Mnaposema R.I.P(Rest In Peace),huwa mnamwambia nani haswa!,Mungu au marehemu!,acheni kuiga mambo yasiyokuwa na maana yoyote,wengi nimeona wanasema rest in peace!,haiwezi kubadili sehemu marehemu alipokwenda,kifo kimewekwa mara moja na ukishakufa unakwenda moja kwa moja hukumuni,unapoiambia maiti ipumzike kwa amani haisikii,haifahamu tena mambo ya duniani,muda tunapokuwa hai hapa duniani,ni wakati wa kutenda mema na kutengeneza maisha ya baadae baada ya kifo,sisi tulio wakristo tunaambiwa kwamba pasipo kuwa na utakatifu kamwe hatutaweza kumwona Mungu,sasa haya maneno ya R.I.P,mimi binafsi naona tu kuwa ni faraja za kujitaabisha wala hayawezi kubadili chochote,(mtu asipozaliwa mara ya pili,kwa maji na kwa roho hawezi kuurithi ufalme wa mbinguni),tutafute kwa bidii kuwa na amani na watu wote na huo utakatifu ambao hakuna atakayemwona Mungu asipokuwa nao.Kupumzika kwa amani(R.I.P) kwa Mkristo anatengeneza mwenyewe akiwa hai,akishakufa huwezi kumuombea tena.Mbarikiwe.