Ni mimi tu huwa sipendezwi na chakula cha mgahawa na Hotelini?

Ni mimi tu huwa sipendezwi na chakula cha mgahawa na Hotelini?

Nikifa MkeWangu Asiolewe

JF-Expert Member
Joined
Feb 26, 2024
Posts
11,252
Reaction score
24,089
Wakuu sijawahi kula nikasema hiki chakula kitamu na kinazidi na chakula cha nyumbani.

Niseme ukweli chakula cha nyumbani kwetu hata kama kimepikwa na mama yangu mwenye umri wa miaka 74 bado huwa nakiona kitamu na kila ladha asili kuliko chakula chochote cha hotelini.

Nimeenda kwenye hoteli kubwa kadhaa wa kadhaa lakini bado msosi wake haujawahi kuupiku msosi wa nyumbani kwangu licha viungo wanavyotumia huko ni viungo vya kila aina nyumbani wanaweza kutumia kitunguu maji nyanya, carot, tangawizi na binzari pekee yake na chakula kikawa pambee!!

Nachojua na kufahamu hoteli zote kubwa au za kitalii wapishi mara nyingi huwa wamesomea mapishi na kukizi viwango vyote vinavyohitajika lakini badala chakula chao sio kitamu wala hakina ladha kama cha nyumbani.

Nimeuliza kwa watu kadhaa nao hudai hivyohivyo kuwa chakula cha nyumbani kina utamu wake na ladha yake!!

Huwa kinamapungufu gani hiki chakula ama ni mimi tu ndo sipendezwi nacho?
 
Inategemea na unakula wapi

Nenda Chef, Alcove,Moyo steak house n.k uniambie vyakula vyao siyo vizuri😅

Kwakweli sehem unayokula matters a lot.

Pia maranying huwez kuta chakula kizur sana hotelini. Pale chakula ni kama buffee (kama cha harusin au msibani ) na Lengo lao kubwa la kuuza Vyumba .

Ila ingia restaurant ambazo ni special kwa ajili ya chakula tu. Then uone utofauti.
 
Back
Top Bottom