Ni dhahiri CCM wamechanganyikiwa

Makirita Amani

JF-Expert Member
Jun 6, 2012
1,781
3,072
kwa hali ya mambo ilivyo ccm wamechanganywa sana na hili vugu vugu la mabadiliko. Kwa mambo ambayo viongozi wa ccm wanafanya inaonesha kabisa wamepanic na hawajui waanzie wapi.

Kwanza kabisa ni serikali kutoa majibu ya matatizo ya wananchi kwenye mkutano wa hadhara. Ccm imeandaa mkutano wa kutoa majibu ya matatizo ya ajira, uchumi, uchukuzi n.k. Je serikali inaendeshwa kwa kujibu wananchi kwenye mikutano ya hadhara?? Leo unawajibu waliopo dar es salaa, je waliopo namtumbo utaenda kuwajibu lini?? Na wa ujiji je??

Pili ni viongozi wa ccm kutumia kauli chafu kwa upinzani na wana ccm wanaokihama chama hicho. Tumeshuhudia nape akiwakashifu wanaokihama ccm kwamba ni vinyago mara oli chafu n.k. Wassira akipewa nafasi yeye ni kuponda chadema tu kwa nn ccm mnaweweseka hivi??

Mimi nawashauri acheni kuiga kila chadema wanachofanya, nyinyi ndio mmeshika dola, tekelezeni ilani, kuzeni uchumi na mmboreshe maisha ya watanzania hakika watawakumbuka kwenye sanduku la kura. Ila mkiendelea kuweweseka hivi kifo chenu kitakuwa rahisi mno.
 
Umeongea vizuri.
Kazi ya Chama kilichopo madarakani ni kuwaletea wananchi maendeleo na kutekeleza malengo/ilani waliyojiwekea.
CCM wanapopata fursa ya jukwaa inawapasa waseme wamefanya nini, na sio watafanya nini.
 
Nakubali mkuu umepatia sana na hii thread yako...mm binafsi namshangaa wassira anapoweweseka na Mbowe pamoja na Chadema nzima ana matatizo ya kiakili huyu mzee,namshauri asome alama za nyakati kizazi hiki si cha kifala tunataka maendeleo na sio watu wa kusinzia hovyo!!!
 
Mkuu nakuchagua kuwa propagandist wa jukwaa la siasa humu JF.

Umetoa point nzuri sana ila inabidi sisi wenyewe tujiulize; je, huu mkutano wa hadhara (CCM/Jangwani) ni wa kuikashifu Chadema au CCM (chama kilicho madarakani) kujisafisha na kutuambia sie wapiga kura ni nini wamefanya since 2010 na nini tutarajie kunako 2015.

Utashangaa wana strategists wao pale ambao wamesoma ukiondoa Nnape lakini hawajui how to seduce the general public ili tuwakubali. Kingine pia, unaweza kukuta sie wapiga kura ndio wajinga badala ya kutaka kauli ya ukweli kutoka CCM tuko tu pale Jangwani kushabikia na usije kukuta watu wengi pale wapo tu ili kujaza namba.

Watu badala ya kujiuliza hivi toka tumepata uhuru mpaka leo hii TANU/CCM imetuletea kitu gani cha kujivunia? Umasikini bado uko pale pale tena miaka hii ya JK ndiyo kiboko zaidi, watu kulala na njaa ni kitu cha kawaida. Na pengine hata hawa waliofurika hapa jangwani huenda hawajala siku nzima, wapo hapa kupiga kelele ili siku ipite wasubiri kesho. Kwa kweli inasikitisha!

CCM imepoteza malengo ya uongozi hapa Tanzania na haina budi kuzikwa kunako 2015.
 
Huwezi ukawa unacheza ligi ya mabingwa halafu, unafanaya mazoezi kwa kuangalia timu za daraja la nne...
 
Hawa nyinyiem badala ya kuelezea utekelezaji wa ilani yao uko katika hali au hatua gani wao wanapanda majukwaani kutoa mipasho kwa cdm, hawana lolote la maana ila ni mipasho na hoja zilizokosa staha, inaonesha dhahiri kuwa cdm inawaumiza sana kichwa kwa kuwa viko vyama vingine vingi vya upinzani ila hawavinangi kwao upinzani ni cdm tuuu, na hii ndo dalili ya wazi kuwa cdm inawachachafya na kuwapelekesha wakianzisha jambo cdm basi na ccm haoo nyuma yao kuiga loo! kweli ccm imeishiwa vina, wamepagawa, wanachamba kabla ya kwenda haja kubwa!
 
Umeongea vizuri.
Kazi ya Chama kilichopo madarakani ni kuwaletea wananchi maendeleo na kutekeleza malengo/ilani waliyojiwekea.
Wanapopata fursa ya jukwaa inawapasa waseme wamefanya nini, na sio watafanya nini.

Hawa watakuwa wamejisahau wanadhani wako kwenye kampeni za kisiasa wamesahau wapo madarkani ndio maana wanaendeleza ahadi zao.
 
Watanzania ngumu sana kubadilika jamani. Tuwe makini tu CCM ndio itaondoka vinginevyo tutakuwa tunampigia mbuzi gitaa.
 
HAKUNA MAREFUYASIYO NA NCHA. MAGAMBAZ wakubali sasa kuwa enzi zao zimekwisha na wakaze mioyo na kuanza kujifunza kuishi kama wapinzani. kashfa nyingi hazitawasaidia. Inakuwaje umshawishi mtu uliyofanya, wakati sisi ndio walewale tunaoishi huko mtaani na hatuoni jipya lolote?
 
CCM ya zamani wamefanya mambo mengi sana ...ccm ya sasa ndo tatizo kinachowaumiza sasa hivi ni usaliti waliofanya kwa watanzania maana wamechafuka hata wakioga hawatakati tena ...mi nawashauri wakae pembeni hata miaka 10 tu wajisugue wakitakasika wataingia tena
 
Mheshimiwa Makirita -big up kwa saaaana.
Naungana na wote wliochangia hapo juu kwa ziada tu kuwa kuendelea kw awatanzania ni suala gumu kwani wanaotakiwa kuchagiza maendeleo kutoka kwa viongozi wao ndio wanaoshabikia hata lisilofaa madamu tu anakpenda chama husika, tujifunze kuangalia utaifa kwanza kabla ya maslahi ya vyama vyetu.
Tukifanya hivyo tutawachukia na kuwanyima nafasi wale wote ambao tunadhani hawajajipanga kutuhudumia kujikwamua na hali ngumu ya maisha. Tunahitaji kuwa wakali kwa walafi wote bila kujali anahusiana nasi vipi-kichama, kifamilia, kikabila, kikanda au kidini. Tuwaepuke kabisa. CCM (wanachama kueni sasa, siasa za kupigana vijembe kwa suala la maendeleo ya nchi tuachane nalo, tuwakemee na kuwazodoa pale wanapochemsha):clap2:
 
9.JPG


Mapepo?
 
Back
Top Bottom