Ni Corona ipi serikali ya Tanzania inapambana nayo? Wapi? Kwa kina nani?

G Sam

JF-Expert Member
Apr 20, 2013
11,555
35,880
Nimefanikiwa kusikiliza "audio clip" ya mtu anayedaiwa kuwa ni Gloria Michael ambaye bila shaka ni mtangazaji wa TBC. Katika hiyo sauti iliyorekodiwa inaonekana dada huyu anakiri wazi kuwa amejiridhisha kuwa ana kila dalili inayoonyesha anaugua COVID 19 na kwa sasa yanaendelea vyema.

Dada anaelezea kuwa alipitia zahanati kadhaa kabla hajalazimika kukimbilia taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete baada ya kuwa anahisi maumivu makali sana kwenye moyo na upande wa mgongoni achili mbali kikohozi kikavu. Anaelezea kuwa ni kweli pale Taasisi ya JK walimpima na kugundua kuwa mishipa ya karibu na moyo imetanuka kwa sababu blood pressure ilikuwa juu. Wakampa dawa akaruhusiwa.

Dawa ambazo yeye mwenyewe anaelezea kuwa hazikumsaidia kitu. Lakini vilevile hapo kabla anakiri kuwa alienda hospitali ndogo ambapo walipompima walimueleza kuwa ana maambukizi mengi kwenye damu bila kuambiwa hasa ni maambukizi ya aina gani.

Kwa maelezo ya dada yetu ni wazi kuwa kote huko hakuna aliyewaza kuhusu COVID kwani achilia mbali kumpima hakuna aliyeweza hata kuongelea jambo hili. Hata taasisi ya JK? Hawana kipimo?

Dada yetu anadai kuwa kilichomfanya akagutuka na kuanza kuwaza kuhusu Corona ni vifo vya wenzao wawili wa kazini na anasema kuwa baada ya kusikia habari ile ya vifo ndipo akagundua kuwa mmoja wa marehemu walifanya kazi kwa ukaribu sana kwa wiki nzima ikiwa ni kuchapisha nyaraka mbalimbali ikiwemo barua ya kupeleka Ubalozi wa Korea kuhusu swala zima la ARIDHIO.

Anasema alipata mshituko na presha kuzidi kuwa juu kutokana na habari hizi. Lakini baada ya hapo ndipo akaanza kuomba ushauri kwa wenzake (Anawataja) ni nini cha kufanya. Akaelekezwa atumie malimao, tangawizi mbichi pamoja na vingine ili kujinusuru. Anadai baada ya kufanya hivyo walau kwa sasa ana nafuu.

Audio hiyo aliitoa siku ya Jumapili ya Pasaka.

Anadai siku ya mwisho kuwa kazini walikuwa na kikao cha menejimenti, alikuwa akilalamikia ugonjwa ila kila mmoja kwenye kile kikao akaona ni jambo tu la kawaida.

Kilichonishtua ni kuwa anadai ameji "lockdown" yeye pamoja na familia yake. Yani serikali haijahusika na yeye pamoja na hii familia! Kweli?

Kiukweli jambo hili linaacha maswali mengi sana yasiyo na majibu.

1. Taasisi ya Jakaya Kikwete haina uwezo wa kupima COVID 19 mpaka mwezi huu wa nne? Au ni kutokuchukulia jambo hili kwa upekee?

2. Serikali inafanya nini kuhakikisha usalama wa jamii kama mgonjwa anadai kuwa ameamua kuji lock down yeye na familia yake? Nini hatima ya hili?

3. Inasubiri hadi lini kusambaza vifaa vya kupimia ugonjwa huu kwenye hospitali zake mbalimbali pamoja na incubators ili sampuli nyingi zipate majibu kwa haraka? Katika hili dada yetu aliambukiza watu wangapi huko alikopita?

Yapo madai mengi mitaani kuwa serikali inasubiri hadi mtu aumwe, ajipeleke mwenyewe hospitali ndipo waitwe kuja kumchukua wakampime ili kugundua kama ana maambukizi ya huu ugonjwa, madai haya yanathibitishwa pia na kisa cha kifo cha kwanza kutokea hapa nchini na sasa haya yaliyotokea TBC.

Hizo fedha za kutoka kwa wafadhili, zile za sherehe zilizoelekezwa huko na ambazo zinatengwa kwenye mfuko wa waziri mkuu wa kukabiliana na majanga kwenye kila bajeti ya mwaka zimefanya mini? Mbona hatuji na mikakati mipya ya kupambana na huu ugonjwa zaidi tu ya kusikia ipo tume imeundwa ambayo nayo haijawahi kujieleza ina au imekusudia kufanya nini la ziada kukabiliana na hili janga?

Chonde chonde Watanzania, narudia tena chonde chonde! Kwa hili tunacheza waziwazi!
 
Bila shaka serikali au wenye mamlaka wanawatumia wataalamu wetu kabla ya kutoa maelekezo yoyote kuhusu afya na usalama kwa ujumla.

Nadhani kuna kiwango kimewekwa tukifika hapo maamuzi magumu lazima yachukuliwe.

Ni sahihi au sivyo sijui. Hili ni janga angamizi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Akijitokeza ntu wa kujibu kwa kina hayo maswali nitapata mwanga.
Naomba uweke hiyo audio hapa.
 
Hakuna anaejali kwasababu haijawafika
Ikimfika moja tutapimwa majumbani mwetu
Safari za wilaya moja kwenda nyingine zitafutwa
 
Mi nashangaa huu udouble standard wa nini?bar zipo wazi,Ibada zinaendelea mfano mazishi ya askofu wa KKKT lakini shule zimefungwa case zinaongezeka.
 
..malimao na tangawizi mbichi na vingine.

weka hiyo audio clip ama link
 
Nimefanikiwa kusikiliza "audio clip" ya mtu anayedaiwa kuwa ni Gloria Michael ambaye bila shaka ni mtangazaji wa TBC. Katika hiyo sauti iliyorekodiwa inaonekana dada huyu anakiri wazi kuwa amejiridhisha kuwa ana kila dalili inayoonyesha anaugua COVID 19 na kwa sasa yanaendelea vyema.

Dada anaelezea kuwa alipitia zahanati kadhaa kabla hajalazimika kukimbilia taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete baada ya kuwa anahisi maumivu makali sana kwenye moyo na upande wa mgongoni achili mbali kikohozi kikavu. Anaelezea kuwa ni kweli pale Taasisi ya JK walimpima na kugundua kuwa mishipa ya karibu na moyo imetanuka kwa sababu blood pressure ilikuwa juu. Wakampa dawa akaruhusiwa.

Dawa ambazo yeye mwenyewe anaelezea kuwa hazikumsaidia kitu. Lakini vilevile hapo kabla anakiri kuwa alienda hospitali ndogo ambapo walipompima walimueleza kuwa ana maambukizi mengi kwenye damu bila kuambiwa hasa ni maambukizi ya aina gani.

Kwa maelezo ya dada yetu ni wazi kuwa kote huko hakuna aliyewaza kuhusu COVID kwani achilia mbali kumpima hakuna aliyeweza hata kuongelea jambo hili. Hata taasisi ya JK? Hawana kipimo?

Dada yetu anadai kuwa kilichomfanya akagutuka na kuanza kuwaza kuhusu Corona ni vifo vya wenzao wawili wa kazini na anasema kuwa baada ya kusikia habari ile ya vifo ndipo akagundua kuwa mmoja wa marehemu walifanya kazi kwa ukaribu sana kwa wiki nzima ikiwa ni kuchapisha nyaraka mbalimbali ikiwemo barua ya kupeleka Ubalozi wa Korea kuhusu swala zima la ARIDHIO. Anasema alipata mshituko na presha kuzidi kuwa juu kutokana na habari hizi. Lakini baada ya hapo ndipo akaanza kuomba ushauri kwa wenzake (Anawataja) ni nini cha kufanya. Akaelekezwa atumie malimao, tangawizi mbichi pamoja na vingine ili kujinusuru. Anadai baada ya kufanya hivyo walau kwa sasa ana nafuu.

Audio hiyo aliitoa siku ya Jumapili ya Pasaka.

Anadai siku ya mwisho kuwa kazini walikuwa na kikao cha menejimenti, alikuwa akilalamikia ugonjwa ila kila mmoja kwenye kile kikao akaona ni jambo tu la kawaida.

Kilichonishtua ni kuwa anadai ameji "lockdown" yeye pamoja na familia yake. Yani serikali haijahusika na yeye pamoja na hii familia! Kweli?

Kiukweli jambo hili linaacha maswali mengi sana yasiyo na majibu.

1. Taasisi ya Jakaya Kikwete haina uwezo wa kupima COVID 19 mpaka mwezi huu wa nne? Au ni kutokuchukulia jambo hili kwa upekee?

2. Serikali inafanya nini kuhakikisha usalama wa jamii kama mgonjwa anadai kuwa ameamua kuji lock down yeye na familia yake? Nini hatima ya hili?

3. Inasubiri hadi lini kusambaza vifaa vya kupimia ugonjwa huu kwenye hospitali zake mbalimbali pamoja na incubators ili sampuli nyingi zipate majibu kwa haraka? Katika hili dada yetu aliambukiza watu wangapi huko alikopita?

Yapo madai mengi mitaani kuwa serikali inasubiri hadi mtu aumwe, ajipeleke mwenyewe hospitali ndipo waitwe kuja kumchukua wakampime ili kugundua kama ana maambukizi ya huu ugonjwa, madai haya yanathibitishwa pia na kisa cha kifo cha kwanza kutokea hapa nchini na sasa haya yaliyotokea TBC.

Hizo fedha za kutoka kwa wafadhili, zile za sherehe zilizoelekezwa huko na ambazo zinatengwa kwenye mfuko wa waziri mkuu wa kukabiliana na majanga kwenye kila bajeti ya mwaka zimefanya mini? Mbona hatuji na mikakati mipya ya kupambana na huu ugonjwa zaidi tu ya kusikia ipo tume imeundwa ambayo nayo haijawahi kujieleza ina au imekusudia kufanya nini la ziada kukabiliana na hili janga?

Chonde chonde Watanzania, narudia tena chonde chonde! Kwa hili tunacheza waziwazi!
Mh, mkiambiwa unaleta ubishi na mkikamatwa mnatukana mamlaka. Weka hiyo audio ya Gloria Michael ulinganishe na video hii, ndio uendeleze mjadala wako
 
Nimefanikiwa kusikiliza "audio clip" ya mtu anayedaiwa kuwa ni Gloria Michael ambaye bila shaka ni mtangazaji wa TBC. Katika hiyo sauti iliyorekodiwa inaonekana dada huyu anakiri wazi kuwa amejiridhisha kuwa ana kila dalili inayoonyesha anaugua COVID 19 na kwa sasa yanaendelea vyema.

Dada anaelezea kuwa alipitia zahanati kadhaa kabla hajalazimika kukimbilia taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete baada ya kuwa anahisi maumivu makali sana kwenye moyo na upande wa mgongoni achili mbali kikohozi kikavu. Anaelezea kuwa ni kweli pale Taasisi ya JK walimpima na kugundua kuwa mishipa ya karibu na moyo imetanuka kwa sababu blood pressure ilikuwa juu. Wakampa dawa akaruhusiwa.

Dawa ambazo yeye mwenyewe anaelezea kuwa hazikumsaidia kitu. Lakini vilevile hapo kabla anakiri kuwa alienda hospitali ndogo ambapo walipompima walimueleza kuwa ana maambukizi mengi kwenye damu bila kuambiwa hasa ni maambukizi ya aina gani.

Kwa maelezo ya dada yetu ni wazi kuwa kote huko hakuna aliyewaza kuhusu COVID kwani achilia mbali kumpima hakuna aliyeweza hata kuongelea jambo hili. Hata taasisi ya JK? Hawana kipimo?

Dada yetu anadai kuwa kilichomfanya akagutuka na kuanza kuwaza kuhusu Corona ni vifo vya wenzao wawili wa kazini na anasema kuwa baada ya kusikia habari ile ya vifo ndipo akagundua kuwa mmoja wa marehemu walifanya kazi kwa ukaribu sana kwa wiki nzima ikiwa ni kuchapisha nyaraka mbalimbali ikiwemo barua ya kupeleka Ubalozi wa Korea kuhusu swala zima la ARIDHIO.

Anasema alipata mshituko na presha kuzidi kuwa juu kutokana na habari hizi. Lakini baada ya hapo ndipo akaanza kuomba ushauri kwa wenzake (Anawataja) ni nini cha kufanya. Akaelekezwa atumie malimao, tangawizi mbichi pamoja na vingine ili kujinusuru. Anadai baada ya kufanya hivyo walau kwa sasa ana nafuu.

Audio hiyo aliitoa siku ya Jumapili ya Pasaka.

Anadai siku ya mwisho kuwa kazini walikuwa na kikao cha menejimenti, alikuwa akilalamikia ugonjwa ila kila mmoja kwenye kile kikao akaona ni jambo tu la kawaida.

Kilichonishtua ni kuwa anadai ameji "lockdown" yeye pamoja na familia yake. Yani serikali haijahusika na yeye pamoja na hii familia! Kweli?

Kiukweli jambo hili linaacha maswali mengi sana yasiyo na majibu.

1. Taasisi ya Jakaya Kikwete haina uwezo wa kupima COVID 19 mpaka mwezi huu wa nne? Au ni kutokuchukulia jambo hili kwa upekee?

2. Serikali inafanya nini kuhakikisha usalama wa jamii kama mgonjwa anadai kuwa ameamua kuji lock down yeye na familia yake? Nini hatima ya hili?

3. Inasubiri hadi lini kusambaza vifaa vya kupimia ugonjwa huu kwenye hospitali zake mbalimbali pamoja na incubators ili sampuli nyingi zipate majibu kwa haraka? Katika hili dada yetu aliambukiza watu wangapi huko alikopita?

Yapo madai mengi mitaani kuwa serikali inasubiri hadi mtu aumwe, ajipeleke mwenyewe hospitali ndipo waitwe kuja kumchukua wakampime ili kugundua kama ana maambukizi ya huu ugonjwa, madai haya yanathibitishwa pia na kisa cha kifo cha kwanza kutokea hapa nchini na sasa haya yaliyotokea TBC.

Hizo fedha za kutoka kwa wafadhili, zile za sherehe zilizoelekezwa huko na ambazo zinatengwa kwenye mfuko wa waziri mkuu wa kukabiliana na majanga kwenye kila bajeti ya mwaka zimefanya mini? Mbona hatuji na mikakati mipya ya kupambana na huu ugonjwa zaidi tu ya kusikia ipo tume imeundwa ambayo nayo haijawahi kujieleza ina au imekusudia kufanya nini la ziada kukabiliana na hili janga?

Chonde chonde Watanzania, narudia tena chonde chonde! Kwa hili tunacheza waziwazi!
Very sad indeed. Tunajenga stigila na fulaiova na upuuzi mwingine
 
Mh, mkiambiwa unaleta ubishi na mkikamatwa mnatukana mamlaka. Weka hiyo audio ya Gloria Michael ulinganishe na video hii, ndio uendeleze mjadala wako

Ukweli hauwezi kupatikana maana na Gloria hawezi kusema ukweli! Mktoka madarakani ukweli wa kila kitu utajulikana
 
Mh, mkiambiwa unaleta ubishi na mkikamatwa mnatukana mamlaka. Weka hiyo audio ya Gloria Michael ulinganishe na video hii, ndio uendeleze mjadala wako

Hiyo video ni fake! Mkome kurahisisha mambo kwa kutumia ujinga!
 
Hata Mimi huku ni maumivu ya kifua kinauma nikaenda kupima nikakuta gastritis na dalili zote za hyo type of ulcers na natumia dawa pia natumia tangawizi na malimao tuondoe hofu jmn tule diet ya vitamini C


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimefanikiwa kusikiliza "audio clip" ya mtu anayedaiwa kuwa ni Gloria Michael ambaye bila shaka ni mtangazaji wa TBC. Katika hiyo sauti iliyorekodiwa inaonekana dada huyu anakiri wazi kuwa amejiridhisha kuwa ana kila dalili inayoonyesha anaugua COVID 19 na kwa sasa yanaendelea vyema.

Dada anaelezea kuwa alipitia zahanati kadhaa kabla hajalazimika kukimbilia taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete baada ya kuwa anahisi maumivu makali sana kwenye moyo na upande wa mgongoni achili mbali kikohozi kikavu. Anaelezea kuwa ni kweli pale Taasisi ya JK walimpima na kugundua kuwa mishipa ya karibu na moyo imetanuka kwa sababu blood pressure ilikuwa juu. Wakampa dawa akaruhusiwa.

Dawa ambazo yeye mwenyewe anaelezea kuwa hazikumsaidia kitu. Lakini vilevile hapo kabla anakiri kuwa alienda hospitali ndogo ambapo walipompima walimueleza kuwa ana maambukizi mengi kwenye damu bila kuambiwa hasa ni maambukizi ya aina gani.

Kwa maelezo ya dada yetu ni wazi kuwa kote huko hakuna aliyewaza kuhusu COVID kwani achilia mbali kumpima hakuna aliyeweza hata kuongelea jambo hili. Hata taasisi ya JK? Hawana kipimo?

Dada yetu anadai kuwa kilichomfanya akagutuka na kuanza kuwaza kuhusu Corona ni vifo vya wenzao wawili wa kazini na anasema kuwa baada ya kusikia habari ile ya vifo ndipo akagundua kuwa mmoja wa marehemu walifanya kazi kwa ukaribu sana kwa wiki nzima ikiwa ni kuchapisha nyaraka mbalimbali ikiwemo barua ya kupeleka Ubalozi wa Korea kuhusu swala zima la ARIDHIO. Anasema alipata mshituko na presha kuzidi kuwa juu kutokana na habari hizi. Lakini baada ya hapo ndipo akaanza kuomba ushauri kwa wenzake (Anawataja) ni nini cha kufanya. Akaelekezwa atumie malimao, tangawizi mbichi pamoja na vingine ili kujinusuru. Anadai baada ya kufanya hivyo walau kwa sasa ana nafuu.

Audio hiyo aliitoa siku ya Jumapili ya Pasaka.

Anadai siku ya mwisho kuwa kazini walikuwa na kikao cha menejimenti, alikuwa akilalamikia ugonjwa ila kila mmoja kwenye kile kikao akaona ni jambo tu la kawaida.

Kilichonishtua ni kuwa anadai ameji "lockdown" yeye pamoja na familia yake. Yani serikali haijahusika na yeye pamoja na hii familia! Kweli?

Kiukweli jambo hili linaacha maswali mengi sana yasiyo na majibu.

1. Taasisi ya Jakaya Kikwete haina uwezo wa kupima COVID 19 mpaka mwezi huu wa nne? Au ni kutokuchukulia jambo hili kwa upekee?

2. Serikali inafanya nini kuhakikisha usalama wa jamii kama mgonjwa anadai kuwa ameamua kuji lock down yeye na familia yake? Nini hatima ya hili?

3. Inasubiri hadi lini kusambaza vifaa vya kupimia ugonjwa huu kwenye hospitali zake mbalimbali pamoja na incubators ili sampuli nyingi zipate majibu kwa haraka? Katika hili dada yetu aliambukiza watu wangapi huko alikopita?

Yapo madai mengi mitaani kuwa serikali inasubiri hadi mtu aumwe, ajipeleke mwenyewe hospitali ndipo waitwe kuja kumchukua wakampime ili kugundua kama ana maambukizi ya huu ugonjwa, madai haya yanathibitishwa pia na kisa cha kifo cha kwanza kutokea hapa nchini na sasa haya yaliyotokea TBC.

Hizo fedha za kutoka kwa wafadhili, zile za sherehe zilizoelekezwa huko na ambazo zinatengwa kwenye mfuko wa waziri mkuu wa kukabiliana na majanga kwenye kila bajeti ya mwaka zimefanya mini? Mbona hatuji na mikakati mipya ya kupambana na huu ugonjwa zaidi tu ya kusikia ipo tume imeundwa ambayo nayo haijawahi kujieleza ina au imekusudia kufanya nini la ziada kukabiliana na hili janga?

Chonde chonde Watanzania, narudia tena chonde chonde! Kwa hili tunacheza waziwazi!

Nimesikiliza taarifa ya "Habari hivi punde" toka Radio 1/ITV kwamba Waziri wa Afya SMZ Dr. Hamad Rashid ametangaza kuongezeka kwa maambukizi ya Corona Zanzibar kwa watu 6( 5-Watz na 1-Mmisiri).
Kati ya hao 6 Kuna 2 WAMESHA FARIKI tayari mmoja tarehe 7/4 na mwingine sikumbuki....!!!
Hakika huu Ni UTANI wa kucheza na afya za Watz.....!!! Hii nji Tanzania(Bara na Zanzibar) chini ya CCM inatawaliwa na mazwazwa!!!
Kuna kitu hawa WATAWALA wanaficha kwa maksudi maalumu na malengo fulani. Haiwezekani MTU AMEUGUA CORONA mpaka amekufa Leo ndiyo unatoa taarifa...!! Je,Hawa walokufa walitangamana na watu wangapi na hivo wameambukiza wangapi?
Tukisema hata TAKWIMU ZA CORONA TANZANIA ZINATIA MASHAKA kuna Ukweli kwa 90%...!!
Kama TBC kuna watangazaji 2 wameathirika na 1 tayari keshafariki Serikali inangoja Nini kufunga TBC na staff wake wote kwenda Quarantine?
Kumbuka Hawa TBC Ni media na kila siku wanatafuta Habari mtaani na hata huko Bungeni wapo...!! Uwezekano wa TBC kuwa inatumika kusambaza Corona Ni mkubwa Sana...!!
Serikali itoe tamko iache upuuzi wa kulaghai watu....!!!
Serikali na Bunge wajue kuwa TBC Ni media ya Serikali na inatangamana na Viongozi na Raia katika kutafuta Habari hivo uwezekano wa kuambukiza wengine ni mkubwa....!!
 
Nimesikiliza taarifa ya "Habari hivi punde" toka Radio 1/ITV kwamba Waziri wa Afya SMZ Dr. Hamad Rashid ametangaza kuongezeka kwa maambukizi ya Corona Zanzibar kwa watu 6( 5-Watz na 1-Mmisiri).
Kati ya hao 6 Kuna 2 WAMESHA FARIKI tayari mmoja tarehe 7/4 na mwingine sikumbuki....!!!
Hakika huu Ni UTANI wa kucheza na afya za Watz.....!!! Hii nji Tanzania(Bara na Zanzibar) chini ya CCM inatawaliwa na mazwazwa!!!
Kuna kitu hawa WATAWALA wanaficha kwa maksudi maalumu na malengo fulani. Haiwezekani MTU AMEUGUA CORONA mpaka amekufa Leo ndiyo unatoa taarifa...!! Je,Hawa walokufa walitangamana na watu wangapi na hivo wameambukiza wangapi?
Tukisema hata TAKWIMU ZA CORONA TANZANIA ZINATIA MASHAKA kuna Ukweli kwa 90%...!!
Kama TBC kuna watangazaji 2 wameathirika na 1 tayari keshafariki Serikali inangoja Nini kufunga TBC na staff wake wote kwenda Quarantine?
Kumbuka Hawa TBC Ni media na kila siku wanatafuta Habari mtaani na hata huko Bungeni wapo...!! Uwezekano wa TBC kuwa inatumika kusambaza Corona Ni mkubwa Sana...!!
Serikali itoe tamko iache upuuzi wa kulaghai watu....!!!
Serikali na Bunge wajue kuwa TBC Ni media ya Serikali na inatangamana na Viongozi na Raia katika kutafuta Habari hivo uwezekano wa kuambukiza wengine ni mkubwa....!!
Wanaficha wakati kituo kizima wana Corona
 
Kama moyo ni dalili za Corona tumeisha Mana hata Mimi izi siku za karibun moyo ulikua unaniuma nikajua labda ni stress zangu tu na unene sababu nimeacha mazoezi

Sent using Jamii Forums mobile app
Mbavu zinavuta na hilo la moyo ni kutokana na pressure kupanda sana. Nashindwa tu ku upload hiyo audio huku.
 
Kuna kipindi nimeumwa kifua nakohoa huku mbavu zinauma nikaenda hospital wakapima lakin hamna kitu nadhani hawana kipimo Cha Corona mpka Sasa naishi kimungu MUNGU tu wazee twafaaaaaaaa
 
Kuna kiongozi mmoja alisikika akisema chadema kama corona.naona wanapambana na chadema kwanza alafu corona baadae.inaonekana chadema ina inawalaza bila ya shuka.
 
Kuna kiongozi mmoja alisikika akisema chadema kama corona.naona wanapambana na chadema kwanza alafu corona baadae.inaonekana chadema ina inawalaza bila ya shuka.
Huyo kiongozi sijui kapotelea wapi,nahisi na yeye atakuwa mgonjwa saa hizi.
 
Back
Top Bottom