Ni kama nchi imesimama, hakuna kinachoendelea

Ni kama nchi imesimama, hakuna kinachoendelea

Sasa hivi sehemu nyingi duniani mwezi kuanzia wa Saba mpaka 12 ni high season. Ni msimu wa biashara. Lakini ati sisi Tanzania ni msimu wa kukimbizana na wapinzani. Hakuna plani mpya yoyote.plani mpya labda ni ile ya kuwadanganya wananchi kuwa ongezeko la kodi za miamala ya simu ni la benki na siyo la wananchi wakati huku wewe wewe umewaambia bank ni VAT. Sasa sijui VAT maana yake nini! Inasikitisha sana
 
Kwenye nyekundu hapo imeharibu mtiririko mzima wa maelezo yako.

Ni kweli wananchi tusitegemee sana kitu cha kusaidiwa kutoka serikalini, lakini ni wajibu wa serikali kutoa huduma stahiki kwa wananchi wanaolipa kodi hasa katikakipindi kigumu cha kiuchumi.

Mkuu na mimi nimeandika "kodi stahiki". Ni nchi ya wapi utaishi bila kulipa kodi za kaisari ndugu yangu? Hizo huduma zitatoka wapi bila kulipa kodi? Kikubwa ni kuweka misingi (bunge?) kuiwajibisha serikali kuhakikisha kodi zetu zinakuwa na matumizi yanayoendana na vipaumbele vyetu kama wananchi/taifa.
 
Akili za kijinga? You have to know. Umasikini ni laana. Ndiyo maana akili za masikini Siku zote hutamani hata uje mwisho wa dunia watu wote wafe. %70 ya masikini ni wachawi. Na wewe Nina Imani ni mmoja wao.

😀😀😀😀😀😀😀😀😀 Mkuu umetishaa....!
 
miaka 50 tunasubiri viwanda halafu kwa ujasiri unasema eti subira yavuta heri hivi huoni hata aibu kweli
fikra kama hizi ndio zakuziondoa kwenye nchi hii hazina tija kwetu.
Miaka 50 ipi mkuu? Magufuli kaahidi viwanda ata mwaka haujaisha au ww unazungumzia utawala upi?
 
Sasa hivi sehemu nyingi duniani mwezi kuanzia wa Saba mpaka 12 ni high season. Ni msimu wa biashara. Lakini ati sisi Tanzania ni msimu wa kukimbizana na wapinzani. Hakuna plani mpya yoyote.plani mpya labda ni ile ya kuwadanganya wananchi kuwa ongezeko la kodi za miamala ya simu ni la benki na siyo la wananchi wakati huku wewe wewe umewaambia bank ni VAT. Sasa sijui VAT maana yake nini! Inasikitisha sana

Hivi kwa akili yako unaamini kabisa serikali ilikuwa haijui inachokifanya? wajinga ni mimi na wewe ambao tuliamini kwamba serikali haijui inachokifanya! Otherwise, ukishasema VAT kila mwenye akili anaelewa una maana gani. Sasa ukiamini uongo.....shida siyo serikali tena ni wewe uliyeamini hivo wakati unajua si kweli.
 
Ni kweli hiyo iringa
Usiandikie mate. Bei ya nyanya sasa hivi ktk masoko ya Dar ni 6000 kwa tenga. Tenga moja kulisafirisha kutoka Iringa. mpaka Dar ni 5000. Sasa ww unafikiri mkulima atakuwa ameuza sh ngapi shamba?. Nakuapia ni kilio kila kona ya nchi hii
 
ifike time muwe mnasoma kwa ajiri ya kuelimika mama ako kijijini anakula nyasi wewe umekalia upambe sidhani kama wazazi wako walikuleta duniani ili uwe mpambe wa wanaume badilika unaipa familia yako wakati mugumu kila wanapo kufukiria walijua wamezaa kumbe ndo ivyo tena wamezaa yahaya
Kwa hiyo wewe ndio unajiona "umekwenda shule", sio?
 
Hujaelewa ninachomaanisha, maana yangu ni hii sio kwamba awamu hii ndo hali iko hvo km mnavotaka kuaminisha watu
Yeye alivyo vaa jezi alikuwa ajui mchezo anaotaka kuucheza hii timu anayochezea c mpya mpya kwake amekaa nayo kwa zaidi ya miaka 30 alivyoomba kuiongoza alijua anaweza kuipeleka mahara pazuri mambo ya kusema hata fulani alikosea huu si muda wake mbona yeye wanaoenda kinyume na mipango yake analala nao mbele ifike hatua akubari kuelekezwa na sikujifanya Mungu mtu.
 
Binafsi nahisi ni kama Tanzania kwa sasa hivi tuna wakati mgumu kuliko kipindi chochote cha uhai wa nchi hii kilichopita.

Sasa hivi wataalamu wote wa nchi hii wanakwazwa na wanasiasa ambao 100% hawana utaalam wowote. Doctor msomi na mzoefu kazini anaweza kufukuzwa kazi na mkuu wa wilaya! Ambaye hata kusoma na kuandika hajui vizuri. Ni hatari sana.

Hatari kubwa zaidi ni viongozi kujaribu kuyatumia majeshi yetu kisiasa. Hii ni hatari kubwa kuliko wao wanavyofikiri. Kama hali itaendelea hivi, basi kuna Siku haya haya majeshi yetu na yenyewe yatatamani kutawala. Hakuna atakayeweza kuyazuia.

Nchi imekosa dira kabisa. Wananchi hawajui wafanye nini! Kwa mfano. Mwaka huu wakulima wamelima nyanya na mazao ya mboga mboga kwa wingi sana. Wengi walihamasika baada ya kiongozi wetu kuwaahidi kuwa ni Tanzania ya viwanda. Matokeo yake kila mkulima analia. Nyanya hazina bei na hakuna hata kiwanda kimoja cha kusindika nyanya. Zinaozea mashambani.

Wakulima wa nyanya ni kilio kila kona ya nchi hii. Sasa hivi tenga moja la nyanya ambalo lina wastani wa kilo 30 bei yake ni Tsh elfu tatu (3000) hakuna juhudi zozote za kuwaokoa hawa wakulima. Waziri anayehusika na viwanda hawezi kufanya lolote la dharura ili kuwaokoa hawa wakulima kwa sababu anaogopa bila sababu. Sasa kama hatuwezi kuhifadhi hata mazao yetu tunayolima, je ni viwanda gani tunafikiri tunaweza kumiliki?

Kila kiongozi mwenye taaluma anaogopa kufanya maamuzi kwasababu nyuma yake kuna anayemsimamia ambaye ni mwanasiasa asiye na taaluma yoyote. Yeye taaluma yake ni kutafuta sifa tu, madhara yake ni makubwa kuliko tunavyofikiri. Tusipobadilika mapema, tutakwama sana na tunastahili kukwama.
Siku nyingine mtajifunza kuchagua viongozi sio watawala acha muisome namba
 
Usiandikie mate. Bei ya nyanya sasa hivi ktk masoko ya Dar ni 6000 kwa tenga. Tenga moja kulisafirisha kutoka Iringa. mpaka Dar ni 5000. Sasa ww unafikiri mkulima atakuwa ameuza sh ngapi shamba?. Nakuapia ni kilio kila kona ya nchi hii
Haya, basi tuone hayo maelfu ya watanzania wakijitokeza kwa wingi kuunga mkono "ukuta".
 
Binafsi nahisi ni kama Tanzania kwa sasa hivi tuna wakati mgumu kuliko kipindi chochote cha uhai wa nchi hii kilichopita.

Sasa hivi wataalamu wote wa nchi hii wanakwazwa na wanasiasa ambao 100% hawana utaalam wowote. Doctor msomi na mzoefu kazini anaweza kufukuzwa kazi na mkuu wa wilaya! Ambaye hata kusoma na kuandika hajui vizuri. Ni hatari sana.

Hatari kubwa zaidi ni viongozi kujaribu kuyatumia majeshi yetu kisiasa. Hii ni hatari kubwa kuliko wao wanavyofikiri. Kama hali itaendelea hivi, basi kuna Siku haya haya majeshi yetu na yenyewe yatatamani kutawala. Hakuna atakayeweza kuyazuia.

Nchi imekosa dira kabisa. Wananchi hawajui wafanye nini! Kwa mfano. Mwaka huu wakulima wamelima nyanya na mazao ya mboga mboga kwa wingi sana. Wengi walihamasika baada ya kiongozi wetu kuwaahidi kuwa ni Tanzania ya viwanda. Matokeo yake kila mkulima analia. Nyanya hazina bei na hakuna hata kiwanda kimoja cha kusindika nyanya. Zinaozea mashambani.

Wakulima wa nyanya ni kilio kila kona ya nchi hii. Sasa hivi tenga moja la nyanya ambalo lina wastani wa kilo 30 bei yake ni Tsh elfu tatu (3000) hakuna juhudi zozote za kuwaokoa hawa wakulima. Waziri anayehusika na viwanda hawezi kufanya lolote la dharura ili kuwaokoa hawa wakulima kwa sababu anaogopa bila sababu. Sasa kama hatuwezi kuhifadhi hata mazao yetu tunayolima, je ni viwanda gani tunafikiri tunaweza kumiliki?

Kila kiongozi mwenye taaluma anaogopa kufanya maamuzi kwasababu nyuma yake kuna anayemsimamia ambaye ni mwanasiasa asiye na taaluma yoyote. Yeye taaluma yake ni kutafuta sifa tu, madhara yake ni makubwa kuliko tunavyofikiri. Tusipobadilika mapema, tutakwama sana na tunastahili kukwama.

Kuwa na viwanda lazima uwe na nguzo, halizungumzwi tu kwakuwa unazungumza na kutaka viwepo they are technical issues ambazo lazima zifanyiwe kazi na badae utangaze viwanda, nguzo ndi zitasimamisha viwanda na si ajabu vitakuja vyenyewe.
 
Mkuu nchi haijasimama. Watu wanachapa kazi na maisha yanasonga. Maisha hayajawahi kuwa rahisi. Ni kweli changamoto ni nyingi lakini Kikubwa...wewe pambana kwenye nafasi yako uliyonayo. Usaidie familia yako na wategemezi wako (ikiwa ni pamoja na kulipa kodi stahiki za jamhuri). Hayo mengine waachie wenyewe.

Tanzania ya viwanda haitaletwa na serikali. Ukiona nyanya zinaozea shambani..hebu fikiria ni namna gani unaweza kutumia fursa ya kuzisindika. ni wewe na mimi kuona fursa zilizopo na kuzitumia. Ukisubiri kwamba serikali ifanye hili au lile..utasubiri bila majibu.

Mimi nadhani wananchi wengi hatujui wajibu wa serikali. We expect too much from it. Yet the truth is our expectations are in most cases misplaced!

Lets stop complaining! Do something. Hata akitoka Magufuli atakuja mwingine na yeye atakuja na wimbo wake. Mwisho wa siku ni wewe unayeumia na kukosa ufumbuzi wa matatizo yako na jamii inayokuzunguka.
ukiacha ukabila kujengea hojautauona ukweli.Ngosha funguka macho.
 
Sema ni lini katika miaka ya karibuni tenga la nyanya limeuzwa kwa shilingi 300?
Tatizo lenu BAVICHA nyie mkiambiwa mnachukua kitu kama kilivyo na kukitete bila kujua kikoje.Hiyo nyanya msimu wa 2011/2012 iliuzwa elf2 (2000/=) kaa chini uliza ndugu zako wa Ilula vizuri ndo urudi tena hapa.
 
Ha ha ha, endelea kujipa moyo
watumie ndugu zako pesa wanunue pembejeo za kilimo msimu wa kilimo umefika kijana uko mjini unazungusha suluali unakitu kichwani kazi kuzunguka kwenye maofisi ya wanaume kumsifia mtu anaefanya vitu visivyo onekana kwa macho kuwa muwazi acha tabia ya kufurahia kuwa kibaraka unaipa familia yako mateso anza upya elimu si bure kwa hii miaka ambayo jamaa yako yuko madalakani utoke hata na cheti cha la 7 kizuri
 
miaka 50 tunasubiri viwanda halafu kwa ujasiri unasema eti subira yavuta heri hivi huoni hata aibu kweli
fikra kama hizi ndio zakuziondoa kwenye nchi hii hazina tija kwetu.
Ajabu ndugu yangu. Miaka 50 bado mazao ya wakulima yanaozea mashambani kwa kushindwa kuwawekea viwanda vya kusindika. Bado ati tunanunua tomato souse toka Kenya na India. Wakati nyanya za wakulima wetu zinaozea shambani!that is a shame. Wakulima wanalia kila kona ya hii nchi
 
Tenga 3,000? Bado ghali sana, wataisoma tu namba ili wapunguze ushabiki kipindi cha uchaguzi, watulize akili wajitambue ndipo wafanye maamuzi. Ahadi ya kiwanda sio kiwanda na wala kiwanda sio uyoga kiote na kukimbizana na nyanya.
 
Back
Top Bottom