Ni lazima ceo awe na mba( masters of business administration degree)?

sikiolakufa

JF-Expert Member
Feb 1, 2010
411
54
Taswira mkazi wa kawaida wa Dar es Salaam anayoipata anaposikia fulani ni CEO wa kampuni au bank kubwa ni kwamba ni mtu Mtanashati, anayepanda gari la kifahari lenye hewa baridi wakati wote, mkononi amevaa saa iliyopakwa dhahabu simu yake(zake ni za hali ya juu...anaishi maeneo ya watu wa hadhi ya juu kwa ujumla ni mtu mwenye maisha ya raha...

Lakini hali halisi ni kwamba huyu ni mtu mwenye majukumu mengi sana na anabeba mzigo mkubwa sana kwenye kampuni au benki. kwa kifupi yeye ndiyo injini ya kampuni( decision maker) na maamuzi yake mara nyingi huathiri utendaji wa kampuni husika...
Ninavyofahamu mimi...CEO ndiye huandika ripoti ya mwaka ya kampuni ili awa convince shareholders katika mkutano mkuu wa mwaka
Huhusika na utendaji wa kila siku, kama kudraft barua, kusaini cheki, kutoa maelekezo ya nini kifanyike kwa wasaidizi wake, kuangalia mwenendo mzima wa kampuni, kumanage crisis n.k
kumanage mahusiano na makampuni mengine anayofanya nayo kazi

Ma CEO wengi huwa wamesomea degree ya pili ya MBA...hii degree ina mchanganyiko wa masomo mbalimbali yanayo mpa CEO uwezo na weledi wa ku oversee shughuli zote


JE NINI KAZI NYINGINE ZA CEO...DADA YANGU ANAFANYA KWENYE KAMPUNI MOJA YA MAFUTA...ANASEMA CEO WAO NI MFARANSA....NI CHECK BOB NA KAZINI KUWA ANAINGIA SAA TANO ASUBUHI....LAKINI HUWA ANAKAA MPAKA SAA TANO USIKU UFISINI...AKITOKA HAPO VIWANJA...KWENYE MACASINO...LAKINI UTENDAJI WAKE WA KAZI HAMNA MFANO...NASIKIA HUWA AKIINGIA OFISINI ANAKUTA VILE VI TRAY VYA INN NA OUT VIMEJAA NDANI YA SAA MOJA AMEKWISHA PITIA VYOTE NA KUTOA MAELEKEZO KWA WAHUSIKA...AMEAMURU WAFANYAKAZI WOTE WA LEVEL YA MANAGEMENT WAWE NA SIMU YA BLACKBERRY ILI AWEZE KUWASILIANA NAO KWA EMAIL MDA WOTE....JE WAKUU HII IMEKAAJE...UTENDAJI WA NAMNA HII UNGEFAA SANA KWA MASHIRIKA YA HAPA NYUMBANI?
WAZUNGU JEMBE DUH!
 
Back
Top Bottom