Mzee Uchwara
Senior Member
- Oct 28, 2013
- 119
- 35
Ndungu zangu wanachama na wapenzi wa Chadema,kuna mgogoro mzito unaoendelea ndani ya chama cha Chadema. Ingawa viongozi wanakanusha, hii inatokana na CC kumvua madaraka yote Mh. Zito na wenzake. Ni lazima tukubali kuwa zito bado ana wafuasi wanaomuunga mkono ndani ya Chadema. Ili binadamu uendelee ni lazima ukubali kukabiliana na changamoto mbali mbali na Chadema ili kistawi vizuri ni lazima kipitie katika changamoto mbali mbali na pia kikubali mgongano wa mawazo. Ndugu zako ili Chadema iepuke huu mtego wa kusambaratika ni lazima busara itumike na si jazba wala kuoneshana ustadi wa kujibizana kwenye vyombo vya habari. Hali hii haijenga, zito kama kijana anae jijenga katika siasa ana mazuri na mabaya,kama tumeona ana mapungufu ni vema tukamwita na kumwambia mapungufu yake na hivyo hivyo kwa uongozi kama una mapungufu ni lazima ukubali kukosolea hii ndio DEMOKRASIA. Ili tutoke hapa salama ni vema suluhu ikapatikana kati ya zito na uongozi wa Chadema. Ebu tujikumbushe kuhusu sheria ya mabadiliko ya katiba uliopitishwa na wabunge wengi wa CCM lakini Raisi kikwete alitumia busara kwa kukaa meza moja na wapinzani na yakaisha. Na hivyo hivyo ndani ya Chadema suluhisho la mgogoro huu si kuwa fukuza kina zito bali ni kukaa meza moja ili Chadema iwe kitu kimoja, na sio maamuzi magumu kama tunavojidanganya. Naomba sana Mh. Mbowe na Dr.slaa mtafakari kwa makini sakata ili na mtumie busara kulimaliza na ubabe. Ni vema mkakaa na zito na wenzake katika meza moja na kutatua mgogoro huu. Kwani mkikaa pamoja mtakosoana na kupata suluhu. Wahenga wanasema vita ya panzi ni furaha ya kunguru. Ili kuwaziba mdomo CCM ni vema tukawa wamoja kwa kutafuta suluhu na kuendelea kukijenga Chama na kujiandaa na uchaguzi wa serikali za mitaa hapo mwakani. Mungu ibarike CHADEMA.