Ni kwanini wageni wanaotoka mikoa mingine kuhamia kwenye majiji huwa wanafanikiwa kuzidi wenyeji ?

Ni kwanini wageni wanaotoka mikoa mingine kuhamia kwenye majiji huwa wanafanikiwa kuzidi wenyeji ?

mkata uzi

JF-Expert Member
Joined
Aug 3, 2025
Posts
1,910
Reaction score
5,451
Hii ni hali inayoonekana kwa mfano wazi kwenye majiji mfano Dar es Salaam, ambapo wenyeji wengi, licha ya kuwa wamezaliwa na kukulia hapa, bado wanakutana na changamoto kubwa katika kufikia mafanikio.

Zaidi ya hayo, siku hizi hatuwezi kusema kuwa wenyeji wa Dar ni Wazaramo pekee kama ilivyokuwa zamani. Kwa sasa, jiji linajivunia wenyeji kutoka makabila mbalimbali, hasa wale waliozaliwa kuanzia miaka ya 70 na kuendelea.

Kwa upande mwingine, wageni wanaotoka mikoani, wameonyesha kasi kubwa ya mafanikio. Ingawa wameingia katika miji mipya, wanashangaza kwa namna wanavyoweza kuanzisha biashara, kujenga mali, na kuwa na ushawishi mkubwa ndani ya kipindi kifupi. Kwa mfano, mtu mmoja aliyehamia jiji, kwa muda wa miaka 10-15, anaweza kuwa ameanzisha biashara inayostawi, kujenga nyumba, kumiliki magari, na kuwa na mtaji wa kutosha.
 
Spirit ya kupambana ndio inakufanya utoke home kwenda kutafuta maisha mbali, so ukifika kule unakuwa na hasira za maendeleo. Wale uliowakuta wao hawana hasira, anakaa home, anakula home, akikosa mlo anawatu wa kumbeba, usafiri wa home nk,sio rahisi kuwa na hasira na uchu wa maendeleo.
 
Sasa mgeni anapajua kitambaa cheupe, sinza na tabata?? Kwa wanaokuja dsm
 
Mkuu, mbona ni akili ya kawaida tu.
Mtu anapata moyo wa kupambana akiwa mazingira mapya, kule anakuwa hana support hana back up, anaishi kwa nidhamu mno.

Mimi ni mzaliwa wa Dar, nimezaliwa na kusoma apo ila niliona Mafanikio yangu kwa Dar ni vigumu kutoboa, maana Nina utitiri wa ndugu wengi. So nashindwa kupambana na ukizingatia najulikana pia ni mazingira niliyokulia.

Kwaiyo nikaona nitoke niende mikoani uku, sasa uku kumenijenga kiakili maana hata nikipata pesa naithamini, natumia kwa adabu na mipango ni mingi naifanikisha kwa wakati.

Nimeweza hili sababu Sina wa kumlilia uku nilipo,hakuna ndugu wa kunisumbua au kunikatisha tamaa nikitaka kufanya jambo langu, ni mm na akili yangu na Mungu wangu. Ile hali ya kubweteka haipo sababu najiona ni mgeni uku.

Ni ngumu kutoboa sehemu uliyokulia, sababu akili inaamini upo home bado. So unaweza kuweka juhudi kwenye utafutaji ila zinaweza zisifikie vile inatakiwa.
 
Mkuu, mbona ni akili ya kawaida tu.
Mtu anapata moyo wa kupambana akiwa mazingira mapya, kule anakuwa hana support hana back up, anaishi kwa nidhamu mno.

Mimi ni mzaliwa wa Dar, nimezaliwa na kusoma apo ila niliona Mafanikio yangu kwa Dar ni vigumu kutoboa, maana Nina utitiri wa ndugu wengi. So nashindwa kupambana na ukizingatia najulikana pia ni mazingira niliyokulia.

Kwaiyo nikaona nitoke niende mikoani uku, sasa uku kumenijenga kiakili maana hata nikipata pesa naithamini, natumia kwa adabu na mipango ni mingi naifanikisha kwa wakati.

Nimeweza hili sababu Sina wa kumlilia uku nilipo,hakuna ndugu wa kunisumbua au kunikatisha tamaa nikitaka kufanya jambo langu, ni mm na akili yangu na Mungu wangu. Ile hali ya kubweteka haipo sababu najiona ni mgeni uku.

Ni ngumu kutoboa sehemu uliyokulia, sababu akili inaamini upo home bado. So unaweza kuweka juhudi kwenye utafutaji ila zinaweza zisifikie vile inatakiwa.
Hakika, naunga mkia hoja.
 
Back
Top Bottom