Masokotz
JF-Expert Member
- Nov 26, 2018
- 3,490
- 5,525
Sote tumewahi kufanya makosa na tunafahamu jinsi hisia ya ukosefu inavyouma. Hii hali ya kujisikia kwamba una hatia ni moja kati ya hisia zenye maumivu makali sana. Pamoja na ukweli huo lakini bado maumivu hayo hayafikii maamuzi anayopata yule uliyemkosea hasa pale anapokataa kusamehe.
Mtu anapofanyiiwa kosa huwa na uchungu mkubwa sana moyoni. Hudhilika na kuumia sana kwa yale aliyofanyiwa. Maumivu ya kutendewa kosa ni maumivu makali sana. Jaribu kufikiri maumivu unayopata unapoonewa au kutendewa jambo baya na mtu uliyamuamini na kumthamini utaelewa ukubwa wa maumivu haya.
Maumivu ya kutenda au kutendewa jamo baya huwa yana tiba moja tu. MSAMAHA sio kujifanya hujui, sio kujificha, sio kukimbia wala sio kukana hapana ni MSAMAHA-FORGIVENESS
Msamaha una mambo mengi sana ila kubwa kabisa ni kwamba MSAMAHA una NGUVU kubwa sana. MSAMAHA unakupa uhuru,amani na utulivu. Msamaha unakupa nafasi ya kuendelea na maisha yako. Msamaha unakupa nafasi ya kujenga mahusiano mapya. Msamaha unakupa mwanga mpya. MSAMAHA unakufungulia BARAKA.
Ukweli ni kwamba Aliyefanyiwa kosa huwa ndiye anafaidi zaidi pale anapotoa msamaha na siyo aliyetenda.ALiyetenda bado atabaki na deni kwani kutoa msamaha ni process ndefu ila kuomba msamaha ni process ndefu zaidi.
Mtu anapoomba msamaha anakuwa anajaribu kutua mzigo na Unapomsamehe unakuwa umemtwisha na mzigo wako ili aubebe yeye. Yaani ni kama mtu kakukuta na ndoo ya maji kichwani na yeye ana yake kisha ukachukua ndoo moja kubwa ukajaza maji yenu wote ukampa abebe na wewe ukachukua ndoo tupu mbili ukabeba wewe. Hiyo ndio nguvu ya Msamaha. Mtu akikukosea muonye na akiomba msamaha msamehe. Usikubali kubeba mizigo ya watu.
Kuna wale ambao huwa hawaombi msamaha kabisa. Hao wewe waambie ukweli kwamba wamekukosea na uwape msamaha wa bure kabisa kwani hakuna sababu ya kubeba uchafu kwenye nafsi yako.
Msamaha ni muhimu kwa afya yako ya kihisia, kiakili na kimwili.
Nakutakia siku njema
Mtu anapofanyiiwa kosa huwa na uchungu mkubwa sana moyoni. Hudhilika na kuumia sana kwa yale aliyofanyiwa. Maumivu ya kutendewa kosa ni maumivu makali sana. Jaribu kufikiri maumivu unayopata unapoonewa au kutendewa jambo baya na mtu uliyamuamini na kumthamini utaelewa ukubwa wa maumivu haya.
Maumivu ya kutenda au kutendewa jamo baya huwa yana tiba moja tu. MSAMAHA sio kujifanya hujui, sio kujificha, sio kukimbia wala sio kukana hapana ni MSAMAHA-FORGIVENESS
Msamaha una mambo mengi sana ila kubwa kabisa ni kwamba MSAMAHA una NGUVU kubwa sana. MSAMAHA unakupa uhuru,amani na utulivu. Msamaha unakupa nafasi ya kuendelea na maisha yako. Msamaha unakupa nafasi ya kujenga mahusiano mapya. Msamaha unakupa mwanga mpya. MSAMAHA unakufungulia BARAKA.
Ukweli ni kwamba Aliyefanyiwa kosa huwa ndiye anafaidi zaidi pale anapotoa msamaha na siyo aliyetenda.ALiyetenda bado atabaki na deni kwani kutoa msamaha ni process ndefu ila kuomba msamaha ni process ndefu zaidi.
Mtu anapoomba msamaha anakuwa anajaribu kutua mzigo na Unapomsamehe unakuwa umemtwisha na mzigo wako ili aubebe yeye. Yaani ni kama mtu kakukuta na ndoo ya maji kichwani na yeye ana yake kisha ukachukua ndoo moja kubwa ukajaza maji yenu wote ukampa abebe na wewe ukachukua ndoo tupu mbili ukabeba wewe. Hiyo ndio nguvu ya Msamaha. Mtu akikukosea muonye na akiomba msamaha msamehe. Usikubali kubeba mizigo ya watu.
Kuna wale ambao huwa hawaombi msamaha kabisa. Hao wewe waambie ukweli kwamba wamekukosea na uwape msamaha wa bure kabisa kwani hakuna sababu ya kubeba uchafu kwenye nafsi yako.
Msamaha ni muhimu kwa afya yako ya kihisia, kiakili na kimwili.
Nakutakia siku njema