Ni application gani nzuri za kitanzania unazotumia?

Tanzania Tech

JF-Expert Member
Dec 8, 2016
355
276
Habari wana JF, Natumain wote humu mko salama kabisa. Leo tulikuwa tunatafuta app nzuri za kitanzania za kushiriki na wasomaji wetu wa tovuti ya Tanzania Tech, lakini kwa haraka haraka hatujafanikiwa kupata App nyingi kutokana na kuwepo kwa Apps nyingi sana kwenye soko la Play Store.

Sasa basi, tunaomba msaada wenu au kama wewe ni mmiliki wa App yoyote ya android ambayo unahisi inaleta mchango fulani wa maana kwa jamii basi unaweza kushare hapa na sisi tutashiriki app hizo kwenye tovuti yetu na App yetu ya Tanzania Tech.

  • Kifupi App yako inatakiwa iwe ina mchango wa maana kwenye jamii hasa ya Kitanzania na iwe inafanya kazi kikamilifu.
  • Kitu kingine unaweza kuweka maelezo kidogo Jinsi App hiyo inavyofanya kazi ikiwa pamoja na link yake kwenye soko la Play Store.
  • Kingine kama app yako haiko kwenye soko la Play Store basi unaweza kuweka link ya file la apk lakini hakikisha app yako ni salama na haina malware au virus.

Natumaini hii itasaidia pia hata kwa hapa JF, kwani wengi wetu tunatumia Apps zinazo tengenezwa na wabunifu kutoka nje ya Tanzania na tunasahau kuwa hata watanzania wanaweza.
 
Pia kuna ZOOM TANZANIA na JOBS IN TANZANIA(Ni nzuri kwa wanaotafuta kazi), AZAM TV(Online Tv streaming),MPESA(njia rahisi ya malipo vodacom),ELIMU SOLUTION ( inatoa fursa za masomo nje - scholarships),KUPATANA - ni nzuri kwa manunuzi ya kimtando.
IMG_20180601_164510.jpg
IMG_20180601_164432.jpg
 
Maelezo yote yako kwenye website. Soma download tumia
This is not about me, ni kwa ajili ya watu wote ambao wangependa kutumia app yako, as i can see app yako ina maelezo ya kiingereza. I don't think this will fit our criteria.
 
Pia kuna BRANCH na TALA(Ni app nzuri kwa wanaohitaji mikopo ya sh 10K - 1000K)
SEKRETARIETI YA AJIRA(ni mfumo/app ya serikali kwa ajili ya kuajiri wafanyakazi wa Umma - Maombi ni online,) me natumia hizi wakuu.
 
Back
Top Bottom