Yoda
JF-Expert Member
- Jul 22, 2018
- 37,597
- 46,244
Wabongo tuache kujipumbaza kwamba sisi ni taifa special sana linalotazamwa na Mungu kipekee ndio maana tumekuwa na rasilimali nyingi, maziwa, mito, bahari, hali ya hewa nzuri n.k. Mataifa yote unayoyaona Afrika leo ni zao la mkutano wa Berlin wa mwaka 1884/1885 wakoloni wenye nguvu(mabeberu) walipojisevia ardhi zetu kama mlo wa mchana na sisi tukaendelea na urithi huo baada ya uhuru. Ni mataifa machache sana Kama Sudan ya kusini, Somalia na Ethiopia ambayo hayakupitia utaratibu huo.
Hutajapendelewa na Mungu kuwa na utulivu wa muda mrefu kupitia chama kimoja tawala tofauti na mataifa mengi ya Afrika. Chama tawala kimekuwa kuanzia TANU mpaka CCM ya sasa kimekuwa na weledi mkubwa sana katika kuyaleta makundi mbalimbali ya kijamii chini ya himaya yake kwa ushawishi wa kimaslahi zaidi kuliko kutumia dola ndio maana kipo imara madarakani kwa miongo yote hiyo, hakuna muujiza wa kiMungu katika hilo.
Wengine wanafika mbali katika kujifariji huku na kudai hata kuna mabadiliko makubwa yametokea ili Mungu kulisaidia taifa hili! Kama hilo ni kweli kwa nini mabadiliko hayo yasitokee huko kwingine dunia ambapo wanayahitaji zaidi kuliko sisi tena kwa miongo mingi?
Hutajapendelewa na Mungu kuwa na utulivu wa muda mrefu kupitia chama kimoja tawala tofauti na mataifa mengi ya Afrika. Chama tawala kimekuwa kuanzia TANU mpaka CCM ya sasa kimekuwa na weledi mkubwa sana katika kuyaleta makundi mbalimbali ya kijamii chini ya himaya yake kwa ushawishi wa kimaslahi zaidi kuliko kutumia dola ndio maana kipo imara madarakani kwa miongo yote hiyo, hakuna muujiza wa kiMungu katika hilo.
Wengine wanafika mbali katika kujifariji huku na kudai hata kuna mabadiliko makubwa yametokea ili Mungu kulisaidia taifa hili! Kama hilo ni kweli kwa nini mabadiliko hayo yasitokee huko kwingine dunia ambapo wanayahitaji zaidi kuliko sisi tena kwa miongo mingi?