NDUGU zangu ,
Wahehe wana msemo; Isenga imbofu na isenga indenyeefu. Kwamba ng'ombe kipofu ni sawa tu na ng'ombe aliyevunjika mguu. Wote watakufa njaa.
Ng'ombe kipofu hawezi kuyaona majani, na yule aliyevunjika mguu naye hawezi kujikokota kwenda kutafuta nyasi za kula.
Tunavyoenenda kama jamii wakati mwingine ni sawa na ng'ombe kipofu na yule aliyevunjika mguu. Unaweza kuliona hilo nyumbani kwako, katika ukoo wako, na hata mahala pako pa kazi.
Tumekuwa jamii ya ovyo ovyo. Tunafanya mambo ya ovyo ovyo. Ni kutoka ngazi ya familia hadi ngazi ya kitaifa.
Tubadilike. Na hilo Ni Neno Fupi La Usiku Huu.
Maggid Mjengwa,
Wahehe wana msemo; Isenga imbofu na isenga indenyeefu. Kwamba ng'ombe kipofu ni sawa tu na ng'ombe aliyevunjika mguu. Wote watakufa njaa.
Ng'ombe kipofu hawezi kuyaona majani, na yule aliyevunjika mguu naye hawezi kujikokota kwenda kutafuta nyasi za kula.
Tunavyoenenda kama jamii wakati mwingine ni sawa na ng'ombe kipofu na yule aliyevunjika mguu. Unaweza kuliona hilo nyumbani kwako, katika ukoo wako, na hata mahala pako pa kazi.
Tumekuwa jamii ya ovyo ovyo. Tunafanya mambo ya ovyo ovyo. Ni kutoka ngazi ya familia hadi ngazi ya kitaifa.
Tubadilike. Na hilo Ni Neno Fupi La Usiku Huu.
Maggid Mjengwa,