Acha nidandie treni kwa mbele.
Ukishaoa unaishi maisha yako kwa namna utayokubaliana na mwenzako huku mkochukua tahadhari ya jamii inayowazunguka namna wanavyoishi mnaweza jikuta nanyi mnaishi kama wao japo si sheria.
Kama baba yako yupo, muulize yeye alikuwa anapeleka pesa ukweni?
Kama una kaka wakubwa wailize pia. Kama una dada zako wameolewa muulize mama au baba, shemeji yako anawapa mshiko kila mwezi?
Kuna wanaopeleka matumizi (pesa na vitu) ukweni kila mwezi kwa ridhaa yao kama shukrani kwa kile mkewe anachomfanyia (Mahaba, utamu, mapishi, kujua kulea watoto na ndugu wa mume, anajua bajeti yaani sio mbahili sio mfujaji wa hela, sio mchoyo, hana gubu n.k.)
Hainaga fomula ukikuta unakerwaaa hata ukipigiwa simu na mkwe unajiskia kutukana

Nimeteremka kwenye treni nililodandia.
Alamsiki.