot, anaweza akafika South Afrika wakati wewe bado uko kwenye foleni hujafika kwenu?
 
Back
Top Bottom