Fidel80
JF-Expert Member
- May 3, 2008
- 21,947
- 4,445
Inauma sana na kusikitisha tr.20 March 2008. Wanachuo wa chuo cha Ualimu Morogoro [MOTCO] maarufu kama Kigurunyembe walitaka kufanya mgomo wakigomea fedha za mafunzo ya vitendo {BTP} kuwa ni kiduchu serikali hutoa sh.15000/= kwa mwezi kwa mchanganuo huo kila siku mwanachuo analipwa sh.500/= haijalishi umepangiwa Dar es salaam au Mbeya au Iringa pesa ndo hiyo hiyo. Mkuu wa mkoa wa Morogoro Kalembo alienda kuokoa jahazi lakini swala la kulipwa 500 kwa siku alishindwa kulitatua zaidi ya ahadi hewa kibao.
Je hii ni haki?Kweli kwa hali hii unamjengea mazingira gani mwalimu mtarajiwa?Kwa vile ni mwalimu basi hana haki ya kupewa fedha za BTP?Serikali yetu imelifumbia macho kabisa swala hili kwani ni la muda mrefu na vyuo vyote nchini vinalipwa fedha hiyo.
Kwa mtindo huu tunasafari ndefu sana tusipo badilisha safu za kuongozi katika safu za juu basi tutaendelea kudumaa na nidhamu za woga.
Naomba msaada wadau wa elimu.Serikali inatenda haki hapo?
Huyu ni Mkuu wa Chuo cha Ualimu Morogoro bwana Ngonyani maarufu kama Mayombo.
Wanachuo wakiingiza viti kwenye ukumbi baada ya kuitishwa kikao cha dharura na mkuu wa Mkoa Said Kelembo.
Wanachuo wakiwa wamechoka na kukata tamaa na hii fani.
Je hii ni haki?Kweli kwa hali hii unamjengea mazingira gani mwalimu mtarajiwa?Kwa vile ni mwalimu basi hana haki ya kupewa fedha za BTP?Serikali yetu imelifumbia macho kabisa swala hili kwani ni la muda mrefu na vyuo vyote nchini vinalipwa fedha hiyo.
Kwa mtindo huu tunasafari ndefu sana tusipo badilisha safu za kuongozi katika safu za juu basi tutaendelea kudumaa na nidhamu za woga.
Naomba msaada wadau wa elimu.Serikali inatenda haki hapo?
Huyu ni Mkuu wa Chuo cha Ualimu Morogoro bwana Ngonyani maarufu kama Mayombo.
Wanachuo wakiingiza viti kwenye ukumbi baada ya kuitishwa kikao cha dharura na mkuu wa Mkoa Said Kelembo.
Wanachuo wakiwa wamechoka na kukata tamaa na hii fani.