Ni nani aliyewaambia na kuwadanganya Wamisri kuwa wana umiliki wa 87% ya maji yote ya Mto Nile?

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Jul 13, 2013
56,623
108,986
Nilipoona tu tamko la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa likisema kuwa haliwezi Kuingilia kati Mgogoro wa Matumizi ya Maji ya Mto Nile kati ya nchi za Misri na Ethiopia kwakuwa inajua kuwa Misri ina uhalali wa 87% ya Maji ya Mto huo nimeshtuka na kuwa na maswali mengi mno.

Hivi ni lini Waafrika na hasa huu Umoja wa Afrika (AU) utasimama imara kabisa Kutetea na Kusimamia Maslahi ya Bara la Afrika na Rasilimali zake kwa ujumla? Kwanini iliyokuwa (OAU) miaka ya nyuma ilishindwa kuwa Sauti ya Kujiamini kwa nchi zote za Afrika ili Afrika tusikike, tueleweke na tuheshimike mno.

Hainiingii Akilini kabisa leo hii kusikia nchi kama za Misri na Ethiopia kila Uchao tu zinagombania Umiliki wa Mto Nile wakati sehemu Kubwa na iliyoanzia hadi hata kupita nchi kama za Uganda na Sudan nazo zina haki ya Umiliki lakini zimenyamaza na zikiwaangalia kama hata si Kuwashangaa pia.

Wazungu wanapenda sana Kutuingilia na Kutupangia mambo yetu mengi Waafrika na kwa jinsi Viongozi wengi wa Bara la Afrika walivyo Goi Goi na wa hovyo hovyo kiasi cha Kuwaogopa Wazungu hawa Waafrika wote tunadharaulika na kuonekana hakuna tunalolijua na hata kuliweza zaidi ya kuwa Waongo, Wavivu na Wachawi wa Kutukuka.
 
Wamisri walikua wanatupiga mkwara hata sisi kutumia hayo maji ya ziwa victoria nakimbuka waziri Mkuu kipindi hicho alikataa huo upuuzi na kuanza kusambaza maji huko Shinyanga na Mwanza hao Wamisri wanafanya mambo kihuni tu..inakera mno
 
Huwa najiuliza nani aliwamilikisha Masri hiyo 87% nakosa jibu. Labda wajuzi wa history watatujuza.
Sasa nimeanza kuamini Maudhui ( Content ) ya Kitabu alichoandika Rais Yoweri Museveni wa Uganda mwaka 1992 ambacho Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere aliandika Dibaji ( Fowerword ) yake chenye Title ya ' What is Africa's Problem ' ambapo Rais Museveni aliwalaumu mno Mababu zetu kwa Kuzubaa, Kutojitambua na Kuwaachia Wazungu wawatawale na kuwazidi Akili kiasi kwamba hadi sasa Waafrika tupo tupo tu kama Watu Wendawazimu na tuliolaanika wakati Utajiri Wetu mkubwa ndiyo unazitajirisha nchi za Wazungu hawa hawa.
 
Ila wa Ethiopia wabishi kinoma wamejenga Bwawa na wamehanza kuingiza maji , muda si muda itazuka Vita kati Wamisri Na Ethiopia
Hata Mimi pia hii Vita naiona inakuja Mkuu ila Mfaidika Mkuu wa Maslahi ya hii Vita ni Waingereza na Wamarekani ambao wanazichochea hizi huku Mmoja akimpa Misri jeuri ya Kumkopesha Pesa zaidi ya Miradi yake na mwingine akimuuzia Silaha nzito nzito Ethiopia ili amsaidie Kupambana vizuri na Waarabu ambao Kimsingi ndiyo Adui zake wake Wakubwa Kimaslahi.
 
AU badala ya kuwaunga mkono Ethiopia wamepiga kimya. Kenya wanakubaliana na maamuzi ya Ethiopia sijui Tanzania tuko upande upi.

Hata Mimi pia hii Vita naiona inakuja Mkuu ila Mfaidika Mkuu wa Maslahi ya hii Vita ni Waingereza na Wamarekani ambao wanazichochea hizi huku Mmoja akimpa Misri jeuri ya Kumkopesha Pesa zaidi ya Miradi yake na mwingine akimuuzia Silaha nzito nzito Ethiopia ili amsaidie Kupambana vizuri na Waarabu ambao Kimsingi ndiyo Adui zake wake Wakubwa Kimaslahi.
 
AU badala ya kuwaunga mkono Ethiopia wamepiga kimya. Kenya wanakubaliana na maamuzi ya Ethiopia sijui Tanzania tuko upande upi.
Tanzania bado tunahangaika Kwanza kujua Chanzo cha Moto wa Kimkakati na wa Kihujuma uliounguza Soko Kuu la Kariakoo jana Usiku na ambao ulizimwa Alfajiri ya Kuamkia leo ila Usiku huu umeanza tena Kuwaka kwa Kuunguza Mbilimbi, Pilipili na Hirizi pamoja na Vibuyu vya Wafanyabiashara humo ( mule )
 
Nchi IMEKWAMA siyo siri.

Tanzania bado tunahangaika Kwanza kujua Chanzo cha Moto wa Kimkakati na wa Kihujuma uliounguza Soko Kuu la Kariakoo jana Usiku na ambao ulizimwa Alfajiri ya Kuamkia leo ila Usiku huu umeanza tena Kuwaka kwa Kuunguza Mbilimbi, Pilipili na Hirizi pamoja na Vibuyu vya Wafanyabiashara humo ( mule )
 
Back
Top Bottom