Ni Jaji yupi ambaye hukumu zake unapenda sana kuzisoma?

ChamaDola

JF-Expert Member
Dec 23, 2016
3,432
2,804
Wakuu,
Ni Japi yupi ambaye hukumu zake unapenda sana kuzisoma?
Haijalishi,awe ni Jaji wa Mahakama Kuu ya Rufaa!
Mie binafsi nazikubali hukumu za Samata J,.!
Ana good command of English language na huwa sikosi lakujifunza kwake!
Na mwisho nazikubali za Jaji Lubuva pia!
Wewe je?
 
Wakuu,
Ni Japi yupi ambaye hukumu zake unapenda sana kuzisoma?
Haijalishi,awe ni Jaji wa Mahakama Kuu ya Rufaa!
Mie binafsi nazikubali hukumu za Samata J,.!
Ana good command of English language na huwa sikosi lakujifunza kwake!
Na mwisho nazikubali za Jaji Lubuva pia!
Wewe je?

Ni Kweli Samatta alikuwa akitoa hukumu nzuri sana na zenye kueleweka. Napenda sana hukumu zake.

Jaji mwingine ni marehemu Mwalusanya. Huyu alikuwa anatoa kesi hukumu yake kama anafundisha vile. Usipoelewa hukumu za huyu jamaa bora uachane ma mambo ya sheria. Hata Mahakama ya rufaa walikuwa wanapata tabu kupindua hukumu za huyu jamaa. alikuwa akisimamia haki, tena hata kama ni against serikali. Aliipiga chini serikali mara nyingi sana. So sad mahakama na serikali kwa ujumla wakamtupa mkono, hawakumpromote na alipostaafu hadi kufa alitelekezwa. Atabaki legend kwenye mahakama ya tanzania na hadi leo hakuna jaji aliyemfikia. RIP.
Kuna huyu jamaaa Rutakangwa. Hukumu zake zimesimama na ni very authoritative. reasoning yake utaipenda, hababaiki na anakuwa imara kwenye msimamo wake.

Mjamaa mwingine ni Massati bwana. anaandika long judgments na anaweka ma authority ya kufa mtu, ni researcher mzuri.

Mwingine ninaevutiwa na hukumu zake japo kwa mbali ni Nsekela, anajitahidi kuandika. Kalegeya pia anajitahidi.
 
Judge Mwalusanya (huyu hukumu zake ni kama unasoma Thesis na hadi leo hii hakuna aliyemfikia na kwa mfano ukiisoma kesi ya Mbushu juu ya hukumu ya kifo utafurahi alivyochambua)
Judge Lugakingira
Kidogo Na Judge Samatta
 
Back
Top Bottom