SALOK
JF-Expert Member
- Sep 20, 2011
- 3,308
- 1,924
Amini usiamini ndugu mtanzania haya yametokea leo tarehe 09 april 2012 ktk hospitali ya wilaya tandahimba, kuna ndugu yangu alimpeleka mwanae, kwa kudra zake manani alipata huduma, mwanae alipatiwa vipimo akagundulika na malaria akaandikiwa dawa 'mseto' alipoenda dirishani kuchukua dawa akaambiwa akanunue dukani, alipofika duka lilokaribu na hospitali akaambiwa amsubiri mwenye duka kaenda hospitali kuchukua dawa. Baada ya muda kidogo akatokea akiwa na box lenye dawa. Hizi ndio hospital zetu. Je tutafika?