Ni hasara gani kubwa ulishawahi kuipata ikakurudisha nyuma?

Dah! Imenihuzunisha aisee, pole mkuu.

Kwaupande wangu nilipoteza 1mil kwenye biashara ya mbogamboga(brucol, cauliflower, letuce). Nilikuwa na mshkaj wangu aliyekuwa napiga nae hizi mishe za kufungasha hizo mboga halafu tunatuma Dar kwa mama mmoja ambae alikuwa anatupa oda yaan anawatumia idadi ya kg za hizo mboga mnakata mnafunga mnatuma halafu mnatumiwa hela akiupokea mzigo.
Nashukuru biashara ilianza vizuri sana nakumbuka nilianza na mtaji wa laki 4 hiyo pesa nilitoa mimi huyo jamaa yangu alikuwa anafanya kazi ya kutafuta mboga kwa wakulima na kufunga kwakuwa mimi ni Mwl. na kazi yenyewe ilikuwa inafanyika siku za kazi . Basi tukapiga kazi kama miez 2 nilikuwa napata faida kuanzia elfu 35 mpk 50 kwa wiki kwakweli niliona hii kitu inalipa sana basi nikajichanga nikaongeza mtaji ukafika mil 1.
Nakumbuka tukafunga mzigo usafirishwe kwenda mjini dah ilikuwa kipindi cha mvua barabara ya kutoka Soni kwenda Mombo ikazingua kuna kifusi na mawe makubwa yakashuka aisee njia zikawa hazipitiki gari zikalala pale siku 2 na mboga zinatakiwa zifike mjini usiku au mapema sana sokoni, mboga zilioza pale na ndio ukawa mwisho wangu kwenye biashara, aisee niliumia sana kwasababu hela yenyewe ya kuongezea mtaji nilikopa kama laki 4 tena kwa riba.

Sent using Jamii Forums mobile app
Vitu ksma hivyo ilibidi ukodi magari yenye friji yale
 
Sita sahau nilitapeliwa milion 19 na mtu alie jifanya ana tengeneza hela bandia kwa kukopi namba za hela zenyewe .
Yaani kwamba alisema ukimpa milion m0ja yeye anazitoa milioni 2 . Jamaa alinipiga story mpaka nikakolea Nilishutuka kama jamaa alikuwa ananitapeli tayari nishapigwa milion19 adi leo maisha hayapo sawa.
 
Ni wazi Katika harakati za maisha kuna pingamizi nyingi sana, kuna muda unapambana sana kutafuta kile unachokihitaji, unabahatika unakipata lakini kinapotea na kubakiza kama ambaye hajafanya chochote,

Yaweza iwe kwa kuibiwa, kutapeliwa, kudhulumiwa, kupoteza, kuharibika n.k n.k

Kwa kweli huwa inauma sana, tena sanaaa,
Sizungumzii kitu kikubwa, hapana nazungumzia kitu chochote ambacho ulikipambania kukipata lakini kikatoweka haraka/kirahisi.

Binafsi Wakati nipo chuo mwaka wa kwanza nilikua nahifadhi pesa yangu kwa kujibana sana, zaidi ya nusu ya hela yangu ya Boom(nilikua napata 100%) nilikua naitunza inisaidie nikishamaliza au popote nitakapo pata nafasi ya kuianzishia biashara,

Hela yangu yote ya kujikimu, field, special faculty na za vikazi kazi kipindi cha likizo nikawa nimefikisha 2.6M mpaka namaliza,

Wazo kubwa nililokuwa nalo baada ya kumaliza ni kufungua stationary Morogoro, kulikuwa na uhaba sana wa stationary, nikaona hii ni fursa na bahati nzuri nikapata eneo zuri kabisaa.

Basi ile nimehitimu tuu sikutaka kukaa kabisa nyumbani, nilienda tuu kuwasalimia wazee nikawaomba kuondoka baada ya week moja nikatafute maisha,

Kiukweli hawakukubali mwanzo, waliomba hata wakae na mimi kidogo maana kiukweli sijawahi kukaa nao kwa muda mrefu tangu nianze darasa la kwanza, ila baadae wakalazimika sababu ya kuwashawishi, sikuwaambia chochote kuhusu ile pesa na mpango mzima.

Nikiwa nimeandika mahitaji yangu yote, nikaenda mjini kwenye duka flani hivi pale mtaa wa uhuru, nikanunua kila kitu kihusianacho na stationary(niliuza simu yangu nikajazia na kwingne ile hela ikafika 3.0M) na baadhi ya accessories za simu nikafungasha mzigo wangu ile jioni nikaupeleka Kwenye haya malori ya Mizigo yanayoleta mizigo Dar na kurudi mikoani Usiku, mimi nikarudi zangu home.

Lengo mzigo usafiri ule usiku, kuna rafiki yangu aupokee asubuhi mimi niukute huko mchana, ile ndio ikawa kwa heri 3.0M yangu.

Kiufupi mpaka leo hii sijajua ule mzigo ulipotelea wapi, Dereva na konda wanadai waliufikisha kwa mpokeaji na akapokea, Mpokeaji(rafiki yangu) nikimuuliza anadai amesubiri ila hakupata mzigo.

Mpaka dakika za mwisho naongea na konda anasema mpokeaji huyu hapa ongea naye, nikaongea na Mshkaji kweli akasema anashushiwa mzigo, Baadae nampigia sasa yeye kwa simu yake akasema hajapokea mzigo wala hajaongea na mimi kupitia simu ile...

Hiyo ilikua asubuhi niko pale Ubungo na mimi ndio nataka nitoke,

Sitosahau ile siku....nilikaachini bila kujijuaa,
Maumivu yale sitokuja kuyasahau, nilikaa pale chini kama nusu saa hivi,

Mdada mmoja msafiri aliona ile hali yangu ndio akaja kunisaidia,

Yule dada Alichelewesha safari yake kwa kunisaidia kunivusha barabara na kuhakikisha mpaka napanda daladala akaniomba namba, akamwambia konda huyu anashukia sehemu flani ni mgeni hapajui, ndio akaondoka, sidhani kama ile siku ningepita salama pale mataa,

Network ilipotea kabisa, kufika kituoni ndio konda akanishtua "shuka dogo ndio hapa" pasipo kujua nimekulia hapo ila pamegeuka pageni kwangu, narudi nyumbani wanashangaa, kila wanachouliza nipo kimya, sio kama sitaki kujibu ila hata kinywa hakifunguki, macho yanaonesha kbsa nazuia machozi, walielewa ile hali, wakaniambia nenda kalale,

Nilianza kwa kuwaomba sana msamaha wazee, nikawaelezea kisa changu, nikawaonesha risiti za manunuzi na za kusafirishia mzigo, waliumia sana Mwishowe wakanipa support...

Hasara zipo nyingi, lakini je ni ipi ilikuumiza zaidi na kuona kama imekurudisha sana nyuma na ni ngumu kurudi kwenye Hali ya kawaida.

Sio lazima iwe pesa,
Yaweza kua ulipoteza mda kwa kitu flani, Nguvu, Matuaini/Mtarajio makubwa yakabuma n.k n.k
SHARE
Wengi wenu mmesimesha wachumba wakaoa wengine hasara hiyo au
 
Ni wazi Katika harakati za maisha kuna pingamizi nyingi sana, kuna muda unapambana sana kutafuta kile unachokihitaji, unabahatika unakipata lakini kinapotea na kubakiza kama ambaye hajafanya chochote,

Yaweza iwe kwa kuibiwa, kutapeliwa, kudhulumiwa, kupoteza, kuharibika n.k n.k

Kwa kweli huwa inauma sana, tena sanaaa,
Sizungumzii kitu kikubwa, hapana nazungumzia kitu chochote ambacho ulikipambania kukipata lakini kikatoweka haraka/kirahisi.

Binafsi Wakati nipo chuo mwaka wa kwanza nilikua nahifadhi pesa yangu kwa kujibana sana, zaidi ya nusu ya hela yangu ya Boom(nilikua napata 100%) nilikua naitunza inisaidie nikishamaliza au popote nitakapo pata nafasi ya kuianzishia biashara,

Hela yangu yote ya kujikimu, field, special faculty na za vikazi kazi kipindi cha likizo nikawa nimefikisha 2.6M mpaka namaliza,

Wazo kubwa nililokuwa nalo baada ya kumaliza ni kufungua stationary Morogoro, kulikuwa na uhaba sana wa stationary, nikaona hii ni fursa na bahati nzuri nikapata eneo zuri kabisaa.

Basi ile nimehitimu tuu sikutaka kukaa kabisa nyumbani, nilienda tuu kuwasalimia wazee nikawaomba kuondoka baada ya week moja nikatafute maisha,

Kiukweli hawakukubali mwanzo, waliomba hata wakae na mimi kidogo maana kiukweli sijawahi kukaa nao kwa muda mrefu tangu nianze darasa la kwanza, ila baadae wakalazimika sababu ya kuwashawishi, sikuwaambia chochote kuhusu ile pesa na mpango mzima.

Nikiwa nimeandika mahitaji yangu yote, nikaenda mjini kwenye duka flani hivi pale mtaa wa uhuru, nikanunua kila kitu kihusianacho na stationary(niliuza simu yangu nikajazia na kwingne ile hela ikafika 3.0M) na baadhi ya accessories za simu nikafungasha mzigo wangu ile jioni nikaupeleka Kwenye haya malori ya Mizigo yanayoleta mizigo Dar na kurudi mikoani Usiku, mimi nikarudi zangu home.

Lengo mzigo usafiri ule usiku, kuna rafiki yangu aupokee asubuhi mimi niukute huko mchana, ile ndio ikawa kwa heri 3.0M yangu.

Kiufupi mpaka leo hii sijajua ule mzigo ulipotelea wapi, Dereva na konda wanadai waliufikisha kwa mpokeaji na akapokea, Mpokeaji(rafiki yangu) nikimuuliza anadai amesubiri ila hakupata mzigo.

Mpaka dakika za mwisho naongea na konda anasema mpokeaji huyu hapa ongea naye, nikaongea na Mshkaji kweli akasema anashushiwa mzigo, Baadae nampigia sasa yeye kwa simu yake akasema hajapokea mzigo wala hajaongea na mimi kupitia simu ile...

Hiyo ilikua asubuhi niko pale Ubungo na mimi ndio nataka nitoke,

Sitosahau ile siku....nilikaachini bila kujijuaa,
Maumivu yale sitokuja kuyasahau, nilikaa pale chini kama nusu saa hivi,

Mdada mmoja msafiri aliona ile hali yangu ndio akaja kunisaidia,

Yule dada Alichelewesha safari yake kwa kunisaidia kunivusha barabara na kuhakikisha mpaka napanda daladala akaniomba namba, akamwambia konda huyu anashukia sehemu flani ni mgeni hapajui, ndio akaondoka, sidhani kama ile siku ningepita salama pale mataa,

Network ilipotea kabisa, kufika kituoni ndio konda akanishtua "shuka dogo ndio hapa" pasipo kujua nimekulia hapo ila pamegeuka pageni kwangu, narudi nyumbani wanashangaa, kila wanachouliza nipo kimya, sio kama sitaki kujibu ila hata kinywa hakifunguki, macho yanaonesha kbsa nazuia machozi, walielewa ile hali, wakaniambia nenda kalale,

Nilianza kwa kuwaomba sana msamaha wazee, nikawaelezea kisa changu, nikawaonesha risiti za manunuzi na za kusafirishia mzigo, waliumia sana Mwishowe wakanipa support...

Hasara zipo nyingi, lakini je ni ipi ilikuumiza zaidi na kuona kama imekurudisha sana nyuma na ni ngumu kurudi kwenye Hali ya kawaida.

Sio lazima iwe pesa,
Yaweza kua ulipoteza mda kwa kitu flani, Nguvu, Matuaini/Mtarajio makubwa yakabuma n.k n.k
SHARE
Pole
 
Kupata Mwanaume MVuta bangi..Hii ndo hasara kubwa niliyowai ipata...YAAANI KUNA watu ukikutana nao maishani UMEKWISHA...hapa nilipo Leo Ni matokeo ya yule kuwa na yule mtu....

Hasara ilioji
Duh.kuna watu wamefika mbali na bwana mvuta bhangi
 
Dah kaka umeniumiza kweli kwa huu Uzi ,Mimi niliingia chuo nikiwa na 1.5 mil kutoka nyumban,then nikawa na Mkopo 100% ,basi nikafanya biashara ya ukopeshaji kwa wanafunzi wenzangu kwa riba ya 28%,mpaka nqfika mwaka wa tatu ,ioa duh Corina na kitendo cha wanafunzi kukatwq hela ya kujikimu hakika kilinifulisi kila kitu ba sasa nimemaliza chuo sijui kama nitakuja kumiliki pesa kma kipindi kile
 
Pole Sana! Mm nililima pamba ekari 30, dada yangu pamoja na shemeji yangu tukakubaliana nitoe pesa wao wasimamie kilimo cha mpunga tukakodi ekari kumi,kilichotokea zile mbegu za pamba zenye manyoya hazikuota kabisa, tukarudia shamba zima pia zikagoma, ule mradi wa mpunga kla nikipiga cm dada ananiambia mambo mazuri so nikiambiwa tuma ela cjui ya kupandia, Kung'olea,yaani chochote kinachohhusu Shamba bas fasta natuma,kuna kpnd machale yakanicheza coz walikua wananiambia vitu vile vile ambavyo nimeshawatumia peas,so ikabidi nimtume rafiki yangu akaone mradi ulipofikia na unavyoendelea du! Jamaa wakampeleka ktk shamba la mtu mwingine jamaa ananipigia cm ananipongeza kwamba shamba limekubali na hata watu aliojaribu kuongea nao hapo wanasema hapo nimekosa sana basi gunia200_250 hapo nikajipa moyo kwamba ili nirudushishe hasara ya pamba mm sitauza mpunga nitakoboa niuze mchele ikikaribia christmass, kuanzia nilikua nikituma Sana ela na kla nikituma lazma niwatumie na za matumizi yao ili wasichukue zle za mradi.after six months kimbembe kikaanza nawauliza nipeni bajeti ya uvunaji ili niwatumie ela,mara naambiwa subiri mpunga haujakauka vizuri mara usiwe na wasiwasi shemeji yako anasimamia uvunaji usitume era, nimesubiri mwezi ukapita wananiambia tumeshavuna bado kupiga na kupepeta niwatumie ela muweke vibarua wanasema hapana, niliomba ruhusa kazini wakaniruhusu Kwa mbinde nikaenda bila kuwapa taarifa LA! nafika stendi naita boda ananiuliza wapi nikamtajia jina la Shem anipeleke kwake yule akaniambia huyo ndo bosi wake mwenye hiyo boda na aliznunua mbili zinapiga mzgo mm ckuwa na waswas balaa nilipofka wakashkwa na butwaa kuniona baada ya salamu tu nikataka wanioneshe magunia waliovuna yaani ilikua mvurugano mambo hayaeleweki na kumbuka hiki kilimo ni cha umwagiliaji hakuna kusingizia mvua, mwisho walinieleza tu ukweli kwamba pesa nilizokua nawatumia wao walifungulia miradi yao shem alinunua pkpk mbili sista akafungua mgahawa wa kisasa wakaniomba radhi na kuniahidi kunilipa kdogokdogo maza nae akanisihi nisiwe na hasira, mm sikuzungumza ktu niligeuka cku hyohyo nikarudi toka cku hyo mpaka leo ckumbuki kama nimewahi kuwapigia cm,mpaka leo cwezi jiingiza ktk mradi wa kilimo milele nilijibana mno kwa muda Ilse nifanye saving ya kutosha lakn mwsho wa cku nikaambulia patupu inauma nikikumbuka.
Pole sana mkuu!

Kisa chako sehemu ya pili kinakaribiana kufanana na cha kwangu.

Mimi nililima mpunga hivyo hivyo sehemu 2 tofauti, sehemu ya kwanza nilikuwa namtumia rafiki yangu hela aweke vibarua lakini mwisho wa siku sikuvuna hata kilo moja. Sehemu hii nililima hekari 4 na ilinigharimu kama 1M. Niliamua kumpotezea tu ila hadi leo hatuna mawasiliano naye.

Sehemu ya pili niliyolima walikuwa wanasimamia dada yangu na shemeji yangu. Huku nililima hekari 20 na ilinigharimu kama 4.6M kuanzia kukodi eneo hadi kipindi cha kuvuna. Na nilipokuwa natuma hela ya kulimia pia nilikuwa nawapa na hela ya matumizi yao nikiassume kuwa wasihangaike. Kumbe kwanza eneo walilokodi zilikuwa ni ekari 15 tu na hela ya kulimia niliyowapa hawakuweka vibarua wa kulima badala yake walikuwa wanabangaiza kutafuta watu wanaalika wanalima kama sehemu ya shamba la familia lao hivyo hela ya kulimia wakala na walilima kwa kuchelewa sana japokuwa hela niliituma kwa wakati. Kwenye kuhupalilia tena walipalilia sehemu ndogo tu sehemu nyingine hawakupalilia wakala hela na pia dawa ya kupulizia hawakununua walikula pesa. Ila cha ajabu ni kwamba walikuwa wananitumainisha sana kuwa mazao yako vizuri na nitatajirika mwaka huo nitakapokuja kuvuna but nilichoambulia sikuamini aisee.

Kutokana na kuwa busy na majukumu sikuweza kufika kipindi chote cha kulima. Sasa ilipofika kwenye kuvuna ikabidi nimwambie mdogo wangu aende maana ilikuwa ni likizo alikuwepo home. Alichoenda kukutana nacho aliishia kusema bro hapa umepigwa hakuna shamba la thamani ya pesa uliyoitumia.
Nikamwambia avune tu kiasi kilichopo na auze angalau apate tu hata nauli na hela ya kumhudumia mwenyewe akiwa anarudi shule. Alivuna akauza na kupata kiasi cha 700000.

Ila kuanzia hapo nimeshasema kuhusu shemeji na dada tutasaidiana kwa mambo mengine lakini sio kifedha tena hata wakiwa na shida kiasi gani otherwise labda iwe kwenye kuokoa uhai tu ndio tutasaidiana kifedha itakapolazimu vinginevyo walishajilipa tayari kwa kile walichokula.

Kwa hiyo nikawa nimepata hasara mbili kwa rafiki yangu na kwa sister.
 
Pole sana mkuu!

Kisa chako sehemu ya pili kinakaribiana kufanana na cha kwangu.

Mimi nililima mpunga hivyo hivyo sehemu 2 tofauti, sehemu ya kwanza nilikuwa namtumia rafiki yangu hela aweke vibarua lakini mwisho wa siku sikuvuna hata kilo moja. Sehemu hii nililima hekari 4 na ilinigharimu kama 1M. Niliamua kumpotezea tu ila hadi leo hatuna mawasiliano naye.

Sehemu ya pili niliyolima walikuwa wanasimamia dada yangu na shemeji yangu. Huku nililima hekari 20 na ilinigharimu kama 4.6M kuanzia kukodi eneo hadi kipindi cha kuvuna. Na nilipokuwa natuma hela ya kulimia pia nilikuwa nawapa na hela ya matumizi yao nikiassume kuwa wasihangaike. Kumbe kwanza eneo walilokodi zilikuwa ni ekari 15 tu na hela ya kulimia niliyowapa hawakuweka vibarua wa kulima badala yake walikuwa wanabangaiza kutafuta watu wanaalika wanalima kama sehemu ya shamba la familia lao hivyo hela ya kulimia wakala na walilima kwa kuchelewa sana japokuwa hela niliituma kwa wakati. Kwenye kuhupalilia tena walipalilia sehemu ndogo tu sehemu nyingine hawakupalilia wakala hela na pia dawa ya kupulizia hawakununua walikula pesa. Ila cha ajabu ni kwamba walikuwa wananitumainisha sana kuwa mazao yako vizuri na nitatajirika mwaka huo nitakapokuja kuvuna but nilichoambulia sikuamini aisee.

Kutokana na kuwa busy na majukumu sikuweza kufika kipindi chote cha kulima. Sasa ilipofika kwenye kuvuna ikabidi nimwambie mdogo wangu aende maana ilikuwa ni likizo alikuwepo home. Alichoenda kukutana nacho aliishia kusema bro hapa umepigwa hakuna shamba la thamani ya pesa uliyoitumia.
Nikamwambia avune tu kiasi kilichopo na auze angalau apate tu hata nauli na hela ya kumhudumia mwenyewe akiwa anarudi shule. Alivuna akauza na kupata kiasi cha 700000.

Ila kuanzia hapo nimeshasema kuhusu shemeji na dada tutasaidiana kwa mambo mengine lakini sio kifedha tena hata wakiwa na shida kiasi gani otherwise labda iwe kwenye kuokoa uhai tu ndio tutasaidiana kifedha itakapolazimu vinginevyo walishajilipa tayari kwa kile walichokula.

Kwa hiyo nikawa nimepata hasara mbili kwa rafiki yangu na kwa sister.
Pole mkuu ndugu siku hizi hawaeleweki
 
Sita sahau nilitapeliwa milion 19 na mtu alie jifanya ana tengeneza hela bandia kwa kukopi namba za hela zenyewe .
Yaani kwamba alisema ukimpa milion m0ja yeye anazitoa milioni 2 . Jamaa alinipiga story mpaka nikakolea Nilishutuka kama jamaa alikuwa ananitapeli tayari nishapigwa milion19 adi leo maisha hayapo sawa.
Duuh huyo alitumia dawa aiseee

Sent from my SM-G611K using JamiiForums mobile app
 
Sita sahau nilitapeliwa milion 19 na mtu alie jifanya ana tengeneza hela bandia kwa kukopi namba za hela zenyewe .
Yaani kwamba alisema ukimpa milion m0ja yeye anazitoa milioni 2 . Jamaa alinipiga story mpaka nikakolea Nilishutuka kama jamaa alikuwa ananitapeli tayari nishapigwa milion19 adi leo maisha hayapo sawa.

Aisee, huu wizi uliingia sana... tena jamaa waliokuwa wanafanya hizi mambo... walikuwa wanajifanya wakongo...
Watu wengi sana wameharibiwa maisha yao kutokana na huu utapelii... maana jamaa wakikuingia hawakupigi padogoo... yan ukija kupikicha macho hivi... 50M ishakatikaaa.
 
Back
Top Bottom