PARAPANDA...
Lyrics1:
NYERERE:Karibu Mzee kingunge,kwenye makazi ya milele
Mi huku na mji wangu,tayari unaitwa Nyerere
Nimeshtuka kukuona huku,nini chanzo cha msiba?
KINGUNGE:Ni mipango ya mungu,na nmekumiss swahiba
NYERERE:Vipi nchi yangu mtawala ni chama gani?
KINGUNGE:Bado CCM ingawa kuna upinzani
NYERERE: Unamaana gani,kwani Rais ni nani?
KINGUNGE:Rais ni John,ndo anaongoza usukani
NYERERE: John Mallecela?
KINGUNGE:No, Magufuli, ulimwacha mbunge wa chato sijui unamkumbuka vizuri?
NYERERE: Aaah! ngoja kwanza,unajua haya mambo haya,
Mi nlidhani alipotoka Mkapa angefata Jakaya
KINGUNGE:Jakaya alitawala,akaja akaretire
Nimeacha mambo mengi,yani mambo ni moto, mambo ni fire
NYERERE: Aa'aaa! mbona naskia mambo si sawa
Na ni akina nani wanaojiita hawa,ambao wanajiita ukawa?
KINGUNGE:Ni wapinzani waloungana, lakini hawakumshinda magu
Wengine chama walihama,na bado wakapata tabu (sana)
Kakomesha ufisadi,kaongeza ukusanyaji kodi,hakika wamepata mkombozi ambae atawafikisha nchi ya ahadi
NYERERE: Niliskia skuizi bunge halioneshwi kwenye TV
Inamaana hoja za viongozi wananchi hawaziskii
Mitandao ya kijamii je? vipi inasaidia?
KINGUNGE: Kuna dada anaitwa Mange,please hide my ID
Lyrics2:
NYERERE: Je vipi kaburi langu,tayari wamelijengea?
Na vipi kuhusu mke wangu,Maria wanamtembelea?
KINGUNGE: Kuhusu kumtembelea, hilo toa shaka
Wanamjali na kumlea,tena kwa heshima ya mamlaka
NYERERE: Nimemuona shemeji yangu,ama kweli mnapendana
Penzi la kweli kufa na kuzikana
Vipi mwanangu Makongoro,analinda mali zangu?
KINGUNGE:Bora wakwako mwenzie yupo busy na Tunda
Hivi Julias ulikua simba au yanga?
NYERERE: Kiukweli niliipenda yanga, ila simba ni kisanga
KINGUNGE:hahaa! mwalimu unajua hadi kisanga
NYERERE: Acha hilo naskia mengi, kibamia hadi kudanga
KINGUNGE: HahaHAa
NYERERE:Namuona komba huku,nyimbo za chama anatunga nani?
KINGUNGE:Mi naskia wataisoma namba ila sijui ametunga nani?
NYERERE: Sijakuelewa kwani anaesimamia baraza nani?
KINGUNGE: lipo baraza ila wasanii wanaishi uani
Chorus
Wanamiliki vicent,
Mambo yamebuma mipango haielewekii
Kuna manabii fekii,Ramani hakuna kila kitu hakielewekii
Parapanda italia parapanda
Parapanda italia parapanda
Lyrics3:
NYERERE: vipi kuhusu muungano upo au umechuja?
KINGUNGE: Mpemba anauza kariakoo, mzaramo anamiliki duka unguja
NYERERE:vUjinga, Maradhi, Umaskinu bado maadui wataifa? nipe taarifa
KINGUNGE: Ujinga angalau, hao wengine janga la taifa
NYERERE: Kuhusu barabara?
KINGUNGE: zipo
NYERERE: Madaraja?
KINGUNGE: Yapo
NYERERE: kama ni hivyo uchumi umepanda
KINGUNGE: Wanadai cherehani mbili ukiwanazo ni kiwanda
Vyuma bado vipo still na hospitali hakuna vitanda
NYERERE: Bado nina maswali mengi vipi mwenendo wa katiba
KINGUNGE: Mchakato waliusitisha inasemekana walimpiga
NYERERE: Walimpiga nani? na ni akina nani,na ni nini alifanya?
KINGUNGE: Mwalimu sijui ila ni watu wasiojulikana
NYERERE: walompiga risasi Lissu?
KINGUNGE: ni watu wasiojulikana
NYERERE:na ni akina nani waliomteka Roma?
KINGUNGE: ni watu wasiojulikana
NYERERE: na wanaoteka waandishi wa habari
KINGUNGE: E eeh!sijui ni watu wasiojulikana, hahahaa..