Ni kweli Mh. Komba alitabiri kifo chake?

Ni kweli Mh. Komba alitabiri kifo chake?

Loading

JF-Expert Member
Joined
Feb 10, 2012
Posts
594
Reaction score
101
KOMBA.jpg

Aliyekuwa Mkurugenzi wa Kundi la Tanzania One Theatre ‘TOT’ na pia Mbunge wa Jimbo la Mbinga Magharibi (CCM), Hayati John Komba alitoa kali ya mwaka baada ya kuanika sifa za kaburi ambalo angependa azikwe siku akifa.

Akizungumza na Amani Mei 2, mwaka huu katika Makaburi ya Mwananyamala Kwakopa jijini Dar es Salaam kulikokuwa na mazishi ya msanii wa kundi lake, Fatma Ally ‘Fatuma Dogodogo’, Komba alisema hatafurahi endapo atazikwa kwenye kaburi lisilo na hadhi.

Alidai kuwa, anaamini kaburi lake likijengwa katika muonekano mzuri itakuwa rahisi hata kwa watu watakaokuwa wanakwenda kumuombea kuvutiwa kuliko kumfukia kikawaida.

“Siku nikifa naomba kaburi langu lijengwe kwa marumaru na juu liwekewe kioo cha ‘kuslaidi’ ili hata mtu akitaka kuja kufanya ibada ya kuniombea, awe anavuta tu kioo kisha anashuka ngazi hadi kwenye jeneza langu, sio kama hivi wanavyozikwa wengine,” alisema Komba.

Hivyo tunaimani wana familia watatekeleza matakwa haya.

Source GPL
 
Sasa hivi ibirisi anamgeuza geuza tu kwe moto wa milele,kabla hata hajajengewa hilo kabyri lake la kuslide
 
Kaburi mbwembwe tu, cha muhimu roho inapokwenda(kwa sisi tunaoamini)
 
Leo watu wanakimbizana na marehemu utadhani bado yupo hai
Ukinda FB wamo Twitter wamo IG wamo JF ndio kabisaaa kweli kapteni kumtusi mzee warioba sasa naamini imemkosti
 
Leo watu wanakimbizana na marehemu utadhani bado yupo hai
Ukinda FB wamo Twitter wamo IG wamo JF ndio kabisaaa kweli kapteni kumtusi mzee warioba sasa naamini imemkosti

Kwa hiyo mzee Warioba amemroga
 
Sasa MPOKI wa orijino komedi sijui atakuwa anamuiga nani, ".....eeeeh presha inapanda presha inashuka..."
 
Angefanya operesheni ya kupunguza unene angekuwa hai still
 
deni la crdb noma sana,wapi kaka yangu Kimei! pole sana mjane salome komba na lulu komba,RIP mbunge wangu Komba
 
Komba mwenyewe atakuwa kaachia hata familia madeni. Hivi alitegemea akifa kuna kuombewa.
 
mi~ccm inapo pungua watu wanafarijika kweli,hata wewe ni mmoja wapo!au unakataa?Eeh Mungu tuondolee na hili gaba.choli
 
Chama na Timu nzima ya Lumumba Buku 7FC watalishughulia hili...

MUSSA ALLAN ombi la Komba lifanyiwe kazi haraka ipasavyo
 
Last edited by a moderator:
Masikini hiyo video inasikitisha yaelekea alikwazwa mno na Warioba. Tulio wengi hudhani maombi baada kifo yana nafac kubwa kuliko maisha tuliyoishi . Sasa hilo ombi inabidi litekelezwe manake wosia wa marehemu una nguvu . R.I.P Komba
 
Back
Top Bottom