Ni kama nchi imesimama, hakuna kinachoendelea

Ni kama nchi imesimama, hakuna kinachoendelea

Maendeleo hakuna, misuguano inazidi mpaka watu wanashangilia vivo vya walinzi wa Amani yao. Na kuonyesha kuwa hawa wanasiasa wa Leo hawatumii hekima badala ya hali hiyo kuiondoa kwa kurejesha upendo wanamwagia tena petrol kwa kusema tutawasaka ndani na nje. Hivi ukiwakamata ndio utakuwa umeondoa chuki kati ya polisi na raia? Badala ya kujenga daraja wao wanajenga ngome ya kuwatenganisha zaidi
Halafu nyie BAVICHA mnamatatizo sana sahizi mmekuja na kamsemo eti Chuki kati ya Raia na Polisi kwanini mnawasingizia wananchi semeni chuki kati ya Polisi na BAVICHA maana nyie mnawachukia sana Polisi kwasbb zenu za kutumwa na Mbowe. Wananchi wako busy na kazi zao wanatafuta riziki zao za kihalali nyie ndo magwiji wakuwasemea uongo.
 
Tunaelekea kubaya ... kwan maamuzi mengi yanafanywa na politician... lakin mchango wa wataalam haudhaminiw kabisa kwenye nchi hii... ndii maana kila kitu kinakuwa kigumu.
 
Binafsi nahisi ni kama Tanzania kwa sasa hivi tuna wakati mgumu kuliko kipindi chochote cha uhai wa nchi hii kilichopita.

Sasa hivi wataalamu wote wa nchi hii wanakwazwa na wanasiasa ambao 100% hawana utaalam wowote. Doctor msomi na mzoefu kazini anaweza kufukuzwa kazi na mkuu wa wilaya! Ambaye hata kusoma na kuandika hajui vizuri. Ni hatari sana.

Hatari kubwa zaidi ni viongozi kujaribu kuyatumia majeshi yetu kisiasa. Hii ni hatari kubwa kuliko wao wanavyofikiri. Kama hali itaendelea hivi, basi kuna Siku haya haya majeshi yetu na yenyewe yatatamani kutawala. Hakuna atakayeweza kuyazuia.

Nchi imekosa dira kabisa. Wananchi hawajui wafanye nini! Kwa mfano. Mwaka huu wakulima wamelima nyanya na mazao ya mboga mboga kwa wingi sana. Wengi walihamasika baada ya kiongozi wetu kuwaahidi kuwa ni Tanzania ya viwanda. Matokeo yake kila mkulima analia. Nyanya hazina bei na hakuna hata kiwanda kimoja cha kusindika nyanya. Zinaozea mashambani.

Wakulima wa nyanya ni kilio kila kona ya nchi hii. Sasa hivi tenga moja la nyanya ambalo lina wastani wa kilo 30 bei yake ni Tsh elfu tatu (3000) hakuna juhudi zozote za kuwaokoa hawa wakulima. Waziri anayehusika na viwanda hawezi kufanya lolote la dharura ili kuwaokoa hawa wakulima kwa sababu anaogopa bila sababu. Sasa kama hatuwezi kuhifadhi hata mazao yetu tunayolima, je ni viwanda gani tunafikiri tunaweza kumiliki?

Kila kiongozi mwenye taaluma anaogopa kufanya maamuzi kwasababu nyuma yake kuna anayemsimamia ambaye ni mwanasiasa asiye na taaluma yoyote. Yeye taaluma yake ni kutafuta sifa tu, madhara yake ni makubwa kuliko tunavyofikiri. Tusipobadilika mapema, tutakwama sana na tunastahili kukwama.
Tukikwama tutapata akili, maana kwa sasa wenye nguvu wanatumia ubabe kupinga nawazo mbadala.
 
Inauma sana, tena inakera sana. Juzi nimeona mkuu wa wilaya flani anamfukuza Afisa mifugo uku anafoka na kutajataja huu ni awamu ya tano siyo ya nne. Niliumia sana, sijui ndo njia ya kufanyia kazi matatizo ya wakulima na wafugaji?
Viongozi kila mmoja anaongea lake wananchi wanashindwa kujua wafate lipi, Juzi mwingine kawaambia wafyatue watoto wasijali Jana mwingine akawaambia yule wa mwanzo aliyesema wafyatue watoto alikuwa ati anatania! Hatari sana. Tumefika stage ambayo Mimi Kama mimi siwezi kuvumilia. Nahama
 
Halafu nyie BAVICHA mnamatatizo sana sahizi mmekuja na kamsemo eti Chuki kati ya Raia na Polisi kwanini mnawasingizia wananchi semeni chuki kati ya Polisi na BAVICHA maana nyie mnawachukia sana Polisi kwasbb zenu za kutumwa na Mbowe. Wananchi wako busy na kazi zao wanatafuta riziki zao za kihalali nyie ndo magwiji wakuwasemea uongo.
BAVICHA nao ni raia. Kwa sasa inawezekana wanaowindwa ni BAVICHA, lakini madhara yatakayotokea baadaye hayataangalia BAVICHA. Wale wajasiriamali wa matunda Mwanza, sina hakika kama wote walikuwa BAVICHA na BAWACHA. Huo ni mfano tu wa jinsi madaraka yasipotumiwa kwa hekima na busara yanaweza kuathiri kila mtu bila kuangalia mipaka ya itikadi, rangi wala dini. Sometimes tumieni ubongo wenu kufikiri...assuming it's there in the first place. (sorry)
 
Mkuu nchi haijasimama. Watu wanachapa kazi na maisha yanasonga. Maisha hayajawahi kuwa rahisi. Ni kweli changamoto ni nyingi lakini Kikubwa...wewe pambana kwenye nafasi yako uliyonayo. Usaidie familia yako na wategemezi wako (ikiwa ni pamoja na kulipa kodi stahiki za jamhuri). Hayo mengine waachie wenyewe.

Tanzania ya viwanda haitaletwa na serikali. Ukiona nyanya zinaozea shambani..hebu fikiria ni namna gani unaweza kutumia fursa ya kuzisindika. ni wewe na mimi kuona fursa zilizopo na kuzitumia. Ukisubiri kwamba serikali ifanye hili au lile..utasubiri bila majibu.

Mimi nadhani wananchi wengi hatujui wajibu wa serikali. We expect too much from it. Yet the truth is our expectations are in most cases misplaced!

Lets stop complaining! Do something. Hata akitoka Magufuli atakuja mwingine na yeye atakuja na wimbo wake. Mwisho wa siku ni wewe unayeumia na kukosa ufumbuzi wa matatizo yako na jamii inayokuzunguka.
Nachukia sana hilo neno Tanzania ya viwanda sio kuwa siitakii mema nchi yngu but naona ni msemo tu kama kilimo kwanza
 
Tunaelekea kubaya ... kwan maamuzi mengi yanafanywa na politician... lakin mchango wa wataalam haudhaminiw kabisa kwenye nchi hii... ndii maana kila kitu kinakuwa kigumu.
Mkuu, nakuambia hali ni tete. Hata mawaziri ni Kama hawapo. Kila mmoja anafanya kazi kwa hofu. Hii ni karne ya digital. Nashangaa bado tunaongozwa ki analogia. Tumeshindwa hata kununua viwanda vidogo vya kuhifadhi nyanya za wakulima wetu. It's a very shame
 
Halafu nyie BAVICHA mnamatatizo sana sahizi mmekuja na kamsemo eti Chuki kati ya Raia na Polisi kwanini mnawasingizia wananchi semeni chuki kati ya Polisi na BAVICHA maana nyie mnawachukia sana Polisi kwasbb zenu za kutumwa na Mbowe. Wananchi wako busy na kazi zao wanatafuta riziki zao za kihalali nyie ndo magwiji wakuwasemea uongo.
Shika adabu yako kijana, sio kila anayekosoa serikali ni BAVICHA. Nyie wenye akili ndogo ndio mnaharibu sana nchi hii kwa mawazo kama haya ya kipuuzi.
Kwa taarifa yako kijana maeneo ya vijijini mahusiano ya polisi na raia sio mazuri hata kidogo na hii inatokana na baadhi ya askari wetu kubambika watu kesi kama njia ya kujiongezea kipato. Ndio maana kuna kauli kuwa kuingia rumande ni bure na kutoka ni hela yako. Hayo ndio ya kuangaliwa ili kurudisha imani.
Lakini hayawezi kuwekwa sawa kama akili itakayotumika ni ya aina hii yako
 
Mkuu, nakuambia hali ni tete. Hata mawaziri ni Kama hawapo. Kila mmoja anafanya kazi kwa hofu. Hii ni karne ya digital. Nashangaa bado tunaongozwa ki analogia. Tumeshindwa hata kununua viwanda vidogo vya kuhifadhi nyanya za wakulima wetu. It's a very shame
Ni mbaya mtaalam yoyote kufanya kaz under hofu.. itampelekea ku perform chini ya kiwango . Na ndio madudu tunayo yaona nchini kwetu
 
Shika adabu yako kijana, sio kila anayekosoa serikali ni BAVICHA. Nyie wenye akili ndogo ndio mnaharibu sana nchi hii kwa mawazo kama haya ya kipuuzi.
Kwa taarifa yako kijana maeneo ya vijijini mahusiano ya polisi na raia sio mazuri hata kidogo na hii inatokana na baadhi ya askari wetu kubambika watu kesi kama njia ya kujiongezea kipato. Ndio maana kuna kauli kuwa kuingia rumande ni bure na kutoka ni hela yako. Hayo ndio ya kuangaliwa ili kurudisha imani.
Lakini hayawezi kuwekwa sawa kama akili itakayotumika ni ya aina hii yako
Ahsante mkuu, jaribu kumwelewesha.labda kuna Siku atakuja kuzinduka usingizini, lakini isikupe tabu. Coz imeandikwa, "rushwa ikizidi humwondolea mtu ufahamu " that means, kuna wengine humu jamii forums ukitizama michango Yao utagundua kuwa akili zao ni kama za wanyama. Jua tayari! Wasikupe shida.
 
kama nilivyosema miaka hii mitano itaisha kwa kusikia maneno na kuona mambo mengi ya ajabu kutoka kwa watu tuliokuwa tunawategemea
 
Shika adabu yako kijana, sio kila anayekosoa serikali ni BAVICHA. Nyie wenye akili ndogo ndio mnaharibu sana nchi hii kwa mawazo kama haya ya kipuuzi.
Kwa taarifa yako kijana maeneo ya vijijini mahusiano ya polisi na raia sio mazuri hata kidogo na hii inatokana na baadhi ya askari wetu kubambika watu kesi kama njia ya kujiongezea kipato. Ndio maana kuna kauli kuwa kuingia rumande ni bure na kutoka ni hela yako. Hayo ndio ya kuangaliwa ili kurudisha imani.
Lakini hayawezi kuwekwa sawa kama akili itakayotumika ni ya aina hii yako
Usipaniki nenda kwa hoja tushukuru Mungu kama wanabambikiwa kesi tu maana kule kwa Obama wanawashoot kabisa na kuwaua.Maendeleo ya haki hayaji siku moja ni process ata Ulaya hawajafikia asilimia mia ila kuaminisha kwamba katika utawala huu chuki ya polisi na raia ni kubwa ku nikupotosha uma na nyie BAVICHA mnatengeneza hiyo scenario isiyo na mashiko
 
pesa jasho la kuku imeadimika
Bado, itaadimika kama machozi ya samaki! Ikiwa viongozi ambao tayari wanatuongoza wataacha kufanya siasa na kujikita ktk kutenda kazi. Basi tutashuhudia hali mbaya zaidi kuwahi kutokea.
 
Usipaniki nenda kwa hoja tushukuru Mungu kama wanabambikiwa kesi tu maana kule kwa Obama wanawashoot kabisa na kuwaua.Maendeleo ya haki hayaji siku moja ni process ata Ulaya hawajafikia asilimia mia ila kuaminisha kwamba katika utawala huu chuki ya polisi na raia ni kubwa ku nikupotosha uma na nyie BAVICHA mnatengeneza hiyo scenario isiyo na mashiko
Yaani kubambika kesi kwa RAIA bado unasema mnashukuru Mungu kws hilo?
Huyo mungu wa hivyo labda ni wenu Ccm tuu!
 
Usipaniki nenda kwa hoja tushukuru Mungu kama wanabambikiwa kesi tu maana kule kwa Obama wanawashoot kabisa na kuwaua.Maendeleo ya haki hayaji siku moja ni process ata Ulaya hawajafikia asilimia mia ila kuaminisha kwamba katika utawala huu chuki ya polisi na raia ni kubwa ku nikupotosha uma na nyie BAVICHA mnatengeneza hiyo scenario isiyo na mashiko
Mkuu, Mimi sikushangai. Kwa sababu ni wengi sana tulikuwa nao humu Jf long time kitambo.walikuwa na akili mzuri sana. Michango Yao iliheshimika, lakini baada ya kujiingiza ktk rushwa, akili zao ziligeuka na kuwa Kama hayawani. Nani asiyemjua member mwenzetu Mwanakijiji. Je huyu wa Leo ndiye yule tuliyemjua?. Lazima kila mwenye akili timamu na. Aliyezoea kula kwa jasho lake atambue kuwa tunakoelekea siko!
 
Back
Top Bottom