NGARA ni Tanzania ama?

NGARA ni Tanzania ama?

naungana na mleta mada mi nimesoma ngara sekondari ya rulenge kule hata kiswahili hawajui na ukienda madukani kumejaa bidhaa za burundi tu hata sura zao ni za kiburundiburundi na rwanda kule sio tanzania mkoloni alikosea kwani hata kihangaza kinahingiliana na kirundi na kinyarwanda kuliko kihaya ,wahangaza hawasikilizani na kabila lolote tanzania labda waha
we kijijini kwenu wanajua kiswahili?basi kama walikosea nenda kapime vizuri wewe!mbona hamuwasemi wamasi walioko Namanga au wajaluo wa Sirali?sijui mnatumia kitu gani kufikiri siamini kama mnatumia ubongo
 
Wadau,
Tuache masikhara ya kijiografia na tujikite kiuhalisia, wilaya ya NGARA ni Tanzania ama?
Kama ni Tanzania, basi imetelekezwa na warundi/wanyarwanda wamejiotea mizizi na himaya zao,, amini usiamini hakuna tamaduni za kitanzania katika wilaya hiyo, tembelea ujionee
si uongelee kwenu,Ngara panakuhusu nini,ujinga tu ndy unakusumbua,mtu mzima hovyooooo!
 
Wadau,
Tuache masikhara ya kijiografia na tujikite kiuhalisia, wilaya ya NGARA ni Tanzania ama?
Kama ni Tanzania, basi imetelekezwa na warundi/wanyarwanda wamejiotea mizizi na himaya zao,, amini usiamini hakuna tamaduni za kitanzania katika wilaya hiyo, tembelea ujionee
Ngara kwa asili haina tofauti na Rwanda NA Burundi na mashariki ya Congo. Ngara kuna Clan kubwa tatu. Watutsi, wahutu na watwa. Kwahiyo unapowaona watutsi Ngara wapo kwao na kuhusu kuwepo kwa wanyarwanda Ngara na warundi sidhani km ni tatizo so long as wapo kihalali na idara ya uhamiaji ipo kwa ajili hiyo.
 
Wee bi tch unacheza makida makida relini, subiri treni 'ikupitie'
Aliyekwambia mtutsi kwao sio Ngara ni nani? Watawala wa asili wa Ngara unadhani ni Nani kama sio watutsi? Kasome upya historia
 
Ninapoongelea juu ya Ngara sijakurupuka, tembea iwe ni Nyakanazi, Lusahunga, Ngara mjini yenyewe, Rulenge, Rusumo na hata Kabanga sehemu hizo za wilaya hii si sawa na maeneo mengine ya mipakani mwa nchi hii kama ilivyo Tunduma, Namanga, Sirari, Mbamba bay, Mutukula etc
Sasa nipo Ngara, najionea hali ilivyo, kumesheheni wanyarwanda kuliko warundi, vitendo vya kiharamia vimesheheni, huwezi kuendesha gari yako private baada ya saa mbili usiku hata uwepo Ngara mjini, mgeni anajulikana kwa aina ya kiswahili

Ni aghalabu kukuta watu wakiongea kiswahili, hakuna FM radio zaidi ya radio za kinyarwanda tena wakilonga kinyarwanda na ndizo zinazosikika, ipo radio KWIZERA ambayo pia baadhi ya nyakati ilidiriki kutumia kilugha badala ya kiswahili katika utangazaji wake

Ninachoamini, ni eneo ambalo limetelekezwa kiujumla ndio maana hata matukio mengi ya uharamia yamesheheni katika mapori mazito na milima mirefu inayoizunguka wilaya hii ya Ngara

Kwa yeyote, na aitembelee wilaya hiyo ajionee
Kila sehemu ina utaratibu wake na radio Kwizera huwa wanaongea lugha tatu kiswahili Kirundi na kinyarwanda kwa sababu inasikika mpaka Rwanda na Burundi. Na kirundi na kinyarwanda kinashabihiana na kihangaza kwahiyo hakuna kisichoeleweka kwa watu wa ngara
 
mbona povu jingi narudia maeneo niliyo yataja yapo ngara ila kama hujaelewa maana yangu ipo hv kuwa kanda ya ziwa hasa ngara kumekuwa na muingiliano mkubwa wa wagen hata baada ya kufunga kambi za rukore a na b. ngara ni tz ila kichaka cha wagen haram[/QUOTE huwezi kuzuia warundi na wnyarwanda kuingia Ngara kwasababu wanakuja kwa ndg zao cha muhimu utaratibu wa uhamiaji ufuatwe tu otherwise hata kwao watanzania wanaenda
 
Basi kama ingelikuwa sio dermacation za wazungu, Ngara kiuhalisia ingelikwenda Burundi. Full stop!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

Mkuu vipi sehemu inaitwa kyaka....huko jamaa wakule hawajui kiswahili ni kiganda kwa kwenda....vipi kundi hili nalo tuliite vipi?
 
Shida ni nn mi sijaelewa hapo. Utamaduni wa Ngara unakukera?
Hapana, ni ndugu zangu tu wazuri. Ila wako karibu sana na Burundi kwa lugha, kama wahaya walivyokaribu na waganda. Ukimuuliza Mhaya (hasa waziba) anataka kuwa wapi atakwambia Buganda ( siyo Uganda)
 
Mkuu vipi sehemu inaitwa kyaka....huko jamaa wakule hawajui kiswahili ni kiganda kwa kwenda....vipi kundi hili nalo tuliite vipi?
Hao wanaitwa BagandaKyaka- wanakuwa na wanajihisi wao ni waganda ila walitenganishwa na mipaka. Ni kweli Kiswahili hawajui, mpaka mtu afundishwa shuleni!
 
Ninapoongelea juu ya Ngara sijakurupuka, tembea iwe ni Nyakanazi, Lusahunga, Ngara mjini yenyewe, Rulenge, Rusumo na hata Kabanga sehemu hizo za wilaya hii si sawa na maeneo mengine ya mipakani mwa nchi hii kama ilivyo Tunduma, Namanga, Sirari, Mbamba bay, Mutukula etc
Sasa nipo Ngara, najionea hali ilivyo, kumesheheni wanyarwanda kuliko warundi, vitendo vya kiharamia vimesheheni, huwezi kuendesha gari yako private baada ya saa mbili usiku hata uwepo Ngara mjini, mgeni anajulikana kwa aina ya kiswahili

Ni aghalabu kukuta watu wakiongea kiswahili, hakuna FM radio zaidi ya radio za kinyarwanda tena wakilonga kinyarwanda na ndizo zinazosikika, ipo radio KWIZERA ambayo pia baadhi ya nyakati ilidiriki kutumia kilugha badala ya kiswahili katika utangazaji wake

Ninachoamini, ni eneo ambalo limetelekezwa kiujumla ndio maana hata matukio mengi ya uharamia yamesheheni katika mapori mazito na milima mirefu inayoizunguka wilaya hii ya Ngara

Kwa yeyote, na aitembelee wilaya hiyo ajionee
Haya usemayo yapo sana, nimekaa sana national housing pale.

Wanyarwanda ni wengi mno na wengine wanafanya kazi hadi kwenye taasisi kubwa tu.
 
Unakereka nini? Si ndiyo kuimarisha Jumuiya ya Afrika ya Mashariki, Warundi na Wanyarwanda hoyeeeeee! It is too late maana wilaya za Sengerema na za mkoa wa Geita wamejaa, wananunua mashamba kama hawana akili nzuri, wameleta ng'ombe maelfu kwa maelfu na sasa ili tupate kura kwenye chama chetu, baadhi ni viongozi wa CCM. Tunadeal na watu wenye uraia wa nchi mbili
 
Unakereka nini? Si ndiyo kuimarisha Jumuiya ya Afrika ya Mashariki, Warundi na Wanyarwanda hoyeeeeee! It is too late maana wilaya za Sengerema na za mkoa wa Geita wamejaa, wananunua mashamba kama hawana akili nzuri, wameleta ng'ombe maelfu kwa maelfu na sasa ili tupate kura kwenye chama chetu, baadhi ni viongozi wa CCM. Tunadeal na watu wenye uraia wa nchi mbili
Kuna jamaa mmoja aliwahi Kua RPC Iringa kama sijasahau, siku moja nimeenda Rwanda nikashangaa ana walinzi kama 10 hivi wamemzunguka kumbe amekua sijui general.
 
Back
Top Bottom