Ni makosa kuandika ''TUNAUZA MKAA''

Gang Chomba

JF-Expert Member
Feb 29, 2008
20,301
4,681
sehemu mbali mbali hapa Tanzania nimekuta
tangazo ''TUNAUZA MKAA''.

Unapoandika unauza MKAA inamaana unauza kipande kimoja.
Ila neno fasaha linalotakiwa kutumika hapo ni ''TUNAUZA MAKAA''.

Ukiwa mmoja unaitwa MKAA.
Na yakiwa mengi yanaitwa MAKAA.

Na ndio maana huwezi kukuta neno MKAA WA MAWE huku yakiwa mengi. bali utakuta neno MAKAA YA MAWE.

So ukikuta mahali pameandikwa hivyo basi mtafute
muhusika kisha mnase vibao. Akikupeleka polisi nitafute kisha watajuwa kama kuna wanasheria wa kuzaliwa na wanasheria wa kusomea...
 
Kwa sheria gani hasa inayokuruhusu kupiga vibao watu wanaokosea maandishi ya maneno ya kiswahili?
 
sehemu mbali mbali hapa Tanzania nimekuta
tangazo ''TUNAUZA MKAA''.

Unapoandika unauza MKAA inamaana unauza kipande kimoja.
Ila neno fasaha linalotakiwa kutumika hapo ni ''TUNAUZA MAKAA''.

Ukiwa mmoja unaitwa MKAA.
Na yakiwa mengi yanaitwa MAKAA.

Na ndio maana huwezi kukuta neno MKAA WA MAWE huku yakiwa mengi. bali utakuta neno MAKAA YA MAWE.

So ukikuta mahali pameandikwa hivyo basi mtafute
muhusika kisha mnase vibao. Akikupeleka polisi nitafute kisha watajuwa kama kuna wanasheria wa kuzaliwa na wanasheria wa kusomea...

Kwa hiyo basi itakuwa namna hii au sio....!?

Mkaa = Makaa (Mikaa?)
Jiwe = Mawe

Makaa ya mawe (Wingi)
Mkaa wa jiwe (Jiwe la mkaa? Mkaa wa mawe?)

Hapa ni confused dot com
 
Kwa hiyo basi itakuwa namna hii au sio....!?

Mkaa = Makaa (Mikaa?)
Jiwe = Mawe

Makaa ya mawe (Wingi)
Mkaa wa jiwe (Jiwe la mkaa? Mkaa wa mawe?)

Hapa ni confused dot com
Aiseee yaani wewe ndio umenivuruga kabisa, hata kile nilichokuwa nataka kuchangia kimetoweka! khaa..
 
Kwa hiyo basi itakuwa namna hii au sio....!?

Mkaa = Makaa (Mikaa?)
Jiwe = Mawe

Makaa ya mawe (Wingi)
Mkaa wa jiwe (Jiwe la mkaa? Mkaa wa mawe?)

Hapa ni confused dot com
Wala usichanganyikiwe na haya maneno mawili ambayo ni tofauti.
Mkaa = (charcoal) aina ya nishati inayotokana na miti au mimea uliyoungua nusu kwa kukoseshwa oxygen ya kutosha.
Makaa = (coal) ni aina ya nishati inayotokana na miamba ya mawe.

Mkaa -> unakata miti
Makaa ->unachimba ardhini kwenye miamba ya mawe na hivyo kupata jina "MAKAA YA MAWE"

Makaa si wingi wa neno mkaa, hizi ni bidhaa mbili zenye asili tofauti ingawa zote ni nishati.

Hatuwezi kusema eti wingi wa petroli ni dizeli.
 
Wala usichanganyikiwe na haya maneno mawili ambayo ni tofauti.
Mkaa = (charcoal) aina ya nishati inayotokana na miti au mimea uliyoungua nusu kwa kukoseshwa oxygen ya kutosha.
Makaa = (coal) ni aina ya nishati inayotokana na miamba ya mawe.

Mkaa -> unakata miti
Makaa ->unachimba ardhini kwenye miamba ya mawe na hivyo kupata jina "MAKAA YA MAWE"

Makaa si wingi wa neno mkaa, hizi ni bidhaa mbili zenye asili tofauti ingawa zote ni nishati.

Hatuwezi kusema eti wingi wa petroli ni dizeli.
oh hii imekaa vizuri. kwa hiyo wingi wa Mkaa ni Mikaa si ndio.. Thank you very much.
 
Wala usichanganyikiwe na haya maneno mawili ambayo ni tofauti.
Mkaa = (charcoal) aina ya nishati inayotokana na miti au mimea uliyoungua nusu kwa kukoseshwa oxygen ya kutosha.
Makaa = (coal) ni aina ya nishati inayotokana na miamba ya mawe.

Mkaa -> unakata miti
Makaa ->unachimba ardhini kwenye miamba ya mawe na hivyo kupata jina "MAKAA YA MAWE"

Makaa si wingi wa neno mkaa, hizi ni bidhaa mbili zenye asili tofauti ingawa zote ni nishati.

Hatuwezi kusema eti wingi wa petroli ni dizeli.

Ahsante sana.
 
Aiseee yaani wewe ndio umenivuruga kabisa, hata kile nilichokuwa nataka kuchangia kimetoweka! khaa..
Usiwe na wasi wasi, lengo ni kuonyesha kwa vitendo kuwa anachotaka kueleza sicho.

Wala usichanganyikiwe na haya maneno mawili ambayo ni tofauti.
Mkaa = (charcoal) aina ya nishati inayotokana na miti au mimea uliyoungua nusu kwa kukoseshwa oxygen ya kutosha.
Makaa = (coal) ni aina ya nishati inayotokana na miamba ya mawe.

Mkaa -> unakata miti
Makaa ->unachimba ardhini kwenye miamba ya mawe na hivyo kupata jina "MAKAA YA MAWE"

Makaa si wingi wa neno mkaa, hizi ni bidhaa mbili zenye asili tofauti ingawa zote ni nishati.

Hatuwezi kusema eti wingi wa petroli ni dizeli.
Mkuu, naelewa sana kuwa hizo ni bidhaa mbili tofaiti ila zenye kufanana kimatumizi, ila mleta mada ndio kajichanganya kidogo... Na atambue kuwa kuna vitu ambavyo havina wingi wala umoja.
 
Katika Kamusi ya Kiswahili Sanifu iliyotolewa na Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili, Dar es Salaam, imeandikwa hivi:
"Mkaa pia makaa nm vipande vya miti vilivyochomwa moto na kuzimwa kabla ya kuwa majivu."

Kwa maana hiyo, maneno yote mawili (mkaa na makaa) ni sahihi. Wingi wa mkaa ni ama mkaa au makaa. Yote yanakubalika.
 
Tofautisha kati ya mkaa utokanao na miti na mkaa wa mawe. Mkaa wa miti umoja na wingi unabaki "mkaa". Mkaa utokanao na mawe, wingi na umoja wake ni "makaa ya mawe".
 
nina hakika mtoa mada ameishi kenya ama anaangalia sana tv za huko.
Wakenya hawauzi mkaa, bali wanauza makaa.
 
wapendwa,

vyote "mkaa" na "makaa" ni sahihi kutumika na ni maneno yasiyokuwa na wingi wala umnoja, yaani kiwe kipande kimoja ama vipande kadhaa, huitwa mkaa/makaa. ni sawa na neno "maji", huwezi kusema umoja wa maji ni "mji" au "uji" na wingi wake ndio eti; "maji"! "mji" na "uji" ni maneno tofauti kabisa na yana maana tofauti sana na hayana uhusiano na "maji"

hivyo basi, yeye asemaye mkaa yuko sahihi na yule asemaye makaa pia yuko sahihi, iwe ni mkaa wa mawe ama makaa ya mawe, kauli zote ni sahihi

@ X-Paster, kifungu nomino "makaa ya mawe" ni jina moja la bidhgaa inayoitwa "coal" kwa kiingereza, huwezi kusema kuwa kipande kimoja ni mkaa/makaa ya jiwe na vikiwa vipande kadhaa ndio makaa ya mawe kiwe kipande kimoja au tani kadhaa za bidhaa hiyo, huitwa makaa ya mawe!

wakati mwingine huweza kutumika kifungu maneno "kaa la mawe" kumaanisha kipande kikubwa kuliko ukubwa wa kawaida wa mkaa/makaa ya mawe! halikadfhalika, siyo sahihi vilevile kusema "kaa la jiwe" ukimaanisha pande kubwa la mkaa/makaa ya mawe

mbarikiwe sana

Glory to God!
 
Miss Judith,habari za siku!!
Recently ninekuwa nikijiuliza huyu mpendwa yu wapi tena! Natumaini umekua vyema, na unazidi kubarikiwa.
Nilikukosa sana, ukutane na muujiza wako jumapili ya leo na zaidi Mungu akutane na haja ya moyo wako
 
Miss Judith,habari za siku!!
Recently ninekuwa nikijiuliza huyu mpendwa yu wapi tena! Natumaini umekua vyema, na unazidi kubarikiwa.
Nilikukosa sana, ukutane na muujiza wako jumapili ya leo na zaidi Mungu akutane na haja ya moyo wako

mpendwa King'asti,

mimi sijambo sana na nimekuwa nikizifurahia baraka za Mungu kila siku. nimekuwa na kazi nyingi sana siku za karibuni na pia nililazimika kusafiri kwa dharura majuma kadhaa yaliyopita, lakini Mungu ni mwema na kila kitu kwa sasa kinakwenda vizuri.

asante sana kwa kunim miss mpendwa na kwa dua. Mungu wetu wa rehema na neema asikuache siku hii njema ya leo na akifanye kila kiujazacho moyo wako kuwa kweli, amen.

he, tusijekuwa tunachakachua thread ya watu,

ubarikiwe sana mpendwa

Glory to God!
 
wapendwa,

vyote "mkaa" na "makaa" ni sahihi kutumika na ni maneno yasiyokuwa na wingi wala umnoja, yaani kiwe kipande kimoja ama vipande kadhaa, huitwa mkaa/makaa. ni sawa na neno "maji", huwezi kusema umoja wa maji ni "mji" au "uji" na wingi wake ndio eti; "maji"! "mji" na "uji" ni maneno tofauti kabisa na yana maana tofauti sana na hayana uhusiano na "maji"

hivyo basi, yeye asemaye mkaa yuko sahihi na yule asemaye makaa pia yuko sahihi, iwe ni mkaa wa mawe ama makaa ya mawe, kauli zote ni sahihi

@ X-Paster, kifungu nomino "makaa ya mawe" ni jina moja la bidhgaa inayoitwa "coal" kwa kiingereza, huwezi kusema kuwa kipande kimoja ni mkaa/makaa ya jiwe na vikiwa vipande kadhaa ndio makaa ya mawe kiwe kipande kimoja au tani kadhaa za bidhaa hiyo, huitwa makaa ya mawe!

wakati mwingine huweza kutumika kifungu maneno "kaa la mawe" kumaanisha kipande kikubwa kuliko ukubwa wa kawaida wa mkaa/makaa ya mawe! halikadfhalika, siyo sahihi vilevile kusema "kaa la jiwe" ukimaanisha pande kubwa la mkaa/makaa ya mawe

mbarikiwe sana

Glory to God!
Ngoja tuanze kufafanua vizur haya maneno.
Neno KAZI.
Likitumika kwa mtu itakua MKAZI.
Neno KAA hivyo mtu ataitwa MKAA.

neno TU ikiwa ni mtu ataitwa MTU.

Kwa kua kiwakilishi cha M huhusika kwa mtu.
Hata wewe chunguza utafaham tu!.
 
Back
Top Bottom