Ni kweli maagizo ya Waziri Mkuu hayatekelezwi au wanamuonea tu

saidoo25

JF-Expert Member
Jul 4, 2022
602
1,407
WIKI iliyopita Bunge lilichemka baada ya mvutano baina ya Jenister Mhagama na Spika wa Bunge kuhusu kauli ya Luhaga Mpina kwamba maagizo ya Waziri Mkuu kuhusu wafugaji hayajatekelezwa na wanaendelea kunyanyaswa kwenye nchi yao.

Je ni kweli maagizo ya Majaliwa hayatekelezwi? Kati ya Jenister Mhagama na Mpina nani yuko sahihi?

Tukumbushane maaagizo ya PM ambayo tunaamini hayajatekelezwa hadi sasa tangu yatolewe.

1. Wafugaji walioshinda kesi Mahakamani warejeshewe mifugo yao hii ilikuwa ni mwaka 2021

2. Maagizo kuhusu uchunguzi wa kuungua masoko utekelezaji wake ukoje?

Tuendelee wadau.
 
Raisi yupo fiti na anachapa kazi ofisini. Hii ni siku chache kabla la tarehe 17/3.

kauli hii haikutekelezeka.
 
Back
Top Bottom