Ni aina ipi ya mashine za kufulia nguo inafaa

Ni aina ipi ya mashine za kufulia nguo inafaa

mfianchi

Platinum Member
Joined
Jul 1, 2009
Posts
12,168
Reaction score
8,937
Wadau najua hapa JF huwezi kukosa kitu,baada ya shemeji yenu kwenda masomoni na kazi ya kufua nguo imekuwa shuruba kwangu,sasa nataka kununua mashine ya kufulia nguo ambayo haizidi Tsh 500,000na si ya familia kubwa . je ninunue yenye sifa zipi sababu ni mbumbu wa hizo mashine,najua wengine watasema ni google,lakini kwenye google ni maelezo tu mi nahitaji kusikia kutoka kwa watumiaji,na je inahitaji vitu gani kuvifunga kwa mfano nikinunua ,ni sawa na vile ukinunua jiko la gesi lazima utahitaji mtungi,valve n.k,na je kitu kinachoitwa drum kina kazi gani ?ningependa pia kujua brands na models .Asent
 
Ukakosa mchangiaji kuonesha kwamba wanajf wengi hawana hivyo vitu kwao ni mashokoro mageni.
 
Za malawi ni nzuri zaidi na nyumba nyingi dar wanazitumia, kidogo na za iringa ila za dim ndg usijaribu zinakula umeme balaa na mzigo hazipigi kivile, kuhusu za mtu mweupe mi cjui
 
Chukua za mchina au housegirl au mashine za nni wakat wasiosoma wapoo wape kazi za kufua
 
Mjomba chukua Hotpoint manual ya kilo 10 (uzito inayohimili kwa mwosho mmoja)
Mie ninayo huu ni mwaka wa nne sasa tangu zama shemeji yako akiwa mjamzito.
Ulaji wake wa umeme ni almost invisible.
All the best
 
Mkuu, kwa ushauri wangu kabla ya kununua hii machine andaa chumba cha kufulia, kitakachokuwa na bomba la kuingiza maji na lingine la kutoa(moshi nimeunganisha bomba la kutoa na sewage system ya municipal so sijali sana kisima kujaa, hapa dar nimetumia ujanja fulani ivi, pili tafuta machine za west point, ni nzuri ninatumia kwa miaka sasa na hata moja niliyofunga moshi inaatumiwa na watoto wa hostel na bado inadunda
 
Nunua Hitachi. Mie nimetumia miaka mingi haijawahi kunisumbua. Halafu siyo bei ghali sana.
 
Mkuu, kwa ushauri wangu kabla ya kununua hii machine andaa chumba cha kufulia, kitakachokuwa na bomba la kuingiza maji na lingine la kutoa(moshi nimeunganisha bomba la kutoa na sewage system ya municipal so sijali sana kisima kujaa, hapa dar nimetumia ujanja fulani ivi, pili tafuta machine za west point, ni nzuri ninatumia kwa miaka sasa na hata moja niliyofunga moshi inaatumiwa na watoto wa hostel na bado inadunda
Mdau, je mashine yako inapausha nguo? Kwasababu nguo za kupeleka kufuliwa kwenye maduka ya dry cleaners huwa zinapauka ingawa pia wanatumia mashine?
 
Ndio maana vijana mnawahi kupaata vitambi vinavyoambatana na visukari na mapresha juu.......hamtaki kabisa kuhangaisha miili yenu.....hata jambo dogo kama hilo nalo unataka ufanyiwe na mashine.........
Tukio ambalo halichukui hata masaa mawili kati ya masaa 24.....tena unalifanya huku unalifurahia ikiwa umaridadi ni sehemu ya maisha yako......
 
We nunua yeyote ile. Nina ka Mchina langu ka kg 7 tangu 2010 kanapiga mzigo. Ukipata ile nyenye tub mbili yaani ya kufulia na ya kukaushia, itakusaidia sana, hasa msimu wa mvua.
 
Mdau, je mashine yako inapausha nguo? Kwasababu nguo za kupeleka kufuliwa kwenye maduka ya dry cleaners huwa zinapauka ingawa pia wanatumia mashine?
sheria ya kufua ni ile ile hata ukitumia mashine kama nguo inachuja hata kwenye mashine itachuja, inatakiwa pia kwenye mashine unazieka tofauti tofauti nguo nyeupe zinafuliwa kivyake, majeans yanayochuja kivyake nk

pia kama unatumia mashine kufulia tu halafu unasuuza na maji ya kawaida na kuanika nguo hazichakai ila ule upande wa kukaushia unaweza kuchakaza nguo mapema.
 
Back
Top Bottom