Ni mbunge gani ktk mkoa wa Kagera atarudi 2015?

Nilikuwa Kitendaguro kwa wakwe zangu hivi karibuni na nikazunguka mji wa BK kwa siku 10 nilizokuwa pale!Kama niliyo yaona kwenye mji ule ndiyo Waziri Kagasheki anasifiwa kama kabadili mji basi wakwe zangu wana hali mbaya sana kimaisha!

BK hamna barabara nzuri,hamna maji ya uhakika,umeme kwa siku 10 nilizokaa pale ulikatika zaidi ya mara 11,BK hawana kiwanja kizuri cha ndege;meli zinazokuja BK toka Mwanza ni kuu kuu;BK nauli za ndege mlala hoi huwezi himili na huduma za matibabu nilijionea mwenyewe nilipompeleka mwanangu kwenye hospital ya mkoa ni kichekesho kabisa;shule za BK majengo yake ni hovyo kabisa na mengineyo mengi!

Wilaya ya Kyela ninapotoka iliyoko nje sana ya Mkoa wa Mbeya ni afadhali mara 100 kwa maendeleo kuliko jimbo la BK lililoko ndani ya makao makuu ya Mkoa Kagera!

asante sana shemeji yetu,umeandika ukweli,na kwa kawaida waafrika hatupendi kuambiwa ukweli pale inapofika ukosoaji!
 
Zimbiile vs Kalinjuma,teh, teh!, teh!,.....zama hizo jimbo la Muleba halijagawanywa na kuwa na Muleba kaskazini na kusini...Abaamba na Abanyaihangilo! Ubaguzi, ubaguzi, hadi lini jamani?hadi majimbo yametenganishwa kiubaguzi na sio kijiografia! Pumb@vu zenu!

Ahaaaaa Kamachumu Vs Iyangilo wahaya tupo nyuma sana kukweli.Jimbo la Muleba Kaskazini lipo tupu,Mh.Mwijage won't be back by 2015.Ansbert Ngurumo naskia unataka kugombea kupitia CDM am not sure kama unajulikana.
 
Deogratius Ntukamazina mbunge wa Ngara kumuondoa itakuwa kama kusukuma mlevi,jamaa hafanyi lolote na wananchi hawamkubali kabisa,nawahimiza tu viongozi wa CHADEMA wakaanze kuhamasisha tujichukulie jimbo...kwa sasa sipo nchini ila nimejaribu kuwafungua macho wale ninaoweza kuwafikia,jimbo letu lile
 
Mkoa wa Kagera umerudi nyuma kimaendeleo kutokana na hatua za makusudi za baba wa taifa ili heti ku-balance wiano wa maendeleo
 
Mkuu, huyu bishanga ni GAMBA lililokoma ambalo aliwezi ata kuvulika toka kwa joka zee bali kufa nalo. Mara zote ana aha na kulazimisha watu waende MMU ambapo anadhani watu watapotewa muda bila kujadili mambo ya kitaifa. Alafu ana vitisho.

Mimi ni mtu wa Muleba na nakiri kuwa kule majimbo yote ni kumsukuma mrevi! Kilichowabeba mbali na kuiba ni Prof. Ana alafu kampeni haikuwa na mashiko, kwakuwa tayari watu wanajua ni dhahiri CDM tuingie had mashinani maana magamba wamechukua majimbo na kufunga milango yetu kwenda mashinani
mmmmhhhh!
 
Mkoa wa Kagera umerudi nyuma kimaendeleo kutokana na hatua za makusudi za baba wa taifa ili heti ku-balance wiano wa maendeleo
maneno yako siyo kweli. tujilaumu sisi wenyewe. miaka zaidi ya 27 mwalimu ameondoka madarakani mbona hakuna lolote la maana limefanyika? hata mikoa chovu imetupita! ukitaka kujua tulivyo wazembe angalia idadi wa wabunge kutoka magamba,hakuna hata wilaya yenye mbunge wa upinzani ukiondoa wasubi wa Biharamulo!
 
kaka hasira kiasi hiki haiwezi kukudaidia kujifunza. kujifunza ni pamoja na kukubali changamoto. kwa kiasi hiki cha hisira me nadhan jamvi hili si mahali pako. humu tunachambua, tunashauri, tunapeana changamoto, tunaambizana ukweli hata kama ni mchungu kiadi gani, tuna-compromise, na kufanya hivi tunajifunza zaidi; tunaboreka kiuwezo , kiuchambuzi, kimtuzamo, na hatimaye tunakuwa marafiki. wakati mwingine urafiki wetu unatokana na kutofatiana kwetu. tofauti hizi na uwezo wetu kukabiliana nazo ndo unatutofautisha wengine. kwa hiyo calm down. persevere tutavuka pamoja. lengo ni moja ni kuifanya Tanzania iwe bora zaidi. VIVA LA DEFFERENCE(na zidumu tofauti zetu) . ALUTA CONTINUA

kweli usemalo pia huyu a cmment ambavyo ana uhakika ni ushauri mzuri sana kaka thanx
 
Charles Mwijage Ingawa yuko kwenye chama cha magamba lkn katimiza ahadi nyingi pamoja na jitihada zake dhidi ya wahamiaji haramu toka Rwanda

Charles mwijage ndio hafai hata kidogo zaidi ya majisifu na kupambana na madiwani wa upinzani katika halimashauri ya muleba. Kwa kipindi chote amekuwa nikujipendekeza kwa serikali ili afikiriwe japo unaibu waziri lkn wapi....! Kwa ufupi kagera wangependa kupata wabunge wa vyama vya upinzani 2015.
 
Ndo tatizo lingine la nshomile hakawii kutune external service service kushaua nakusahau kupeleka maendeleo na kusifia ,naishi Dar bwana wakati kimji cha bukoba kichovu huwezi amini ndipo nshomile wanatokea! Aaaaarg....... badillikeni!

Wewe mji wako ni hupi. Nshomile wengi hawajengi bukoba mjini ila hujenga kwao mgombani kama akina meku....!
 
maneno yako siyo kweli. tujilaumu sisi wenyewe. miaka zaidi ya 27 mwalimu ameondoka madarakani mbona hakuna lolote la maana limefanyika? hata mikoa chovu imetupita! ukitaka kujua tulivyo wazembe angalia idadi wa wabunge kutoka magamba,hakuna hata wilaya yenye mbunge wa upinzani ukiondoa wasubi wa Biharamulo!

I strongly support ur ideas. Lkn tunafanya nini ili kuhamasisha wanakagera kujiondoa ndani minyororo ya ccm. Nahitaji mchango ktk hili....
 
mwijage hakuna kitu, mama Tibaijuka anaweza kurudi anafanya mambo kisayansi, bukoba mjini kagasheki nono Nkenge sumputa no, bukoba vijijini no lakini ccm bado ina nafasi chadema tamaa kibao na majungu,
 
Back
Top Bottom