Mwiyuzi
JF-Expert Member
- Jun 30, 2011
- 846
- 432
Nakumbuka enzi zile............... siku chache kabla ya sikukuu kama hizi za Krismas na Mwaka Mpya tulikuwa tukiomba kununuliwa nguo za sikukuu. Endapo mzazi asipokununulia basi sikukuu haina maana kwako!
Mimi niliikuwa nikinunuliwa nguo mpya mfano kama wiki moja kabla then.....kufika siku ya siku kuu tayari ilishachafuka kwani nilikuwa nikijiiba na kuijaribu kila mara!
Mama yangu alikuwa akipenda kutununulia nguo ndefu sana eti........hii utakuwa nayo.....yaani umasikini unasababisha mpaka viatu anakununulia oversize........eti utakuwa navyo........basi ni kuweka mavitambaa, sponji ilimradi tu uweze kutembea!!
Siku moja tukiwa kanisani siku ya maombi mchungaji akaruhusu wenye maombi wayataje iliwaombewe.....basi mtoto wa Mchungaji akasimama akasema........naomba mimi naomba maombi ili Mungu anipatie nguo ya sikukuu!!
Vp ninyi hali yenu ili kuwaje kuhusiana na suala zima la nguo za siku kuu?
Mimi niliikuwa nikinunuliwa nguo mpya mfano kama wiki moja kabla then.....kufika siku ya siku kuu tayari ilishachafuka kwani nilikuwa nikijiiba na kuijaribu kila mara!
Mama yangu alikuwa akipenda kutununulia nguo ndefu sana eti........hii utakuwa nayo.....yaani umasikini unasababisha mpaka viatu anakununulia oversize........eti utakuwa navyo........basi ni kuweka mavitambaa, sponji ilimradi tu uweze kutembea!!
Siku moja tukiwa kanisani siku ya maombi mchungaji akaruhusu wenye maombi wayataje iliwaombewe.....basi mtoto wa Mchungaji akasimama akasema........naomba mimi naomba maombi ili Mungu anipatie nguo ya sikukuu!!
Vp ninyi hali yenu ili kuwaje kuhusiana na suala zima la nguo za siku kuu?