Ni kipi cha kukumbukwa ulichomfanyia Mpenzio 2011?

Kigarama

JF-Expert Member
Apr 23, 2007
2,492
1,230
Muda mfupi ujao tunakwenda kuimaliza siku yetu ya Kwanza ya Mwaka 2012. Lakini tukiangalia nyuma kwenye mahusiano yetu kuna mambo ambayo tumewafanyia wapenzi wetu ambayo ni ya kukumbukwa kwa mwaka 2011. Hata kama umeachwa na mpenzio na ukakubali kuachika hilo nalo ni jambo kubwa sana la kukumbukwa kwani ulimrahisishia mwenzio njia yake ya kuanza maisha mapya.

Ni jambo gani ambalo ukitazama nyuma mwaka 2011 unaliona ni la kukumbukwa hata kama jambo hilo liliacha jeraha kubwa moyoni mwako? Ni sehemu ya kufanya tathimini ya Mwaka jana na kutafakari yajayo kwenye mwaka huu.
 
Nilimnunulia nyumba masaki
nikamnunulia Vog
nimemkabidhi kampuni ndogo ya udafirishaji wa majini.

Ni hayo tu.
 
uwongo njoo utamu kolea
mimi nilijitahidi asijue nina kiasi gani bank
kanda mbili na vivalo kapata
 
Kwahiyo unataka kuniambia hamna mwanamke anaeweza kumpika mwanaume ambae ni "limbwata free" ???
Anyway Lizzy inawezekana, lakini lazima utakuwa umeoa mwanamke Baunsa siyo kama hawa wetu wanaoshindia na kulalia chips mayai!!
 
Anyway Lizzy inawezekana, lakini lazima utakuwa umeoa mwanamke Baunsa siyo kama hawa wetu wanaoshindia na kulalia chips mayai!!
Basi mi mmoja wao, wala ukiniona huwezi kuamini ila ndio hivyo natembeza kichapo kila inapohitajika.

Alafu hao wachips mayai kumbe hua mnawanunulia kwa makusudi ehhh?
 
Back
Top Bottom